Rais amchagua Abdala Mtonga kuwa Internal Auditor General

Rais amchagua Abdala Mtonga kuwa Internal Auditor General

Madcheda

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2009
Posts
423
Reaction score
69
Kuna tetesi zimezagaa kwamba JK amemteua bwana Abdala Mtonga kuwa internal auditor general.

Kama ni kweli nadhani uteuzi wake utakuwa mzuri maana jamaa alikuwa afisa masuhuri wa ofisi ya CAG na pia alikua mkaguzi wa kanda hapo hapo. Ni mtu safi asiyetaka ujinga ujinga kwenye utendaji wa kazi. Tatizo lake ni muoga kufanya maamuzi. Labda anaweza kuleta utofauti kwenye hii ofisi mpya iliyounda

============

Si tetesi tena, ni habari kamili...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemeteua Bw. Mohammed A. Mtonga (52) kuwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali (Internal Auditor General).

Bw. Mtonga ni msomi mwenye Shahada ya Uzamili katika masuala ya Fedha (MSc in Corporate Finance) toka Chuo Kikuu cha Salford nchini uingereza.

Aidha Bw. Mtonga anayo Shahada ya Uhasibu ya CPA (T) inayotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) na Stashada ya Juu ya Uhasibu (Advanced Diploma in Professional Accountancy) toka Chuo cha Jamii Nyegezi ambacho kwa sasa ni Chuo Kikuu cha Mt. Augustine cha Mwanza.

Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mtonga amekuwa na utumishi wa miaka 32 katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Heasabu ambapo amewahi kushika nyadhifa mbalimbali.

Nyadhifa alizowahi kushika Bw. Mtonga ni pamoja na Afisa Masuuli na Mkaguzi wa Hesabu wa Kanda. Pia amewahi kuwa Mkaguzi wa Hesabu Mkazi katika mkoa wa Lindi, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na Makao Makuu ya Jeshi (Ngome).

Uteuzi huu umeanza toka tarehe 06 Aprili, 2011.
 
I am confused...Unasema JK kafanya uamuzi sahihi kumchagua Abdallah maana jamaa ni mtu safi na hataki upuuzi lakini at the same time unasema ni mwoga kufanya maamuzi!!!!!!

Leadership is about making decision na mtu mwoga kufanya maamuzi hafai kuwa kiongozi.

Kama ni kweli Abdallah ni mwoga kufanya maamuzi basi ofisi hii haimfai hata kidogo hata kama angekuwa mwadilifu kama malaika maana kuna wakati itabidi afanye maamuzi mazito na hatayafanya maana ni mwoga. Watu waoga wa kufanya maamuzi huwa wanatakiwa wawe chini ya mtu fulani ili wao wawe wanapokea orders tu na kuzifanyia kazi ili likitokea tatizo aseme boss ndo aliniambia nifanye
 
I am confused...Unasema JK kafanya uamuzi sahihi kumchagua Abdallah maana jamaa ni mtu safi na hataki upuuzi lakini at the same time unasema ni mwoga kufanya maamuzi!!!!!!

Leadership is about making decision na mtu mwoga kufanya maamuzi hafai kuwa kiongozi.

Kama ni kweli Abdallah ni mwoga kufanya maamuzi basi ofisi hii haimfai hata kidogo hata kama angekuwa mwadilifu kama malaika maana kuna wakati itabidi afanye maamuzi mazito na hatayafanya maana ni mwoga. Watu waoga wa kufanya maamuzi huwa wanatakiwa wawe chini ya mtu fulani ili wao wawe wanapokea orders tu na kuzifanyia kazi ili likitokea tatizo aseme boss ndo aliniambia nifanye

Najibu kama kwenye dodoso: Nakubaliana kabisa!
 
I am confused...Unasema JK kafanya uamuzi sahihi kumchagua Abdallah maana jamaa ni mtu safi na hataki upuuzi lakini at the same time unasema ni mwoga kufanya maamuzi!!!!!!

Leadership is about making decision na mtu mwoga kufanya maamuzi hafai kuwa kiongozi.

Kama ni kweli Abdallah ni mwoga kufanya maamuzi basi ofisi hii haimfai hata kidogo hata kama angekuwa mwadilifu kama malaika maana kuna wakati itabidi afanye maamuzi mazito na hatayafanya maana ni mwoga. Watu waoga wa kufanya maamuzi huwa wanatakiwa wawe chini ya mtu fulani ili wao wawe wanapokea orders tu na kuzifanyia kazi ili likitokea tatizo aseme boss ndo aliniambia nifanye

kaka as u kno kila mtu ana mazuri na mapungufu yake,nimesema mazuri yake na mapungufu yake..... bt all in all si mtu mbaya
 
Mwislam Safi, ulamaa aneyejua kazi yake na misingi ya uislam, hongera JK kwa uteuzi huu.

Ondoa dini yake, hii ndio chanzo cha ubaguzi kati ya ndugu zetu waafrika, hizi zote za kuletwa ni chanzo cha kutugawa, Mungu yupo tu, unaweza bila agent hawa washenzi wanaotugombanisha
 
i hope he is the best there is for that position...
 
Tumpe muda afanye kazi ili tuje kumhukumu kwa utendaji wake na sio dini yake
 
Tulieni tupate uhakika, tetesi ni umbea!

Ni uhakika kwamba Ustaadh, Alhaji Abdallah Mtonga ndiye Internal Auditor General. Mimi namfahamu kama mtu mwadilifu na mchapakazi na anaijua kazi yake ya auditing. Anaenda kuanzisha ofisi mpya kwa maana hiyo atakuwa na changamoto nyingi wakati huu wa ufisadi katika ofisi za serikali kuanzi serikali kuu hadi serikali za mitaa.
 
hiyo ni nzuri kwake siku za mwisho, lakini sio Uongozi, maana Umesema ni muoga na hao ndio kikwete anapenda ili hela yetu ichotwe vizuri yeye akiangalia na uoga wake.
ngoja nikwambi sifa kuu ya mtu kama huyo ni mnafiki
na hatufai
ndio maana wewe unasema ni mtu safi, sisi waswahili tunasema ni mtu wa watu.
na taifa alijengwi na viongozi kama yeye, uongozi ni vita mkuu
weupe wanasema
A FRIEND IN POWER IS A FRIEND IN LOSS
KAMA YEYE ANAJIPENDEKEZA KWA KILA MTU BASI HATA KWA MAFISADI ATAJIPENDEKEZA TU.

kaka as u kno kila mtu ana mazuri na mapungufu yake,nimesema mazuri yake na mapungufu yake..... bt all in all si mtu mbaya
 
Who's give power to kikwete to put people any where he want? Constitution Constitution Constitution is only way to stop this joke. These people keep changing offices and screw everything they go and cover their trails, as far as I know why not nominate Ridhiwan to be Minister of Treasure? Thats what kikwete real want...
 
Back
Top Bottom