PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

Kwamhuzi

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2014
Posts
1,762
Reaction score
407
Mashirika ya kijamii yamekuwa yakijitangaza kuwa yana huduma bora sana,mashirika haya ikiwa ni pamoja na PSPF.

Shirika hili lilikuwa linasifiwa kuliko mashirika yote ya huduma za kijamii.

Hata hivyo tumeona katika siku hizi za karibuni huduma za shirika hili zikidorora kwa kiwango kikubwa.

Kwa mfano wastahafu ambao walipaswa kulipa pension zao za kila mwezi angalau ilipofika tarehe moja ya mwezi wa nne mpaka leo hawajalipwa stahili yao.

Mashirika haya yakumbuke kwamba wastahafu hawa wanategemea pension hizi kwa kiwango kikubwa kama vile wafanyakazi wanavyotegemea mishahara yao. Na wakumbuke pia kwamba wastahafu hawa wameneemesha sana mashirika haya.

Ni swala la kiutu tu na uungwana kwamba inabidi watambue mchango wao na shirika hili liwe na mpango thabiti wa kuwalipa wazee hawa mapema. Ni watu waliolitumikia shirika hili kwa siku nyingi kwa hiyo ni vema wakaheshimiwa.

Tukiandika andika hivi mwishoni watapoteza wateja.

Wajirekebishe na watekeleze wajibu wao ipasavyo.
 
mbona wanasema hili ndo shirika makini kuliko yote. Haya mashirika hayaaminiki yote
 
Mashirika ya kijamii yamekuwa yakijitangaza kuwa yana huduma bora sana,mashirika haya ikiwa ni pamoja na PSPF.Shirika hili lilikuwa linasiwa kuliko mashirika yote.Hata hivyo tumeona katika siku hizi za karibuni tumeona huduma za shirika hili zikidforora kwa kiwango kikubwa.Kwa mfano wastahafu ambao walipaswa kulipa pension zao za kila mwezi angalau ifikapo tarehe moja ya mwezi wa nne mpaka leo hawajalipwa stahili yao.Mashirika haya yakumbuke kwamba wastahafu hawa wanategemea pension hizi kwa kiwango kikubwa kama vile wafanyakazi wanavyotegemea mishahara yao.Ni swala la kiutu tu na uungwana kwamba shirika hili liwe na mpango sahihi wa kuwalipa wazee hawa mapema.Ni watu waliolitumikia shirika hili kwa siku nyingi kwa hiyo ni vema wakaheshimiwa.Tukiandika andika hivi mwishoni mtapoteza wateja.


=Wastaafu...

Halafu hizi ni fix na uache kutisha watu wewe kibarua Wa NSSF....
 
Watakuwa hawawatendei haki,wastaafu ni watu ambao wengi wao wategea malipo hayo kwa kila kitu,sasa kuwacheleweshea malipo ni sawa na kuwadhulumu.Mtaani hawakopesheki kutokana na kuonekana maskini wasioweza kulipa.PSPF wawe wepesi kuwahudumia wastaafu
 
=Wastaafu...

Halafu hizi ni fix na uache kutisha watu wewe kibarua Wa NSSF....

Naomba unielewe, mimi si husiki kabisa na NSSF.Kwanza NSSF ndio wa hovyo kuliko wote.Ni ukweli kwamba wastahafu wa PSPF hawajalipwa pension zao kwa kipindi cha April,May na Juni kama ilivyo kawaida.Kama hii sio kweli ndio uongee,vinginevyo kaa kimya usidakie maneno usiyo yajua.
 
Inasikitisha sana, ni kweli wastaafu wa PSPF hawajalipwa pension ya January, February na March
 
=Wastaafu...

Halafu hizi ni fix na uache kutisha watu wewe kibarua Wa NSSF....

Mimi sio kibarua wa NSSF.Kwanza NSSF ndiyo mbaya kuliko.Ila uache kudakia mambo usiyo yajua.Ni kweli PSPF haijawalipa wastahafu kwa kipindi cha April,May na Juni.Kama si kweli waje hapa wakanushe.Hii imewaweka wastahafu kwenye hali ngumu zaidi ya maisha,kwa vile hali yao tayari ni mbaya.Wewe nadhani ndiye kibarua wa PSPF kwa vile inaonekana unaipigia kifua PSPF.
 
Tushirikiane tukomeshe Upuuzi wa mashirika zenye uzembe kama huu kwa sanduku la kura mwezi october mwaka huu.
 
Mimi sio kibarua wa NSSF.Kwanza NSSF ndiyo mbaya kuliko.Ila uache kudakia mambo usiyo yajua.Ni kweli PSPF haijawalipa wastahafu kwa kipindi cha April,May na Juni.Kama si kweli waje hapa wakanushe.Hii imewaweka wastahafu kwenye hali ngumu zaidi ya maisha,kwa vile hali yao tayari ni mbaya.Wewe nadhani ndiye kibarua wa PSPF kwa vile inaonekana unaipigia kifua PSPF.
Asante kwa Tarifa nimefanyia kazi na wazee wanalaumu sana Serekali hii ya Ccm na wameapa kutoirudisha ccm october
 
Mashirika ya kijamii yamekuwa yakijitangaza kuwa yana huduma bora sana,mashirika haya ikiwa ni pamoja na PSPF.Shirika hili lilikuwa linasifiwa kuliko mashirika yote ya huduma za kijamii.Hata hivyo tumeona katika siku hizi za karibuni huduma za shirika hili zikidorora kwa kiwango kikubwa.Kwa mfano wastahafu ambao walipaswa kulipa pension zao za kila mwezi angalau ilipofika tarehe moja ya mwezi wa nne mpaka leo hawajalipwa stahili yao.Mashirika haya yakumbuke kwamba wastahafu hawa wanategemea pension hizi kwa kiwango kikubwa kama vile wafanyakazi wanavyotegemea mishahara yao.Na wakumbuke pia kwamba wastahafu hawa wameneemesha sana mashirika haya.Ni swala la kiutu tu na uungwana kwamba inabidi watambue mchango wao na shirika hili liwe na mpango thabiti wa kuwalipa wazee hawa mapema.Ni watu waliolitumikia shirika hili kwa siku nyingi kwa hiyo ni vema wakaheshimiwa.Tukiandika andika hivi mwishoni watapoteza wateja.Wajirekebishe na watekeleze wajibu wao ipasavyo.

=wastaafu
 
Wastahafu = Wastaafu, hii imekaaje wadau??au ndio hizo shule za kata madesa kwa kwenda mbele?
 
Inasikitisha sana, ni kweli wastaafu wa PSPF hawajalipwa pension ya January, February na March

Pspf bana cjui tatzo ni nini pale ila naskia serikali imekopa sana hii mifuko
 
yani sahivi najutia sana ile tarehe 01.03 nlivojiunga na hili shirika ni ujinga ujinga na uongo uongo mwingi wanatangaza mafao ambayo hata hawana NAJUTA SANA KUJIUNGA PSPF
 
Back
Top Bottom