TUNASHUKURU KWA TAARIFA.hatahivyo kuna maswali mengi bado tunajiuliza, naomba mwanajamvi yeyote aliye na taarifa atujuze; hawa jamaa hawaaminiki na kila wanapotoa taarifa hadharani kunasalia mambo ambayo hata baada ya wanajamii kujiuliza na kuyabainisha serikali huwa hawatoi ufafanizi makini hadi wanapoumbuka. Tuana mifano mingi lakini hili la mauwaji ya wafanyabiashara wa madini na taxi drive (a.k.a. kesi ya zombe). walipoua hawa jamaa walijinadi wakijaribu kuwashawishi wananchi kuwa wao ni weledi na wanajua hata harufu za kwapa za wahalifu, na kwamba wamefanikiwa kuwa uwa wahalifu (??kazi ya polisi ni kuuwa wahalifu??) Baadae walikuja bainika kuwa polisi ilifanya uporaji na kisha kutumia ubabe dola kufukia nyayo zao mchana kweupe!.
Mauaji ya kipuuzi yametokea tena Arusha, Morogoro na lile la Iringa lililo haribu kila kitu. Maelezo ya msemaji wa jeshi la polisi yamekuwa ni ya kikasuku ya ambayo kwa bahati mbaya hayakutengenezwa kwa makini, YANADHIHIRISHA uongo dola.
!
Kila siku na kila saa ninamuomba Mola aingilie kati hatima ya nchi yetu tunayoipenda ya TANZANIA