Ni kupendana tu, maana upendo huleta mambo mengine yote yaliyosalia kama care, attention, wivu mzuri, support, kusaidiana, uaminifu, nk
Kabla sijakupa mauzoefu ya ndoa yangu yenye miaka 47, naomba nikuulize masuali mafupi yafuatayo
1. Umeolewa?
2.Kwanini umeolewa?
3. Umefurahi kuolewa?
4.Kwanini umefurahi?
5.Hujafurahi kuolewa?
6. Kwanini hujafurahi
Nikiangalia hii sredi umeirusha saa tano kasorobo usiku. Kama umeolewa, mzee alikuwa wapi? Kama hujaolewa ulikuwa unawaza nini?
Ahsante kwa kujibu maswali yangu.
Will you marry me?:couch2:
Eiyer you always have brain boy. sasa hapa napata maswali mengine kuwa kumbe ili kuona raha ya ndoa lazima mtu binafsi awe na furaha? je yawezekana mtu kutengenezewa furaha?gfsonwin,hakuna mtu anaeweza kukupa furaha,furaha unayo mwenyewe.Hivyo ndoa haina furaha,lakini furaha ndo hisia ya juu kabisa inayomfanya mwanadamu kujisikia bora,mwenye afya na akiwa na furaha ataiona maana ya maisha.Namna ya kuipata furaha ni kujikubali kama ulivyo na kujitazama na kujipima kwa ubinadamu wako na sio kitu kingine cha nje yako.Ukishapata ridhiko la ndani utaanza kuhisi tofauti na utajiona si mwenye visirani tena.Hapo utaanza kuipata furaha.. . . . Raha ni kitu cha muda,kinakinaisha,hakuna tofauti kati ya raha na utamu.Unapopanda gari zuri au kulala kwenye kitanda kizuri unapata raha,lakini ukishazoea raha huisha. . . . Nikija kwenye swali lako,raha ya ndoa sio kitu kimoja ni vingi,baadhi umeviorodhesha hapo kwenye thread yako,ila navyo hukinai na kuna wakati mtu huiona ndoa haina maana.Yes,unaiona ndoa haina maana kwa sababu wengi kama sio wote tunawekeza kwenye vitu hivyo,tunadhani ndivyo vinamfanya mtu aifurahie ndoa.Badala ya kuwekeza kwenye raha,wekeza kwenye furaha na maswali yako yatapata majibu sahihi!
Mkuu samahani sana, kwani wewe ni jinsia gani? unajua raha ya mema na mabaya? ulishawahi kufanya?.
Je kama una uwezo wa Kununua gari lako mwenyewe au kuazima gari/magari kila wakati kipi bora? yaani kumiriki kifaa chako mwenyewe au kikaa na kifaa cha mtu mwingine kipi bora?. Mia
cacico ma dear umenipa majibu yenye maswali tena hivi kwani wanao wakitimiziwa mahitaji na shangazi au wajomba je itatimiza raha yako? inamaana siku ambayo mumeo hana amani basi kwako raha ya ndoa hakuna?raha yangu kwenye ndoa ni kuwaona watoto wangu wanapata mahitaji yote muhimu! na mume wangu apate amani ya roho in ol aspects, so that we can suport each other in achieving our daily bread and complete th happines we want.
nyumba kubwa wewe nyumba yako umeijenga katika misingi ya urafiki zaid kuliko katika misingi ya mume na huyu mke. manake kuna hatari sana ya kuish katka mazingira ya mume na mke na kuondoa misingi ya urafiki. Mumeo akiwa ni rafiki yako definately utakuwa muwazi kwake na atakuwa your next hand but akibaki na cheo cha mume atakuwa na gap kubwa sana kati yako na hisia zakoa ama uhalisia wako wa kimaisha. nimeipenda sana hiiRaha ya ndoa ni full package. Kuanzia tendo la ndoa, watoto, kugombana kidogo, kufurahi pamoja etc.
Ukinambia unaweza pata furaha au company hata ukiwa kwenu mi nakataa; unless unambie aina ya familia unayotoka watu wapo tu wanakusubili tu kukutoa stress. Mi kwetu mfano wote wameoa na kuolewa hivyo hakuna mwenye muda (wa kutosha) na dada sijuhi kaka bila kumuona intruder.
Lakini mume wangu ndiye kaka, dada, rafiki. Yani maisha yangu ya kazini anayajua ndani nje; hivyo tukikutana jioni naendeleza story tu; basi boss si amekubali ile issue... Basi si nimempa live yule mshenzi... Au unaonaje nikubali au nikatae hiyo proposal... Nina uhakika wa pa kupata second opinion tena genuine, si ya marafiki wanafiki. Mimi na calculate sana nachoongea na so called marafiki; lakini kwa mume wangu najiachia tu kwani siri zangu najua ziko salama.
Kama ndoa ni ya watu wanaopendana; unachopata kwenye ndoa akiwezi kuwa replaced na uhusiano na mtu yeyote, hata mzazi.
Wana mmu polen kwa kazi za kutwa nzima.
haya jamani hebu tuelezane raha ya ndoa ni nini?
je ni mchezo wa matusi tu,
au ni kuish na mtu umpendaye tu
au ni kuwa na familia tu
au ni nini?
hebu tudadavue jamani, manake nashindwa kujua nini hasa raha ya ndoa.
Wana mmu polen kwa kazi za kutwa nzima.
haya jamani hebu tuelezane raha ya ndoa ni nini?
je ni mchezo wa matusi tu,
au ni kuish na mtu umpendaye tu
au ni kuwa na familia tu
au ni nini?
hebu tudadavue jamani, manake nashindwa kujua nini hasa raha ya ndoa.
MI nahisi ivyo vyote hapo juu vinaweza kuleta raha ya ndo kwa kutegemeana
Sijaona raha yoyote ya ndoa zaidi ya kufurahia watoto wangu. Mengine yote kwangu hakuna cha raha wala nini! Kawaida tu.