Tokyo40
JF-Expert Member
- Jun 16, 2013
- 2,065
- 1,926
View attachment 270372
Chuo cha Birmingham cha Uiingereza, kimetangaza kuwa wana Quran ya iliyoandikwa katika ngozi ya mnyama (parchment) ya wakati wa maisha ya Mtume SAW au miaka michache baada ya kufariki.
Kwa kutumia radiocarbon testing, wamefahamu kuwa Quran Tukufu iliandikwa katika ngozi ya mnyama aliyekuwepo wakati wa uhai wa Mtume SAW na kuandikwa aidha alipokuwa hai au muda mfupi baada ya kifo chake.
David Thomas, Profesa wa dini ya Kiislamu na Kikristo wa Chuo cha Birmingham, alisema kuwa maneno ya Quran waliyoandikwa kwenye ngozi hayana tofauti na Quran ya leo pamoja na Quran iliyo na umri sawa inayohifadhiwa na Bibliotheque Nationale de France huko Paris, Ufaransa.
Profesa huyo akaseka kuwa Quran hii itakuwa imeandikwa baina ya mwaka
AD 568 na AD 645 kwa kutumia utaalam wa "radiocarbon testing" ya Chuo Kikuu cha Oxford na ambao unatoa majibu sahihi ya umri kwa asilimia 95.
Mtume Mohamed SAW alizaliwa mwaka 570, Makka.
source: wsj.com
Chuo cha Birmingham cha Uiingereza, kimetangaza kuwa wana Quran ya iliyoandikwa katika ngozi ya mnyama (parchment) ya wakati wa maisha ya Mtume SAW au miaka michache baada ya kufariki.
Kwa kutumia radiocarbon testing, wamefahamu kuwa Quran Tukufu iliandikwa katika ngozi ya mnyama aliyekuwepo wakati wa uhai wa Mtume SAW na kuandikwa aidha alipokuwa hai au muda mfupi baada ya kifo chake.
David Thomas, Profesa wa dini ya Kiislamu na Kikristo wa Chuo cha Birmingham, alisema kuwa maneno ya Quran waliyoandikwa kwenye ngozi hayana tofauti na Quran ya leo pamoja na Quran iliyo na umri sawa inayohifadhiwa na Bibliotheque Nationale de France huko Paris, Ufaransa.
Profesa huyo akaseka kuwa Quran hii itakuwa imeandikwa baina ya mwaka
AD 568 na AD 645 kwa kutumia utaalam wa "radiocarbon testing" ya Chuo Kikuu cha Oxford na ambao unatoa majibu sahihi ya umri kwa asilimia 95.
Mtume Mohamed SAW alizaliwa mwaka 570, Makka.
source: wsj.com