Rais John Magufuli: Nikisema Ukweli, Watanzania Wenye Uchungu Mtalia!!!

Chige

JF-Expert Member
Dec 20, 2008
13,497
29,832
Rais wetu kipenzi, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, jana alifanya yale ambayo huwa anayapatia kweli kweli!!

Kwa kutumia umahiri na ustadi wa hali ya juu! Bila shaka aki-apply mbinu za kijeshi alizojifunza JKT, Mheshimiwa Magufuli aliingia bandarini kwa staili ya kushitukiza! Hilo likawafanya wana-bandari wapigwe butwaa huku wengine mioyo yao ikipiga mkamba; puh!

Hawakutarajia ugeni wa Mheshimiwa!!!


Mbinu hizi za kijeshi, na bila shaka zikijumuisha zile za kijasusi; zilimwezesha Mheshimiwa Rais wetu aweze kukamata makontena kadhaa yaliyojaa dhahabu!!!

Huku akionekana kujawa na uchungu kwa nchi yake, Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alisema:
Kwa taarifa nilizonazo, nikizisema hapa mnaweza mkalia! Dhahabu iliyopo humu ndani! Kwa Mtanzania yeyote anayeipenda Tanzania... atalia! Kwa mali zilizomo humu...!
Maneno siyo yangu abadani... huyu hapa:
.
.

Mnyetishaji wangu akawahi kunitumia meseji kuhusu kilichokuwa kinaendelea bandarini na akaniambia wazi kwamba; "...Ndugu yangu chige, kama noma na iwe noma lakini leo ama nipate utajiri kwa kupora donge la dhahabu au nile shaba wakati na-test zari!"

Akamalizia kwa kizungu kwamba eti "get rich or die trying!"

Ingawaje mimi ni mtoto wa askari niliyekulia kwenye kota za askari na hivyo nimeanza kuziona bunduki tangia nikiwa kinda lakini hadi leo nazeeka bado naziogopa sana bunduki!!!

Ikitokea nimekaa na mtu aliyebeba bunduki, ile akianza kuchezea tu kochoo; kochoo... mi huyoooo naondoka zangu!

Wahenga hawakuwa wajinga walipotutahadhalisha kwa kusema "konkoriko mlango wa chuma, ukiufungua hauna huruma!"

Kwa kufahamu hayo, kauli ya mshikaji wangu ilikosa mvuto, si duniani tu bali hadi akhera! Kwamba, kama vipi poa tu na hata kama kupigwa shaba yupo tayari ni kauli ambayo iliyafanya mapigo ya moyo wangu yakaribie kuketi kwenye sofa!

Nikaogopa na kutishika kweli kweli! Nikajawa na hofu mithili ya mtu aliyekoswa koswa kwa gari moshi inayosafiri kwa kasi ya umeme!!

Mapigo ya moyo wangu nayo yakaanza kusikika... puh! Puh! Mithili ya saa mbovu yenye mishale ya chuma chakavu!!!

Sikuwa tayari kumpoteza swahibu yangu akiwa angali bado kijana. Kwahiyo, kwa kuchelea kupoteza japo sekunde ya ziada, hapo hapo nikamvutia waya ili anitabainishie nini maana ya kwa kauli yake ile ya kuogofya!!

Baada ya kumpigia simu; bila hofu aliongea kwa kujiamini kabisa: "...chige, kama nilivyokuambia Mheshimiwa kayaotea makontena kadhaa yenye lumbesa ya dhahabu! Na ninavyomfahamu Mheshimiwa, huyu bwana hapendi ujinga kwahiyo lazima ataamuru yafunguliwe hapa hapa!!!"

Kwa mbaaaali nikaanza kumwelewa lakini nikajifanyisha ujuha na kuhoji "...Kwahiyo?"

Kuonesha ameamua akajibu: "... Najua makontena yakifunguliwa lazima mijidonge ya dhahabu idondoke!! Ikidondoka tu; lazima nianze nalo moja na kujitosa nalo baharini!"

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu; nami taswira ya utajiri ikaanza kunipitia akilini mwangu!! Tamaa ikanijaa! Harufu ya mavumba ikajaa kwenye pua zangu! Nikauona u-Bakhresa huu unanijia kwa kasi ya mwanga!

Nikajikuta nimeganda kimyaaa!! Sitikisiki wala sijongei!! Macho nayo yalishaachana na kibarua cha kupepesa hadi jamaa aliponigutua na kuhoji eti nasemaje!!!

Sina hakika kama nilijipa muda wa kufikiria japo mara mbili lakini nilijikuta tu nikiropoka: "...Mwana, golden chance never come twice! Test zari na kama vipi, niandae usafiri kabisa ili ukichomoka tu; tupotee mamoja!"

Kwa bahati mbaya, tofauti na mshikaji wangu alivyotaraajia kwamba makontena yaliyojaa dhahabu yangefunguliwa; yakaenda kufunguliwa makontena mengine yenye madudu gani sijui!!! Marapurapu si marapurapu; misulupwete si misulupwete... yaani tafrani!

Sijui ni kwamba funguo za kufungulia makontena yaliyojaa dhahabu zimepotea, au makusudi tu!!!

MY TAKE:

Namshauri Rais wangu apeleke kikosi cha JWTZ chenye silaha mzito mzito kama vile vifaru na mizinga pale bandarini ili kuilinda mikontena iliyojazwa midhahabu yetu!!!

Aidha, ahakikishe kunakuwa na helikopta za kijeshi zitakazokuwa zinarandaranda eneo la tukio manake asipofanya hivi; siku akirudi tena kwenda kuyafungua, atakuta mijidonge yote ya dhahabu imebebwa na kubaki na mchanga peke yake usiofaa hata kwa kutengeneza matofali!!


"Akili za mbayuwayu, changanya na zako!"
 
Na huu ndio ukweli niko na mtu yuko Bandarini kitengo ananiambia hii ishu itachukua heading DuniA Nzima.. Rais magufuli ni noma asee ndo maana mafisadi wanatumia kila njia kutoa watu kwenye direction. Story nyingi za kujaza junks kichwani. Pumbafu Sana wale wote wasiotakia Mema hii nchi.. Go magufuli go Bravo magufuli.. Ifanye tanzania kuwa taifa la mfano DuniA Nzima
 
1490334294187.jpg
 
Hana jipya huyu kila siku kulialia na kulalamika, sasa anamlalamikia nani ikiwa ana mamlaka yote?!! Tunataka uchumi upande na uonekane moja kwa moja kwa wananchi kuwa unapanda na siyo takwimu uchwara tu za kwenye makaratasi. Kama hawezi kazi apishe wenye uwezo wa kuongoza nchi waitumikie.

Rais anatetea jambazi mvamizi na fisadi wa elimu halafu bado mnaleta ngonjera za kumpigia makofi na kumshangilia mtu wa namna hii!!! Huyu kwa nchi yenye watu waliostaarika hakupaswa hata kuwa kiongozi wa mtaa.
 
Mimi kwa mtazamo wangu Jana Rais alikuwa anafuta headlines tu kwa wananchi. Kwa sababu yote haya alishayatolea maagizo kwa waziri na ziara za bandarini si baba. Niludhani rais sasa angetoa adhabu kwa hao anaowaagiza halafu hawatekelezi kuliko kutueleza sisi wananchi wake.
 
Rais wetu kipenzi, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, jana alifanya yale ambayo huwa anayapatia kweli kweli!!

Kwa kutumia umahiri mkubwa kabisa, bila shaka aki-apply mbinu za kijeshi alizowahi kujifunza JKT, Mheshimiwa Magufuli aliingia bandarini kwa kushitukiza hali iliyowafanya watu wa pale wapigwe butwaa huku wengine mioyo yao ikipiga mkamba kwa sababu hawakutarajia kutokea Mheshimiwa huyo!!!

Mbinu hizi za kijeshi, na bila shaka zikichanganyika na mbinu za kijasusi; zilimwezesha Mheshimiwa Rais wetu aweze kukamata makontena kadhaa yaliyojaa dhahabu!!!

Huku akionekana kujawa na uchungu dhidi ya nchi yake, Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alisema:


Mnyetishaji wangu aliwahi kunitumia meseji kuhusu kilichokuwa kinaendelea bandarini na akaniambia wazi kwamba; "...Ndugu yangu chige, kama noma na iwe noma lakini leo ama nipate utajiri kwa kupora donge la dhahabu au nile shaba wakati na-test zari!" Akamalizia kwa kizungu kwamba eti "get rich or die trying!"

Ingawaje mimi ni mtoto wa askari niliyekulia kwenye kota za askari na hivyo nimeanza kuziona bunduki tangia nikiwa mtoto lakini hadi leo nazeeka bado naziogoa sana bunduki!!! Kauli ya mshikaji wangu kwamba, kama vipi poa tu na hata kama kupigwa shaba yupo tayari ni kauli ambayo ilifanya mapigo yangu ya moyo yakaribie kula pozi!

Niliogopa! Nilitishika! Nikajawa na hofu mithili ya mtu aliyekoswa koswa na gari moshi inayosafiri kwa kasi ya umeme!! Hofu yangu ilikuwa kweupe kiasi cha kuweza kuonekana hata na mtu aliyekuwa meta kadhaa kutoka nilipokuwa nimesimama!!

Mapigo yangu ya moyo nayo yalikuwa yanasikika mubashara mithili ya saa mbozi yenye mishale ya chuma chakavu!!!

Kwakweli sikuwa tayari kumpoteza rafiki yangu akiwa bado kijana, kwahiyo, pasi na kupoteza japo sekunde, hapo hapo nikamvutia waya ili aniambie anamaanisha nini kwa kauli yake ile ya kuogofya!!

Baada ya kumpigia simu; bila hofu aliongea kwa kujiamini kabisa: "...chige, kama nilivyokuambia Mheshimiwa kayaotea makontena yenye nyomi la dhahabu! Na ninavyomfahamu Mheshimiwa, huyu bwana hapendi ujinga kwahiyo lazima ataamuru yafunguliwe!!!"

Kwa mbaaaali nikaanza kumwelewa lakini nikajikausha na kuhoji "...Kwahiyo?"

Kuonesha ameamua akajibu: "... Najua makontena yakifunguliwa lazima madonge ya dhahabu yadondoke!! Yakidondoka tu; lazima nidake moja na kujitosa nalo baharini!"

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu; nami taswira ya utajiri ikaanza kunipitia akilini mwangu!! Nikajikuta nimeganda kimyaaa!! Sitikisiki wala sipepesi hadi jamaa aliponigutua na kuhoji eti nasemaje!!!

Sina hakika kama nilijipa muda wa kufikiria japo mara mbili lakini nilijikuta tu nikiropoka: "...Mwana, golden chance never come twice! Test zari na kama vipi, niandae usafiri kabisa ili ukichomoka tu; tupotee mamoja!"

Kwa bahati mbaya, tofauti na mshikaji wangu alivyotaraajia kwamba makontena yaliyojaa dhahabu yatafunguliwa; yakaenda kufunguliwa makontena mengine yenye madudu gani sijui!!!

Sijui ni kwamba funguo za kufungulia makontena yaliyojaa dhahabu zimepotea au vipi!!!

MY TAKE:

Namshauri Rais wangu apeleke kikosi cha JWTZ chenye silaha mzito pale bandarini!! Aidha, ahakikishe kunakuwa na helikopta za kijeshi zitakazokuwa zinarandaranda eneo la tukio manake asipofanya hivi; siku akirudi tena kwenda kuyafungua, atakuta mabonge ya dhahabu yote yametolewa na kubaki mchanga peke yake!!!!
Utalia wewe
 
Katika swala LA michanga na madini tatizo ni mikataba mibovu na wa kulaumiwa hapa ni viongozi wa awamu ya Tatu na ya nne. Kuanzia wakuu wa nchi wa wakati huo, wanasheria wao wakuu, mawaziri husika, makamishina wa wakati huo. Hawakuwa wazalendo kwa taifa bali matumbo yao.
 
Rais wetu kipenzi, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, jana alifanya yale ambayo huwa anayapatia kweli kweli!!

Kwa kutumia umahiri mkubwa kabisa, bila shaka aki-apply mbinu za kijeshi alizowahi kujifunza JKT, Mheshimiwa Magufuli aliingia bandarini kwa kushitukiza hali iliyowafanya watu wa pale wapigwe butwaa huku wengine mioyo yao ikipiga mkamba kwa sababu hawakutarajia kutokea Mheshimiwa huyo!!!

Mbinu hizi za kijeshi, na bila shaka zikichanganyika na mbinu za kijasusi; zilimwezesha Mheshimiwa Rais wetu aweze kukamata makontena kadhaa yaliyojaa dhahabu!!!

Huku akionekana kujawa na uchungu dhidi ya nchi yake, Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alisema:


Mnyetishaji wangu aliwahi kunitumia meseji kuhusu kilichokuwa kinaendelea bandarini na akaniambia wazi kwamba; "...Ndugu yangu chige, kama noma na iwe noma lakini leo ama nipate utajiri kwa kupora donge la dhahabu au nile shaba wakati na-test zari!" Akamalizia kwa kizungu kwamba eti "get rich or die trying!"

Ingawaje mimi ni mtoto wa askari niliyekulia kwenye kota za askari na hivyo nimeanza kuziona bunduki tangia nikiwa mtoto lakini hadi leo nazeeka bado naziogoa sana bunduki!!! Kauli ya mshikaji wangu kwamba, kama vipi poa tu na hata kama kupigwa shaba yupo tayari ni kauli ambayo ilifanya mapigo yangu ya moyo yakaribie kula pozi!

Niliogopa! Nilitishika! Nikajawa na hofu mithili ya mtu aliyekoswa koswa na gari moshi inayosafiri kwa kasi ya umeme!! Hofu yangu ilikuwa kweupe kiasi cha kuweza kuonekana hata na mtu aliyekuwa meta kadhaa kutoka nilipokuwa nimesimama!!

Mapigo yangu ya moyo nayo yalikuwa yanasikika mubashara mithili ya saa mbozi yenye mishale ya chuma chakavu!!!

Kwakweli sikuwa tayari kumpoteza rafiki yangu akiwa bado kijana, kwahiyo, pasi na kupoteza japo sekunde, hapo hapo nikamvutia waya ili aniambie anamaanisha nini kwa kauli yake ile ya kuogofya!!

Baada ya kumpigia simu; bila hofu aliongea kwa kujiamini kabisa: "...chige, kama nilivyokuambia Mheshimiwa kayaotea makontena yenye nyomi la dhahabu! Na ninavyomfahamu Mheshimiwa, huyu bwana hapendi ujinga kwahiyo lazima ataamuru yafunguliwe!!!"

Kwa mbaaaali nikaanza kumwelewa lakini nikajikausha na kuhoji "...Kwahiyo?"

Kuonesha ameamua akajibu: "... Najua makontena yakifunguliwa lazima madonge ya dhahabu yadondoke!! Yakidondoka tu; lazima nidake moja na kujitosa nalo baharini!"

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu; nami taswira ya utajiri ikaanza kunipitia akilini mwangu!! Nikajikuta nimeganda kimyaaa!! Sitikisiki wala sipepesi hadi jamaa aliponigutua na kuhoji eti nasemaje!!!

Sina hakika kama nilijipa muda wa kufikiria japo mara mbili lakini nilijikuta tu nikiropoka: "...Mwana, golden chance never come twice! Test zari na kama vipi, niandae usafiri kabisa ili ukichomoka tu; tupotee mamoja!"

Kwa bahati mbaya, tofauti na mshikaji wangu alivyotaraajia kwamba makontena yaliyojaa dhahabu yatafunguliwa; yakaenda kufunguliwa makontena mengine yenye madudu gani sijui!!!

Sijui ni kwamba funguo za kufungulia makontena yaliyojaa dhahabu zimepotea au vipi!!!

MY TAKE:

Namshauri Rais wangu apeleke kikosi cha JWTZ chenye silaha mzito pale bandarini!! Aidha, ahakikishe kunakuwa na helikopta za kijeshi zitakazokuwa zinarandaranda eneo la tukio manake asipofanya hivi; siku akirudi tena kwenda kuyafungua, atakuta mabonge ya dhahabu yote yametolewa na kubaki mchanga peke yake!!!!
Chige tangu lini umekuwa msaidizi wa Msigwa na wewe. Hivi anayevamia ghafla anakuwa na waandishi wa habari? Labda kama tungemuona kwenye footage za CCTV kweli. By the way nini kimemfanya huyo mkuu wa Bandari kuendelea kuwepo? Hana issue huyo, sound tu hizo.
 
Hivi huwa anamlalamikia nani wakati jeshi tumempa, usalama wa taifa tumempa, polisi tumempa, mahakama tumempa hadi magereza tumempa kila nyenzo tumempa sasa anapotulalamikia sisi ana maana gani? Abadilishe katiba sisi tuwe ndio kiongozi mkuu ndio anze kutulalamikia!!! Watanzania tulilamba Garasa kabisa.
 
Back
Top Bottom