Wee usiseme hivyo mkuu, kuna siku nimetoka Banana naelekea Tandika ndo nikakamate daladala za Buza kama mida ya saa mbili au tatu usiku hivi, si nikapitiwa na usingizi bana (na nilikuwa nimeshapiga vyombo kidogo ingawa nilikuwa sijalewa sana bado nilikuwa level) sasa ile kukaa seat ya dirishani isiyo na usumbufu wa kupisha pisha watu kushuka na kaupepo mwanana nikachapa usingizi bana. Daladala imefika Tandika sokoni abiria wameshuka na wamepanda wengine daladala imegueza kurudi Banana, sasa nikastuka usingizini nikajiuliza mbona gari haifiki kituoni mbona imetumia muda mrefu hivi (hapo inachapa mwendo), naangalia nje dirishani nashangaa tuko maeneo ya njia panda ya Vingunguti kurudi Banana, sasa najiuliza tulikuwa tunaelekea Tandika imekuwaje gari linarudi nyuma tena. Nikatafakari nikaona hapa nimeshabugi......nikasimama kusogea mbele namwambia konda shusha kituo kinachofuata (jet corner) nilitaka nianze kummaind ila nikaona ataniumbua so nikapiga kimya nikamlipa nauli yake nikashuka na kuvuka upande wa pili wa barabara kusubiri tena gari za kurudi Tandika. Kuanzia siku hiyo nilitia akili.