Propaganda za Serikali ya Marekani kupitia filamu zao

Chilojnr

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
302
1,306
Sijajua kwa serikali ya Tanzania kama wameanza kuwekeza kwenye filamu kuionyesha dunia ni kwa namna gani Watanzania tulivyo, serikali ilivyo kwa wananchi wake, bado sijajua.

Kwa Marekani! Serikali yao inajua kwamba filamu zina nguvu sana na ndiyo maana vitu vingi sana wanafikisha ujumbe kupitia filamu hizo, zinaangalia na mamilioni ya watu, nao wanapitisha propaganda zao humohumo.

Serikali ya Marekani ina nguvu sana, na inaogopwa duniani, asilimia kubwa imechangiwa na filamu hizi tunazoziangalia, wamekuwa wakitumia nguvu sana huko, na kweli wanafanikiwa sana.

Itazame filamu kama Captain Phillips! Wewe utaitazama kwa jicho la kawaida ila kiukweli serikali yao walitaka kukuonyesha kwamba usicheze na mtu anayeitwa Mmarekani, serikali itafanya lolote lile kumuokoa mtu wao bila kujali gharama yoyote ile.

Ile filamu ni ujumbe kwa waharamia wa baharini, kwamba nyie tekeni meli ila msithubutu kuteka meli ya Kimarekani, gharama yake huwa kubwa sana, na mnaweza kupotea muda wowote kwa kuwa sisi tunajali sana wananchi wetu.

Cheki filamu kama Eye In The Sky. Kwenye ile filamu walitaka kutuonyesha kwamba mpaka Marekani wanalipua sehemu, basi jua wamefanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanaokoa maisha ya watu wengine kabla ya kumuua mtu wao.

Angalia jinsi watu walivyohangaika kuyanusuru maisha ya mtoto, walifanya mengi ila mwisho wa siku walipoona wameweza kumuondoa sehemu husika, wakalipua, ila bomu lilikuwa kubwa sana, mtoto akafa. Hapa wanakwambia hakufa kwa kukusudiwa.

Serikali ya Marekani inatumia nguvu kubwa kupitia filamu, wanaendelea kutuonyesha nguvu ya jeshi lao huko, wanasambaza ushoga, usagaji kupitia hukohuko, na sisi tunakubaliana nao kwa kuwa tunapenda filamu.

Filamu zina nguvu sana, tena sana. Mnaweza kuonyesha hata jinsi Watanzania wanavyotumia nguvu kuwalinda watalii, kulinda wanyama wao, maliasili nyingine, zote zikawekwa kwenye mtindo wa filamu, watu wakajulia huko.

Ila bado sijajua kama serikali ishaamua kulifanya hivyo ama wanafikiria kulifanya. Kama bado hawajalifanya, wanatakiwa kulifikiria, hizi filamu zina nguvu sana kusambaza propaganda duniani.

Ni maoni binafsi.

Imeandika kwa Nyemo Chilongani.
View attachment 2144498
IMG_20220309_151731_684.jpg
 
baba wa propaganda marekani na media zake hlf kabana taarifa za wenzake zisikike kawekeza haswa ili ajitangaze.

ila kiuhalisia marekani anazingua kwa baadhi ya mambo.
 
baba wa propaganda marekani na media zake hlf kabana taarifa za wenzake zisikike kawekeza haswa ili ajitangaze.

ila kiuhalisia marekani anazingua kwa baadhi ya mambo.
Na kila lenye mwanzo linamwisho
Wengi wamesha Jitambua kuhusu Marekani Wamebakia Wale Fuata Mkumbo tu
 
Bajeti ya hizo filamu sio mchezo hasa kwa nchi masikini kama tz.

Kama kuwasafirisha watanzania toka ukraine mmeshindwa, mnaweza toa $50m plus kuandaa film moja,
 
Marekani kwa sasa kuna mambo yashajiseti yenyewe, serikali hata haihusiki moja kwa moja. Watu wa Hollywood wanafanya kazi zao tu.

Na katika kila sinema inayooonesha Marekani kwa mwanga mzuri, kuna sinema nyingine inayoionesha Marekqni kwa mwanga mbaya.

Kuna sinema za Kimarekani zinazomulika uovu wa serikali na idarq zake, ubaya wa organized crime Marekani, ubaguzi wa rangi Marekani, biashara za madawa ya kulevya Marekani.

Kwa hivyo, Marekani kuna uhuru mkubwa na uchumi mkubwa, watu wqnatengeneza filamu kuhusu kila jambo, bilq hata serikali kupanga.

Enzi za serikali kupanga movies Marekani ziliisha kwa kiasi kikubwa miaka ya 1940 na 1950 wakati serikali ilipowaandama movie stars kwa kuwa Wakomunisti.

Of course serikqli inaweza ku push agenda yake hapa na pale, lakini kwa kiasi kikubwa kinachoendesha movies ni uchumi.

Ndiyo ubepari huo.

Kinachopendwa na watu kinauza. Na Wamarekani wanapenda kuona nchi yao inashinda vita.

Of course utaona movies nyingi za hivyo.

Lakini pia Wamarekani wanapenda movies zote nilizotaja hapo juu, kuqnzia za crime, drugs, ubaguzi etc.

Nazo zinatengenezwa nyingi tu.

It's the market that runs Hollywood, not the government.
 
Serikali ya Marekani huwa inatenga bajeti kiasi gani kufanya hizi propoganda za filamu unazozisema ?

Na muziki je?

Na vitabu je?
Sijajua kwa serikali ya Tanzania kama wameanza kuwekeza kwenye filamu kuionyesha dunia ni kwa namna gani Watanzania tulivyo, serikali ilivyo kwa wananchi wake, bado sijajua.

Kwa Marekani! Serikali yao inajua kwamba filamu zina nguvu sana na ndiyo maana vitu vingi sana wanafikisha ujumbe kupitia filamu hizo, zinaangalia na mamilioni ya watu, nao wanapitisha propaganda zao humohumo.

Serikali ya Marekani ina nguvu sana, na inaogopwa duniani, asilimia kubwa imechangiwa na filamu hizi tunazoziangalia, wamekuwa wakitumia nguvu sana huko, na kweli wanafanikiwa sana.

Itazame filamu kama Captain Phillips! Wewe utaitazama kwa jicho la kawaida ila kiukweli serikali yao walitaka kukuonyesha kwamba usicheze na mtu anayeitwa Mmarekani, serikali itafanya lolote lile kumuokoa mtu wao bila kujali gharama yoyote ile.

Ile filamu ni ujumbe kwa waharamia wa baharini, kwamba nyie tekeni meli ila msithubutu kuteka meli ya Kimarekani, gharama yake huwa kubwa sana, na mnaweza kupotea muda wowote kwa kuwa sisi tunajali sana wananchi wetu.

Cheki filamu kama Eye In The Sky. Kwenye ile filamu walitaka kutuonyesha kwamba mpaka Marekani wanalipua sehemu, basi jua wamefanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanaokoa maisha ya watu wengine kabla ya kumuua mtu wao.

Angalia jinsi watu walivyohangaika kuyanusuru maisha ya mtoto, walifanya mengi ila mwisho wa siku walipoona wameweza kumuondoa sehemu husika, wakalipua, ila bomu lilikuwa kubwa sana, mtoto akafa. Hapa wanakwambia hakufa kwa kukusudiwa.

Serikali ya Marekani inatumia nguvu kubwa kupitia filamu, wanaendelea kutuonyesha nguvu ya jeshi lao huko, wanasambaza ushoga, usagaji kupitia hukohuko, na sisi tunakubaliana nao kwa kuwa tunapenda filamu.

Filamu zina nguvu sana, tena sana. Mnaweza kuonyesha hata jinsi Watanzania wanavyotumia nguvu kuwalinda watalii, kulinda wanyama wao, maliasili nyingine, zote zikawekwa kwenye mtindo wa filamu, watu wakajulia huko.

Ila bado sijajua kama serikali ishaamua kulifanya hivyo ama wanafikiria kulifanya. Kama bado hawajalifanya, wanatakiwa kulifikiria, hizi filamu zina nguvu sana kusambaza propaganda duniani.

Ni maoni binafsi.

Imeandika kwa Nyemo Chilongani.
View attachment 2144498View attachment 2144499
 
Bajeti ya hizo filamu sio mchezo hasa kwa nchi masikini kama tz.

Kama kuwasafirisha watanzania toka ukraine mmeshindwa, mnaweza toa $50m plus kuandaa film moja,
Mbona unaanza kutuchamba......
 
Hata wakenya walitengeneza yakwao inaitwa sijui nini huko mwisho kuna squad. Kalikuwa ni ka-series.
 
Bajeti ya hizo filamu sio mchezo hasa kwa nchi masikini kama tz.

Kama kuwasafirisha watanzania toka ukraine mmeshindwa, mnaweza toa $50m plus kuandaa film moja,
Hy $50m kwao huko ni bajeti ya movies ya love stories 😁😁
 
Back
Top Bottom