Inawezekana maana jana Rais akiwa kwenye mkutano wa CCM Iringa alivunja katiba kwa kusema atawakata mapembe wananchi ambao wanadai haki katika kulinda raslimali za Taifa lao kwa mujibu wa katiba yetu.
Agekuwa ametamka maneno hayo mtu mwingine, muda huu angeitwa mchochezi na tayari MWEMA angetumwa haraka kumkamata.
Naungana na Wabunge Vita Kawawa na Zedi walisema kwenye mahojiano na ITV kuwa wananchi wapewe taarifa sahihi pia wajue umuhimu wa mradi mkubwa wa GESI.
Sasa Kikwete baada ya kusaini mikataba 19 na WACHINA analeta vitisho visivyo na maana kwa wananchi kuwa atawakata mapembe! Atashindwa kwa ajili ya maendeleo ya nchi, na kama amesaini mikataba hiyo usiku kwenye dhifa bila kuipeleka bungeni damu ya wananchi itakuwa mikononi mwake.
Pia matamshi ya Anne Killango bungeni nayo ni ya kutumwa ili kufunka ukweli, anasema baada ya kugunduliwa GESI na URANI basi mataifa ya nje yanajiingiza nchini kuleta vurugu. mama huyo naye aliongea kana kwamba anaigiza kumbe mnafiki.