Rais John Magufuli: Nikisema Ukweli, Watanzania Wenye Uchungu Mtalia!!!

asituletee drama tushamchoka kwa akili yake anadhani watanzania hawajui hayo anayolalama nayo kila siku??labda aje sisi tumwambie yanayoendelea ili alie yeye,kiongozi mnafiki huyu
 
Na huu ndio ukweli niko na mtu yuko Bandarini kitengo ananiambia hii ishu itachukua heading DuniA Nzima.. Rais magufuli ni noma asee ndo maana mafisadi wanatumia kila njia kutoa watu kwenye direction. Story nyingi za kujaza junks kichwani. Pumbafu Sana wale wote wasiotakia Mema hii nchi.. Go magufuli go Bravo magufuli.. Ifanye tanzania kuwa taifa la mfano DuniA Nzima

Kwani GSM wamemlipa kiasi gani??
 
Hivi kuna watu wanaamini yaliyotokea bandarini jana ni kweli?

Hisia zangu zinanilazimisha kuamini kuwa hii ilikuwa mpango mahususi wa kufuta headline ya kutumbuliwa kwa Nape na madudu ya Makonda kuvamia Clouds studio. Haya yaliyoonyeshwa kugunduliwa na Rais, yalishagundulika mapema ndio maana hakuagiza waliohusika wachukuliwe hatua.
 
Mwenyezi Mungu alipumzika siku ya saba. Mwanadamu akaona ni muhimu kuwa na mapumziko pia. Shuleni baada ya vipindi kadhaa kunakuwa na pumziko na kunakuwa na likizo baada ya nusu muhula na mwisho wa muhula. Kazini pia kunakuwa na likizo.

Tusipotumia vipindi vya mapumziko kwa makusudio yake akili huchoka mapema. Tusitarajie mapya toka kwa mtu asiyekuwa na likizo.


Kwa maana hiyo unataka rais wetu kipenzi apumzike ili wapuuzi waendelee kula nchi au?
 
izo siasa tu. nape ndio habari ya mjini sasaivi. atakumbukwa daima hata mkileta habari za kubumba.
 
Ukikua utapata uwezo wa kuzielewa threads za watu wazima; but nice try!!!

Watu wazima wapi??Wale wanaofugia Kichwa nywele??Au wale wanaofuga MAJAMBAZI na kuonea wanyonge??Ukiwa na akili unaangalia matendo yako kwanza.

Tumechoka kudanganywa kamdanganye Makonda
 
Hana jipya huyu kila siku kulialia na kulalamika, sasa anamlalamikia nani ikiwa ana mamlaka yote?!! Tunataka uchumi upande na uonekane moja kwa moja kwa wananchi kuwa unapanda na siyo takwimu uchwara tu za kwenye makaratasi. Kama hawezi kazi apishe wenye uwezo wa kuongoza nchi waitumikie.

Rais anatetea jambazi mvamizi na fisadi wa elimu halafu bado mnaleta ngonjera za kumpigia makofi na kumshangilia mtu wa namna hii!!! Huyu kwa nchi yenye watu waliostaarika hakupaswa hata kuwa kiongozi wa mtaa.
Kwahiyo issue ya Clouds na Makonda ndio serious issue....nyingine sio issue.???

Ama kweli kua uyaone
 
anajitetea tu kwa watanzania hakuna jipya, aseme tu ye si anadai msema kweli na ni mpz wa mungu lakini kwa bashite kusema ukweli hana vyeti imekua ngumu na amekubali kuwa mpz wa shetani
 
Hivi hizi ni kazi za Rais kweli? Taasisi zinazopasa kufanya hizi kazi ziko wapi? Kwa nini kama nchi tunaacha mtu mmoja afanye kila kitu? Siku akiugua basi kila kitu kitakuwa mzobemzobe!
 
Gari zimetoka znz zimeshalipiwz tayari zinakuja dar...ni drama juu ya drama hamna kitt..
Na hayo makonten ya mchanga yapo hapo baada kuagiza yasisafirishwe tena....yamekaa hapo tangu wakati ule hayana makosa ..
Tunata asafishe uongozi wake ..analea watu wasio waaminifu..wanatumia vyeti feki na kujitajirisha....
Muda mfupi mtu amekua tajiri ...unamlinda kwa sababu ni msukuma...hapana
 


MY TAKE:

Namshauri Rais wangu apeleke kikosi cha JWTZ chenye silaha mzito pale bandarini!! Aidha, ahakikishe kunakuwa na helikopta za kijeshi zitakazokuwa zinarandaranda eneo la tukio manake asipofanya hivi; siku akirudi tena kwenda kuyafungua, atakuta mabonge ya dhahabu yote yametolewa na kubaki mchanga peke yake!!!!
Kama ni kweli kwa nini yasingefunguliwa leo (jana)?
 
Rais wetu kipenzi, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, jana alifanya yale ambayo huwa anayapatia kweli kweli!!

Kwa kutumia umahiri mkubwa kabisa, bila shaka aki-apply mbinu za kijeshi alizowahi kujifunza JKT, Mheshimiwa Magufuli aliingia bandarini kwa kushitukiza hali iliyowafanya watu wa pale wapigwe butwaa huku wengine mioyo yao ikipiga mkamba kwa sababu hawakutarajia kutokea Mheshimiwa huyo!!!

Mbinu hizi za kijeshi, na bila shaka zikichanganyika na mbinu za kijasusi; zilimwezesha Mheshimiwa Rais wetu aweze kukamata makontena kadhaa yaliyojaa dhahabu!!!

Huku akionekana kujawa na uchungu dhidi ya nchi yake, Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alisema:




Video kwa Hisani ya Comrade William John Malecela. a.k.a Mzee wa Totoz!!!
Mnyetishaji wangu aliwahi kunitumia meseji kuhusu kilichokuwa kinaendelea bandarini na akaniambia wazi kwamba; "...Ndugu yangu chige, kama noma na iwe noma lakini leo ama nipate utajiri kwa kupora donge la dhahabu au nile shaba wakati na-test zari!" Akamalizia kwa kizungu kwamba eti "get rich or die trying!"

Ingawaje mimi ni mtoto wa askari niliyekulia kwenye kota za askari na hivyo nimeanza kuziona bunduki tangia nikiwa mtoto lakini hadi leo nazeeka bado naziogoa sana bunduki!!! Kauli ya mshikaji wangu kwamba, kama vipi poa tu na hata kama kupigwa shaba yupo tayari ni kauli ambayo ilifanya mapigo yangu ya moyo yakaribie kula pozi!

Niliogopa! Nilitishika! Nikajawa na hofu mithili ya mtu aliyekoswa koswa na gari moshi inayosafiri kwa kasi ya umeme!! Hofu yangu ilikuwa kweupe kiasi cha kuweza kuonekana hata na mtu aliyekuwa meta kadhaa kutoka nilipokuwa nimesimama!!

Mapigo yangu ya moyo nayo yalikuwa yanasikika mubashara mithili ya saa mbozi yenye mishale ya chuma chakavu!!!

Kwakweli sikuwa tayari kumpoteza rafiki yangu akiwa bado kijana, kwahiyo, pasi na kupoteza japo sekunde, hapo hapo nikamvutia waya ili aniambie anamaanisha nini kwa kauli yake ile ya kuogofya!!

Baada ya kumpigia simu; bila hofu aliongea kwa kujiamini kabisa: "...chige, kama nilivyokuambia Mheshimiwa kayaotea makontena yenye nyomi la dhahabu! Na ninavyomfahamu Mheshimiwa, huyu bwana hapendi ujinga kwahiyo lazima ataamuru yafunguliwe!!!"

Kwa mbaaaali nikaanza kumwelewa lakini nikajikausha na kuhoji "...Kwahiyo?"

Kuonesha ameamua akajibu: "... Najua makontena yakifunguliwa lazima madonge ya dhahabu yadondoke!! Yakidondoka tu; lazima nidake moja na kujitosa nalo baharini!"

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu; nami taswira ya utajiri ikaanza kunipitia akilini mwangu!! Nikajikuta nimeganda kimyaaa!! Sitikisiki wala sipepesi hadi jamaa aliponigutua na kuhoji eti nasemaje!!!

Sina hakika kama nilijipa muda wa kufikiria japo mara mbili lakini nilijikuta tu nikiropoka: "...Mwana, golden chance never come twice! Test zari na kama vipi, niandae usafiri kabisa ili ukichomoka tu; tupotee mamoja!"

Kwa bahati mbaya, tofauti na mshikaji wangu alivyotaraajia kwamba makontena yaliyojaa dhahabu yatafunguliwa; yakaenda kufunguliwa makontena mengine yenye madudu gani sijui!!!

Sijui ni kwamba funguo za kufungulia makontena yaliyojaa dhahabu zimepotea au vipi!!!

MY TAKE:

Namshauri Rais wangu apeleke kikosi cha JWTZ chenye silaha mzito pale bandarini!! Aidha, ahakikishe kunakuwa na helikopta za kijeshi zitakazokuwa zinarandaranda eneo la tukio manake asipofanya hivi; siku akirudi tena kwenda kuyafungua, atakuta mabonge ya dhahabu yote yametolewa na kubaki mchanga peke yake!!!!

Hivi bado kuna majuha wanamfatilia Sizonje?
 
Ni vizuri hatukatai, lakini yeye ataweza kwenda bandarini every week kufanya hayo? Haisaidi kitu kama hata weka system nzuri, Mkulu inabidi aendene na wakati, Now the problem facing the whole africa is not strong leaders any more, rather Africa needs strong institutions na hili haliwezekani bila ya kuwa na katiba yenye Maono mapya, hi tulionayo inatengeza ufalme kwa rais ** Ndio udikteta wenyewe
 
Back
Top Bottom