Annina
JF-Expert Member
- Nov 15, 2009
- 437
- 57
Temu, najua umeudhika na unanilaumu, una haki ya kufanya hivyo. Ndio maana nasisitiza niangaliwe kwa jicho la huruma na unipe upendeleo maalum katika kulimaliza hili. Temu, wewe wajua, mimi najua na wengi wanajua kwamba Annina bila ya wewe maisha hayana thamani. Temu, sijasahau hata kidogo uliponiomba niwe mwenzi wako katika maisha kwa kuwa unaamini bila Annina maisha yako hayajakamilika -sijasahau! Temu siku zote nimekuwa msikivu kwako, tumekuwa tukiishi kwa amani na upendo mkubwa huku tukiwa wavumilivu na wenye subira hasa penye majaribu tukitaraji maisha mema baadae - bado naamini hivyo!
Temu, najua una hasira za mlipuko - waswahili wanasema ndio maumbile yako, nakuhurumia sababu najua unavyoteseka unapokuwa kwenye hali hiyo. Nakuhurumia zaidi sababu nakupenda sana na nisingependa kuona moyo wako ukiwa umetawaliwa na hasira, simanzi na huzuni. Naumia zaidi pale ninapokuwa chanzo cha wewe kuwa kwenye hali hiyo - uniwie radhi.
Temu wangu, ni nini kimekufanya ufikiri mimi Annina ninatumia muda wangu mwingi na JF kuliko ninavyotumia na wewe? Kwamba ninawathamini wachangiaji mbalimbali wa JF nisiowafahamu hata kwa sura kuliko ninavyokuthamini wewe? Temu mpenzi, angalia basi hata idadi ya posti nilizonazo JF labda utagundua kitu tofauti na unachoamini sasa.
Temu mpenzi, tafadhali punguza hasira tujadili hili na tulimalize ili tuboreshe zaidi na zaidi mapenzi yetu. Tumeshapoteza muda mwingi sana kukabiliana na vikwazo na changamoto mbalimbali za maisha, naamini tuna kila sababu ya kufurahia maisha yetu sasa - baada ya dhiki faraja...
Nakupenda kabisa!
Annina
Temu, najua una hasira za mlipuko - waswahili wanasema ndio maumbile yako, nakuhurumia sababu najua unavyoteseka unapokuwa kwenye hali hiyo. Nakuhurumia zaidi sababu nakupenda sana na nisingependa kuona moyo wako ukiwa umetawaliwa na hasira, simanzi na huzuni. Naumia zaidi pale ninapokuwa chanzo cha wewe kuwa kwenye hali hiyo - uniwie radhi.
Temu wangu, ni nini kimekufanya ufikiri mimi Annina ninatumia muda wangu mwingi na JF kuliko ninavyotumia na wewe? Kwamba ninawathamini wachangiaji mbalimbali wa JF nisiowafahamu hata kwa sura kuliko ninavyokuthamini wewe? Temu mpenzi, angalia basi hata idadi ya posti nilizonazo JF labda utagundua kitu tofauti na unachoamini sasa.
Temu mpenzi, tafadhali punguza hasira tujadili hili na tulimalize ili tuboreshe zaidi na zaidi mapenzi yetu. Tumeshapoteza muda mwingi sana kukabiliana na vikwazo na changamoto mbalimbali za maisha, naamini tuna kila sababu ya kufurahia maisha yetu sasa - baada ya dhiki faraja...
Nakupenda kabisa!
Annina