Rais Kenyatta aruhusu Watanzania kuanza kufanya kazi na biashara Kenya bila kuwa na Work Permit wala Business visa

Hamna ubaya ila wakenya wakijazana tigo, voda na airtel wakaja TPB, NMB na CRDB wadogo zenu wote watakuwa wauza kashata na kutembeza kahawa! Msije kuanza kulia lia tu wakenya wamezidi
Mama mjanja,hajaongelea kabisa mambo ya ajira,amesisitiza kwenye biashara tu 😀
 
ni kweli mkuu..
lengo lake ni tanzania iseme the same, ili pia waje wafanye biashr upande wa pili bila permit..

na sisi tukifuata hilo, wakenya watakuwa wame win
Ndio mjiandae kisaikolojia. Kuna maduka ukiingia yani wanakudharau Sana, ukiuliza TV samsung inchi 42 sh. Ngapi ? Utasikia aaah! Hiyo bei maelewano kwani wewe una sh. Ngapi? Kumbe anakudharau anajua huna hela. Hata kwenye ofisi za Umma wabongo dharau Sana. Ngoja tulare changamoto
 
Nafikri wafanya biashara na wakulima wa Tz watanfuaika huko KE, na wa KE watanufaika kwa uwekezaji na kuuza bidhaa zao TZ .. lakini kuhusu ajira sijajua maana ajira bongo ni finyu kidogo .. na malipo ya mshahara yatawanufaisha kuliko huko KE
.?
Screenshot_20210506-041355_Brave.jpg
 
Piga kelele kwa Kenyatta akee😁😁😁😁😁😁

Seriously, EA hatutakiwi kuwa na barrier zozote za kibiashara. Tuna custom union ya maneno tu lakini haifanyi kazi. Tunazuia na kubania biashara za Kenya huku tukijaza masoko kwa bidhaa za India na China. EA inatakiwa kufunguka, iwe kama nchi moja. Hapo ndiyo tunaweza fikia shirikisho la kisiasa
Amaaaaa baaaaaa aaaaaae subutuuuuu Kina Museveni je?bado sana
 
Watanzania wenyewe hizo fursa azitutoshi,wabaki huko kwao,bado hatujafikia uchumi wa kugawana fursa 50-50 na mataifa mengine
Zipo kibao hebu ona kukanga chips kuku tu ni fursa ambayo wala watanzania hatujaweza kuijaza ndio maana wakaletwa STEERS kama wawekezaji waje kukaanga chips kuku
 
Nafikri wafanya biashara na wakulima wa Tz watanfuaika huko KE, na wa KE watanufaika kwa uwekezaji na kuuza bidhaa zao TZ .. lakini kuhusu ajira sijajua maana ajira bongo ni finyu kidogo .. na malipo ya mshahara yatawanufaisha kuliko huko KE
Uwekezaji huenda na ajira sasa Mwekezaji akija atasimama na pesa zake barabarani? Akifungua biashara atatoa ajira

Analyisis nyingi zinazofanywa na wanaijiita wasomi humu ziko chini ya kiwango tena mno !!! eti ohhh turusu waje kufanya biashara na kuwekeza ila ajira nooo!!! Hata sielewi wanachoongea.Sababu hata wakileta mizigo yao ya biashara na malori kuna ajira za vibarua wanatoa kwa watanzania za kupakua hiyo mizigo kuingiza madukani

Wakiwekeza kiwanda ajira zitakuwepo wataletana hata 10 sawa kampuni ni ya kwao sio ya serikali na mitaji pesa yote yao sio yetu lakini wataajiri wengine watanzania hata kama ni vyeo vya chini lakini wataajiri.Something is better than nothing je ni heri mtu akae nyumbani bila ajira au apate mwekezaji amwajiri hata cheo cha chini?

atanzania pia ni vizuri kuondokana na mentality kuwa mtu akija akaanzisha kampuni lake lazima watanzania waajiriwe nafasi za juu sio lazima mitaji yake ana uhuru kuweka watu wake sisi chetu kikubwa kodi na ajira zingine atakazotoa

Na hakuna mwekezaji aweza kubali kujaza watu wake watupu shida ikitokea anakuwa mgeni wa nani ? uwekezaji ni siasa pia hasa mkubwa.Ukimtuma mswahili akaongee na mswahili mwenzie ofisa wa serikali kuhusu issue fulani ya business waweza elewana haraka kuliko mgeni nk
 
Nzuri hio Mr Kenyatta.Arusha, Tanga, Kilimanjaro,Mwanza imejengwa na pesa toka kenya.
Uko sahihi mikoa mingine kama Dar es salaam nk wahindi na waarabu ndio wameijenga.Hiyo mikoa imejenga kupitia pesa za kenya na wafanyabiashara wakenya na hadi sasa uchumi wake mkubwa ni uchumi kenya.Wakenya wamewekeza sana mikoa hiyo na watu wa mikoa hiyo wanafanya biashara sana na Kenya

Pia kuna ubia mwingi wa biashara nyingi kati ya watanzania na wakenya.ZIngine hadi zimeandikwa majina ya watanzania lakini wamiliki ni wakenya.Wakenya ukiaminiana nao wako Tayari kukuachia pesa na Biashara uendeshe kwa niaba yao

Mimi ni mmojawapo nilishawahi kuwa Kenya nikapata fursa ya kupeleka ngozi za Ng`ombe mbichi Kenya.Sikuwa na mtaji akaniambia hakuna shida atatoa nimpe tu akaunti namba .Nikamwambia subiri kwanza nikafanye utafiti wa zinakopatikana na kiasi alikuwa akitaka nyingi.Nikazunguka kwenye machinjio ya ngombe nikakuta kuna wajanja watanzania walishawahi hiyo fursa siku nyingi wanapeleka Kenya.Nikamwambia nimeshindwa mimi .Hakuamini akadhani ni uvivu wangu tu akasema mbona wengi wanatoa huko wanasema zipo kibao? Akaja mwenyewe tukazunguka naye akakubali kuwa ni kweli

Wakenya kwenye business wako vizuri na hupenda sana ubia pia.Biashara kwao ni kama family business wanahitaji wakuamini kwanza kabla ya kuku take into their family .Watanzania wengine subira hawana wanataka from day one awe CEO wa kampuni ya MKenya!!! OOH ni haki yangu hapa ni nchini kwangu!!! Haiendi hivyo
 
Bora Uhuru ni binadamu sn na kiongozi bora kabisa kuwahi kutokea Africa, shida walishindwa na Dikteta, mama kaona atakuwa Mwalimu mzuri sn
Shida watu hamjui historia ya Kenya na Tanzania. Kutokuelewana wakenya na watanzania hasa kiserikali hakujaanza leo. Wakati wa Nyerere kulikuwa na hiyo vita ya maneno. Hadi kuitana majina. Nyang'au n.k.
Kenya siku zote wanaitamani ardhi ya Tanzania. Na uchumi wa Kenya adilimia 8 huko mikononi mwa matajiri wwachache hasa wazungu.
Hivyo Kenya wanataka kutumia hyo oen market ili waweze kufaidi maliasili za Tanzania. Na product zao wataandika made in Kenya, wakati viwanda vitakuwa Tanzania.
Nimeishi Kenya toka utoto. Ni watu wsnao jivunia nchi yao. Si kama sisi watanzania. Kenya awawasemi na kuwatukana ovyo viongozi wao. Watatofautiana lkn bado wataipenda nchi yao na kuisifia. Ni tofauti na watanzania. Wanao jidharau na kusifia nchi nyingine.
Subirini wskenya waje. Muanze kulalamika tena.
 
Uko sahihi mikoa mingine kama Dar es salaam nk wahindi na waarabu ndio wameijenga.Hiyo mikoa imejenga kupitia pesa za kenya na wafanyabiashara wakenya na hadi sasa uchumi wake mkubwa ni uchumi kenya.Wakenya wamewekeza sana mikoa hiyo na watu wa mikoa hiyo wanafanya biashara sana na Kenya

Pia kuna ubia mwingi wa biashara nyingi kati ya watanzania na wakenya.ZIngine hadi zimeandikwa majina ya watanzania lakini wamiliki ni wakenya.Wakenya ukiaminiana nao wako Tayari kukuachia pesa na Biashara uendeshe kwa niaba yao

Mimi ni mmojawapo nilishawahi kuwa Kenya nikapata fursa ya kupeleka ngozi za Ng`ombe mbichi Kenya.Sikuwa na mtaji akaniambia hakuna shida atatoa nimpe tu akaunti namba .Nikamwambia subiri kwanza nikafanye utafiti wa zinakopatikana na kiasi alikuwa akitaka nyingi.Nikazunguka kwenye machinjio ya ngombe nikakuta kuna wajanja watanzania walishawahi hiyo fursa siku nyingi wanapeleka Kenya.Nikamwambia nimeshindwa mimi .Hakuamini akadhani ni uvivu wangu tu akasema mbona wengi wanatoa huko wanasema zipo kibao? Akaja mwenyewe tukazunguka naye akakubali kuwa ni kweli

Wakenya kwenye business wako vizuri na hupenda sana ubia pia.Biashara kwao ni kama family business wanahitaji wakuamini kwanza kabla ya kuku take into their family .Watanzania wengine subira hawana wanataka from day one awe CEO wa kampuni ya MKenya!!! OOH ni haki yangu hapa ni nchini kwangu!!! Haiendi hivyo
Hao waarabu na wahindi wengi ni wazawa wa toka Tanganyika. Angalia wafanya biashara wakubwa wengi ni Watanzania. Dar haijajengwa na wakenya. Acha kusifia vitu visivyo. Dar imejengwa na serikali hasa. Angalia majengo makubwa, miundo mbinu. Utakuta ni serikali na taasisi zake. Uwekezaji mwingine ni watu binafsi watanzania. Wakenya uvuna na kupeleka kwao.
Unaongea mambo ya ngozi. Ni kosa kubwa tunafanya. Tunachukua malighafi zetu tunauza Kenya. Huu ni ujinga kwani wapatao faida ni wakenya siyo sisi. Wao wanachakata hizo ngozi na kuwa na thamani kisha wanatengeneza bidhaa. Inakuwa na thamani zaidi. Kuliko sie tunao uza ngozi.
Enzi za mwalimu Nyerere ngozi zote ziliuzwa katika mamlaka yangozi nchini. Kisha zilipelekwa viwandani. Huko tulipata bidhaa kama viatu kutoka Bora. Vilikuwa vizuri. Hatukuingiza toka nje. Lakini tukauwa viwanda vya ngozi. Tukauwa Bora. Ethiopia hawauzi ngozi nje. Wanaviwanda vikubwa na vidogo. Wanazalisha viatu, mabegi, majaketi n.k.
Tunabaki kusifia wakenya.
Watanzania tumeuwa uchumi wetu. Nyerere kwa wati huo aliweza somesha watu bure anzia chekechea hadi chuo kukuu. Wanafunzi kuanzia sekondari walisafirishwa na serikali. Madaftari na kalamu zilitolewa na serikali. Kila mkoa ulikuwa na mabasi yake. Kulikuwa na maduka ya serikali. Mfano RTC. Matibabu yalikuwa bure. Viongozi hawa wote tulio nao wanesoma enzi za mwalimu bure.
Nimeenda ethiopia bado wana maduka ya serikali. Bado wana mabasi ya umma. Wanafunzi wanakula shuleni. Ethiopia walikuwa wajamaa kama sisi. Viwanda vyao bado vipo. Ndege zao bado zipo toka miaka ya 1935. Kila kitu wanaendesha wao.
Sisi wapi tunakosea? Hatuwezi wategemea wakenya kutukuzia uchumi.
 
Uko sahihi mikoa mingine kama Dar es salaam nk wahindi na waarabu ndio wameijenga.Hiyo mikoa imejenga kupitia pesa za kenya na wafanyabiashara wakenya na hadi sasa uchumi wake mkubwa ni uchumi kenya.Wakenya wamewekeza sana mikoa hiyo na watu wa mikoa hiyo wanafanya biashara sana na Kenya

Pia kuna ubia mwingi wa biashara nyingi kati ya watanzania na wakenya.ZIngine hadi zimeandikwa majina ya watanzania lakini wamiliki ni wakenya.Wakenya ukiaminiana nao wako Tayari kukuachia pesa na Biashara uendeshe kwa niaba yao

Mimi ni mmojawapo nilishawahi kuwa Kenya nikapata fursa ya kupeleka ngozi za Ng`ombe mbichi Kenya.Sikuwa na mtaji akaniambia hakuna shida atatoa nimpe tu akaunti namba .Nikamwambia subiri kwanza nikafanye utafiti wa zinakopatikana na kiasi alikuwa akitaka nyingi.Nikazunguka kwenye machinjio ya ngombe nikakuta kuna wajanja watanzania walishawahi hiyo fursa siku nyingi wanapeleka Kenya.Nikamwambia nimeshindwa mimi .Hakuamini akadhani ni uvivu wangu tu akasema mbona wengi wanatoa huko wanasema zipo kibao? Akaja mwenyewe tukazunguka naye akakubali kuwa ni kweli

Wakenya kwenye business wako vizuri na hupenda sana ubia pia.Biashara kwao ni kama family business wanahitaji wakuamini kwanza kabla ya kuku take into their family .Watanzania wengine subira hawana wanataka from day one awe CEO wa kampuni ya MKenya!!! OOH ni haki yangu hapa ni nchini kwangu!!! Haiendi hivyo
Ila ni wajanja Sana kuwa makini Sana wao kukupiga au kukuzulumu ni dakika sifuri.
 
Nimeenda ethiopia bado wana maduka ya serikali. Bado wana mabasi ya umma. Wanafunzi wanakula shuleni. Ethiopia walikuwa wajamaa kama sisi. Viwanda vyao bado vipo. Ndege zao bado zipo toka miaka ya 1935. Kila kitu wanaendesha wao.
Sisi wapi tunakosea? Hatuwezi wategemea wakenya kutukuzia uchumi.
Kilichoua viwanda vyetu vilikufa sababu moja tulikabidhi watu wasio na elimu kuviendesha.Vilikuwa vimejaa darasa la saba na form four failure kama watendaji tofauti na Ethiopia

Pili Soko la ndani halikuwepo la kutosha ku justify uwepo wa viwanda vyetu.Watu wengi walikuwa maskini wasio na uwezo wa kununua bidhaa zilizozalishwa kwa wingi na viwanda.Hivyo ma godown yakaanza kujaa bidhaa zisizo na soko

Mfano mmoja nilipewa wa kiwanda kiko Pugu road kilikuwa kinaitwa Light SOURCE kilikuwa kinatengeneza balbu .Nyumba zenye umeme zilikuwa chache Tanzania nzima huku kiwanda kinaunguruma usiku na mchana kuzalisha balbu.Zikakosa soko .Mtu akiomba likizo badala ya kulipwa nauli hela taslimu alikuwa anapewa box la balbu zinazolingana na pesa ya nauli yake akauze apate hiyo pesa yake.Wengi walitupa mabox ya Balbu jalalani na kwenda kushtaki vyama vya wafanyakazi kuwa mwajiri anawalipa bidhaa badala ya cash kama sheria ya kazi inavyotaka!!!

Tatu viwanda hivyo bidhaa walizokuwa wakitengeneza hazikuwa za viwango vya kimataifa zilikuwa duni zikawa haziuziki nje sasa machine na spea unaagiza nje wakati bidhaa hazina soko kubwa ndani wala nje.Shida ya pesa za kigeni ikatokea sababu ya mavita ya Uganda nk kwani pesa nyingi zilielekezwa vitani kunua vifaa vya kivita na kugharimia vita miviwanda ikaanza kufa kwa kukosa maintanance na baadaye miviwanda hiyo ikapitwa na teknolojia na hela za kuagiza mitambo ya teknolojia mpya serikali ikawa pesa haina za kigeni ndio miwiwanda ikafa ni si viwanda tu bali kuna hata mashirika ya umma yaliathirika na mabadiliko ya teknolojia kwa kiasi kikubwa mfano kampuni ya simu mitambo yao ya simu na miwaya yao ya nguzo ya simu za majumbani iliathirika baada ya ujio wa teknolojia ya simu za mikononi.Suppliers wenyewe wa Simu za kukoroga kama za kampuni ya Simu yetu kampuni zao zikafa ulaya na marekani baada ya wagunduzi wa teknolojia ya simu za mikononi kuingia sokoni.Na teknolojia ikiingia mpya sokoni bei yake huwa ghali mno au wenyewe hawataki kuiuza wanataka tu kuwekeza wao kama binafsi

Ethiopia bahati yao ni kuwa wao walikuwa na watendaji wazuri na wasomi na stable kwa pesa za kigeni soko la ndani na nje likiwa lipo na bidhaa zao kuwa kwenye viwango vya kimataifa kuanzia Ethiopian Airline nk

Mwisho vilikufa sababu vilikuwa haviendeshwi kibiashara ilikuwa kihuduma zaidi!!! Unakuta viongozi au bodi zimejaa wajumbe wa nyumba kumi ,wanasiasa wa chama tawala na vyama vya wafanyakazi nk watu ambao vichwani kibiashara wako weupe kichwani

Nakumbuka Bodi ya Tanesco mwenyekiti wake alikuwa Mkereketwa wa Tanu darasa la saba!!!
 
Ila ni wajanja Sana kuwa makini Sana wao kukupiga au kukuzulumu ni dakika sifuri.
Sio wote wako wengine matapeli

Kuna mmoja nilipata fursa kuongea naye akanieleza kuhusu biashara ya kupeleka vikapu vya kienyeji vya akina mama USA kwenye soko la AGOA ni mmsai wa Kenya .Vikapu vile vizuri sana.Nikaagiza 20 kwa elfu 15 kila kimoja na sample nikampa akasema hivyo viko tele kenya eneo la NAROK akaniletea kwa basi.Sampuli tuliyokubaliana akaleta kimoja tu vingine vyote kachanganya na makapu mengine ya ajabu ajabu .ANYWAY nilichofanya nikauza kile kimoja kwa dola 100 kwa mzungu mtalii hoteli ya Whitesands Dar es salam.Vingine nikauza kwa elfu 25 kwa shida sana kwa wazungu lakini kwa shida sana

Nikipiga simu akawa hapokei simu baadaye akawa hapatikani hadi leo

Wako baadhi sio wema hata mbinguni kwa Mungu shetani alikuwepo .Duniani si watu wote wazuri hata Kenya na Tanzania ni hivyo hivyo.Hata Mitume si wote wazuri Yesu alikuwa nao 12 lakini alikuwepo mtume Yuda Iscariote Mwizi na msaliti.Ila uwepo wao usitufanye tushindwe kushirikiana na wakenya au kufuata fursa au kuogopa kufanya nao business deals ,Sio wote wako hivyo ni baadhi tena wachache
 
Kilichoua viwanda vyetu vilikufa sababu moja tulikabidhi watu wasio na elimu kuviendesha.Vilikuwa vimejaa darasa la saba na form four failure kama watendaji tofauti na Ethiopia

Pili Soko la ndani halikuwepo la kutosha ku justify uwepo wa viwanda vyetu.Watu wengi walikuwa maskini wasio na uwezo wa kununua bidhaa zilizozalishwa kwa wingi na viwanda.Hivyo ma godown yakaanza kujaa bidhaa zisizo na soko

Mfano mmoja nilipewa wa kiwanda kiko Pugu road kilikuwa kinaitwa Light SOURCE kilikuwa kinatengeneza balbu .Nyumba zenye umeme zilikuwa chache Tanzania nzima huku kiwanda kinaunguruma usiku na mchana kuzalisha balbu.Zikakosa soko .Mtu akiomba likizo badala ya kulipwa nauli hela taslimu alikuwa anapewa box la balbu zinazolingana na pesa ya nauli yake akauze apate hiyo pesa yake.Wengi walitupa mabox ya Balbu jalalani na kwenda kushtaki vyama vya wafanyakazi kuwa mwajiri anawalipa bidhaa badala ya cash kama sheria ya kazi inavyotaka!!!

Tatu viwanda hivyo bidhaa walizokuwa wakitengeneza hazikuwa za viwango vya kimataifa zilikuwa duni zikawa haziuziki nje sasa machine na spea unaagiza nje wakati bidhaa hazina soko kubwa ndani wala nje.Shida ya pesa za kigeni ikatokea sababu ya mavita ya Uganda nk kwani pesa nyingi zilielekezwa vitani kunua vifaa vya kivita na kugharimia vita miviwanda ikaanza kufa kwa kukosa maintanance na baadaye miviwanda hiyo ikapitwa na teknolojia na hela za kuagiza mitambo ya teknolojia mpya serikali ikawa pesa haina za kigeni ndio miwiwanda ikafa ni si viwanda tu bali kuna hata mashirika ya umma yaliathirika na mabadiliko ya teknolojia kwa kiasi kikubwa mfano kampuni ya simu mitambo yao ya simu na miwaya yao ya nguzo ya simu za majumbani iliathirika baada ya ujio wa teknolojia ya simu za mikononi.Suppliers wenyewe wa Simu za kukoroga kama za kampuni ya Simu yetu kampuni zao zikafa ulaya na marekani baada ya wagunduzi wa teknolojia ya simu za mikononi kuingia sokoni.Na teknolojia ikiingia mpya sokoni bei yake huwa ghali mno au wenyewe hawataki kuiuza wanataka tu kuwekeza wao kama binafsi

Ethiopia bahati yao ni kuwa wao walikuwa na watendaji wazuri na wasomi na stable kwa pesa za kigeni soko la ndani na nje likiwa lipo na bidhaa zao kuwa kwenye viwango vya kimataifa kuanzia Ethiopian Airline nk

Mwisho vilikufa sababu vilikuwa haviendeshwi kibiashara ilikuwa kihuduma zaidi!!! Unakuta viongozi au bodi zimejaa wajumbe wa nyumba kumi ,wanasiasa wa chama tawala na vyama vya wafanyakazi nk watu ambao vichwani kibiashara wako weupe kichwani

Nakumbuka Bodi ya Tanesco mwenyekiti wake alikuwa Mkereketwa wa Tanu darasa la saba!!!
Umeongea vema. Lakini nikukumbushe. Wakati wa Nyerere viwanda viliendeshwa na hao hao unao waita darasa la saba. Na walifanikiwa na kulikuwa na soko. Viwanda havikufa wakati wa Nyerere vimekufa wakati wa kubinafsishwa. Lakini pia si kweli kuwa walioendsha viwanda hawakuwa wasomi. Nyerere alisomesha watu. Walisoma ndani na nje ya nchi. Na wengi wa viongozi leo ni hao waliosomeshwa wakati huo.
Si kweli kuwa bidhaa haikuwa ya quality. Nakumbuka mfano kanga za Mutex na vitenge kwa Afrika Mashariki ilikuwa bora vilisafirishwa ndani na nje ya nchi. Bora ilikuwa na viatu bora zaidi. Ni mengi.
Kuhusu soko lilikuwepo. Kwanini wakati wa Nyerere iliwezekana. Viwanda vime kufa wakati wa kubinafsisha.
Ok leo tunawatu wanaelimu kubwa PhD holder na Masters. Nini kinaendelea. Angalia juzi tu mwendokasi inakufa. Hao hao wasomi. Tazama bodi nyingi za serikali zinasimamiwa na maprofesa lakini ni vituko. Wakati wa Nyerere hakikufa kitu japo ni darasa la saba.
Kwa taarifa yako. Ethiopia si kwamba imeendeshwa na wasomi la asha. Ni wananchi wa kawaida tu elimu ya kawaida ila kikubwa wanautaifa na uzalendo.
Elimu ya Ethiopia na Tanzania. Tanzania ipo juu. Ila waethiopia wanajivunia na kuipenda nchi yao. Pia wanahulika kuendeleza kitu au miradi inayoanishwa na viongozi walopita.
Kwa sasa wanajitahidi kusomesha vijana wao nje na kuwarejesha kisha kuwaajiri. Hawana rushwa kukithiri japo ipo.
Kuna kiwanda cha ngozi kilibinafsishwa hakikuendelezwa. Na alie chukua ni msomi tena mhindi maarufu na mfanya biashara mkubwa. Wakati wa nyuma kilifanya kazi vizuri.
Kuhusu soko Ethiopia wananunua bidhaa yao wenyewe kwa soko la ndani. Soko la nje pia. Mfano nilitembelea Ethiopia na rafiki toka nchi moja Ulaya. Karibu kila kituo cha kulelea watoto yatima wanamiradi ya kutengeneza product za ngozi. Wanawashawishi wageni kununua pia wanawapa kwa mkopo wakauze makanisani na kwa watu wengine Ulaya. Pesa ikipatikana wanapewa. Na hivi vituo vinaongozwa na waethiopia wenye elimu ya kwaida tu. Na vituoa vimewekeza. Si Tanzania wanasubiria omba omba.
Leo tuna mawaziri wangapi wenye elimu kubwa. Je kunamafanikio yoyote?
 
Back
Top Bottom