EL ELYON
JF-Expert Member
- Jan 2, 2013
- 1,563
- 1,886
Wakuu mmebarikiwa Sana na Mungu WA Mbinguni hakuna laana.
Wakuu mwaka Fulani ndo nimetoka Tu kwenye majanga ya kugombana na mwanamke niliyekuwa nikiishi Naye na kuzaa Naye mpaka kumuweka ndani Kwa kesi ya uwongo alifuta kabla mambo hayajaharibika. Waha Mungu Anawaona aisee.
Ulipita takribani mwaka na miezi kadhaa nikaamua kutafuta binti WA kuoa sasa bahati nzuri Nina rafiki yangu tunaheshimiana sana aisee ni zaidi ya ndugu tumeshibana hasa kwasasa ni pastor.
Nilimshirikisha adhima yangu ya kutaka mchumba nioe, alifurahi Sana na akaniunga mkono akasema Mambo ya kufungisha ndoa atashughurikia yeye mpaka vyeti.
Basi siku moja akanipgia simu akanishirikisha kuhusu binti mmoja WA kisukuma waliyekuwa wanaishi Naye akanipa sifa zake zote kwamba ni mchapa KAZI Sana kwahiyo hata kama Nina miradi basi atasaidia Sana Ila kubwa nisiangalie uzuri Bali niangalie uchapa KAZI wake na sifa za kuwa mke, japo hili la kutongalia uzuri nilimpinga Sana mpka kubishana maana nilimwambia lazima nimpende Kwa macho Kwanza siwezi oa mtu ambaye sjampenda eti kisa Tu ni mchapa KAZI au eti ana sifa za kuwa mke hapana itanipa shida pia binti WA watu Naye Tampa shida.
Basi nilipata likizo nikaamua kwenda huko aliko rafiki yangu kumsalimia lakini pia kumuona na huyo binti. Kweli nilifika nikamuona binti vizuri Ila sikumpenda na sikutaka onyesha hadharani kwamba sijampenda nilinyamaza Tu uzuri rafiki yangu na mkewe nao hawakuniulza lolote mpaka naondoka maana niliokuwepo pale kama wiki mbili nadhani walijiongeza Tu wenyewe.
Sasa siku moja nilikuwa nimetoka na rafiki yangu akapigiwa simu na mtu mmoja ni mmama wakawa wanaongea kwenye maongezi Yao niligundua wanamzungumzia Yule binti japo mwanzo sikujua maana aliyepiga simu aliulizia mama wawili yupo na rafiki yanga akajibu hayupo alishaondoka kwangu mmmh maongezi yaliendelea ndipo niligundua aliyekuwa anazungumziwa ni Yule binti kumbe ana watoto wawili na yule mama akawa analalamika kwamba Yule binti ana tabia mbaya kwani anatabia ya kuhamisha maneno Sana ni mchonganishi.
Mmmh niliumia Sana kusikia Yule binti ana watoto tena wawili na rafiki yangu kwenye maongezi yetu yote kuhusu sifa za Yule binti hakuwahi nambia ana watoto alifanya Siri yeye na mkewe sijui lengo lilikuwa ni nini.
Niliumia Sana nikajawa na hasira kwanini rafiki yangu alitaka kunifanyia kitendo kisicho cha kawaida kunipa mtu WA kuoa ambaye tayari ana watoto na hajanambia SINA maaana Dada mwenye watoto hafai kuolewa hapana Ila Kila mtu anachagua vile anavyoona.
Alipokata simu nilimuulza kwanini hakuwahi nambia Yule binti alikuwa na watoto nilishangaa sana jibu alilonijibu eti mbona wewe Una mtoto aisee, nikamwambia Mimi kuwa na mtoto si sababu ya Mimi pia kuoa mdada mwenye mtoto na ilitakiwa uniambie kama naridhia maana kama ningempenda nikamuona na nikajaletewa watoto huoni ingeniletea shida Sana hiyo Hali uwenda ndoa ingeingia doa kubwa sana ambalo uwenda yangekuwa mengine jamaa naona alichukulia poa Tu.
Mpaka leo huwa nikikumbuka huwa namshangaa Sana Yule ndugu sjui alikuwa anawaza nini.
Je wakuu mliwahi kumbana na maswahibu kama hili.
Je rafiki Yangu Alikuwa ana nia gani au alikuwa sahihi?
Wakuu mwaka Fulani ndo nimetoka Tu kwenye majanga ya kugombana na mwanamke niliyekuwa nikiishi Naye na kuzaa Naye mpaka kumuweka ndani Kwa kesi ya uwongo alifuta kabla mambo hayajaharibika. Waha Mungu Anawaona aisee.
Ulipita takribani mwaka na miezi kadhaa nikaamua kutafuta binti WA kuoa sasa bahati nzuri Nina rafiki yangu tunaheshimiana sana aisee ni zaidi ya ndugu tumeshibana hasa kwasasa ni pastor.
Nilimshirikisha adhima yangu ya kutaka mchumba nioe, alifurahi Sana na akaniunga mkono akasema Mambo ya kufungisha ndoa atashughurikia yeye mpaka vyeti.
Basi siku moja akanipgia simu akanishirikisha kuhusu binti mmoja WA kisukuma waliyekuwa wanaishi Naye akanipa sifa zake zote kwamba ni mchapa KAZI Sana kwahiyo hata kama Nina miradi basi atasaidia Sana Ila kubwa nisiangalie uzuri Bali niangalie uchapa KAZI wake na sifa za kuwa mke, japo hili la kutongalia uzuri nilimpinga Sana mpka kubishana maana nilimwambia lazima nimpende Kwa macho Kwanza siwezi oa mtu ambaye sjampenda eti kisa Tu ni mchapa KAZI au eti ana sifa za kuwa mke hapana itanipa shida pia binti WA watu Naye Tampa shida.
Basi nilipata likizo nikaamua kwenda huko aliko rafiki yangu kumsalimia lakini pia kumuona na huyo binti. Kweli nilifika nikamuona binti vizuri Ila sikumpenda na sikutaka onyesha hadharani kwamba sijampenda nilinyamaza Tu uzuri rafiki yangu na mkewe nao hawakuniulza lolote mpaka naondoka maana niliokuwepo pale kama wiki mbili nadhani walijiongeza Tu wenyewe.
Sasa siku moja nilikuwa nimetoka na rafiki yangu akapigiwa simu na mtu mmoja ni mmama wakawa wanaongea kwenye maongezi Yao niligundua wanamzungumzia Yule binti japo mwanzo sikujua maana aliyepiga simu aliulizia mama wawili yupo na rafiki yanga akajibu hayupo alishaondoka kwangu mmmh maongezi yaliendelea ndipo niligundua aliyekuwa anazungumziwa ni Yule binti kumbe ana watoto wawili na yule mama akawa analalamika kwamba Yule binti ana tabia mbaya kwani anatabia ya kuhamisha maneno Sana ni mchonganishi.
Mmmh niliumia Sana kusikia Yule binti ana watoto tena wawili na rafiki yangu kwenye maongezi yetu yote kuhusu sifa za Yule binti hakuwahi nambia ana watoto alifanya Siri yeye na mkewe sijui lengo lilikuwa ni nini.
Niliumia Sana nikajawa na hasira kwanini rafiki yangu alitaka kunifanyia kitendo kisicho cha kawaida kunipa mtu WA kuoa ambaye tayari ana watoto na hajanambia SINA maaana Dada mwenye watoto hafai kuolewa hapana Ila Kila mtu anachagua vile anavyoona.
Alipokata simu nilimuulza kwanini hakuwahi nambia Yule binti alikuwa na watoto nilishangaa sana jibu alilonijibu eti mbona wewe Una mtoto aisee, nikamwambia Mimi kuwa na mtoto si sababu ya Mimi pia kuoa mdada mwenye mtoto na ilitakiwa uniambie kama naridhia maana kama ningempenda nikamuona na nikajaletewa watoto huoni ingeniletea shida Sana hiyo Hali uwenda ndoa ingeingia doa kubwa sana ambalo uwenda yangekuwa mengine jamaa naona alichukulia poa Tu.
Mpaka leo huwa nikikumbuka huwa namshangaa Sana Yule ndugu sjui alikuwa anawaza nini.
Je wakuu mliwahi kumbana na maswahibu kama hili.
Je rafiki Yangu Alikuwa ana nia gani au alikuwa sahihi?