Tz mbongo
JF-Expert Member
- Mar 12, 2015
- 12,277
- 6,439
Ishu sio kuwa na uhakika maana hali ya kuwa na uhakika inaweza kupatikana hata katika jambo ambalo si la kweli katika uhalisia wake,navyojua mie kuwa na uhakika ni kinyume cha kutokuwa na mashaka. Mfano mtu akikudanganya jambo na akakupa hadi ushahidi wa uongo na mwishowe ukakubali,ni wazi utakuwa na uhakika juu ya hilo jambo lakini kumbe kiuhalisia unachokijua si kweli umedanganywa.(kwa mtazamo wangu,naweza kusahihishwa)Sina uhakika ndio maana nadhani kafa au kasafiri ningekuwa na uhakika ningetoa tamko moja tu
Ni dhana tu kama ile inayosema yupo huku Haina uhakiki
Kwa hiyo swali langu nilitaka kujua sababu iliyopelekea kujenga dhana kama hiyo ni kipi kilichokufanya ujenge dhana za aina hiyo?