fimboyaasali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 8,606
- 8,264
Ugoni sio suala la polisi broAisee nyie acheni haya mambo, kutokana kuwa karibu na watu na sehemu niliyopo kuna jamaa kutoka mkoa x alimuwezesha mke wake kufanya biashara fulani kwenda mikoa fulani, baada ya biashara kukua mke kaanza kuleta zarau na kuwa bize sana na safari za huo mkoa.
Basi jamaa katupigia simu na kututumia picha kama yupo hiyo sehemu. Kwa kweli mwanamke ni mzuri sana na kokote anaitaji ulinzi kwa uzuri aliyo nayo.
Sasa jamaa naona kachanganyikiwa na maeneo tuliyopo mke wake anajiachia na mtu.
Jamaa anafunga safari kuja huku!
Nitakuja na mrejesho naelekea duka la vifaa vya magari kununua grisi
**Mrejesho *
Jamaa yupo njiani kutokana na mkoa aliopo anakuja na private car.tunacho fanya kwanza kutafuta polisi wa hayo maeneo na kufungua jarada kabla yote kuanza akifika na kupumzisha ili kesho tuanze na kazi iliyomleta
Mrejesho
Tumeingia hiyo sehemu X kama tulivokusudia tukiwa na jaziba na vilainishi vya mitambo aka gris.
kumbe jamaa kafungiwa rada bwana tokea alipotoka au siri ya kuja kushika ugoni imevuja humu !
Maana itakuwa kapa habari humu.
ila tunacho fanya tuta mtrack maana uwezo tunao labda akimbilie kwa shetani .
tumekamata mzigo anapokwenda kuchukulia ambao mwanamke alipofika.
kwa sasa kesi hipo polisi.
ila jamaa nilikuwa nimemuandalia kopo zima la grisi maana haishi haraka.
tutaendelea .....
Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app