Project funding sources

dah kwanza kabisa naomba kukupongeza kwa moyo wa dhati kabisa,hongera.
mimi ni kijana kama wewe,nina ndoto kama zako,I have read the post,all of it,Na kwa kweli you have been a real inspiration.Nafurahi sana kuona kwamba kunavijana ambao wanaweza kufanya mabadiliko,bila ya njia za panya na za mkato.hongera sana kwa hilo.
zaidi ya hapo nina swali moja to naomba nikuulize,HOW DID YOUR PARTNER GET YOUR PLAN ONLINE?kama unaweza kunipitishia na mimi hako ka website basi utakua umenisaidia sana.
ahsateh.
 
Mzuzu,
Mimi sitaki kuongea sana.
Ila najua kipo kitu binafsi ambacho naweza kufanya kama mdau.
Nashukuru sana nimesha fahamiana na mkuu Malila na anaendelea kunionesha
what to do and how to do it!
I promise you; huyu jamaa(Malila)"yuko nondo"
Nakushukuru na wewe pia kwa kuuthamini mchango wangu
Tuko pamoja sana.
 
Poa mkuu, ninatarajia kwenda kijiji cha Banduka pale Lindi siku za karibuni, huenda nikakupitia nione mambo hapo Ikwiriri au kibiti kama ulivyosema.
 
Kama kuna makampuni yanahitaji mikopo, naomba wawasiliane nami kwa njia ya email yangu
<donald.asheri@mail.com>
Kampuni yetu inawakilisha watoaji mikopo kutoka nje ya nchi ambao wanapenda sana kuwekeza pesa zao hapa Tanzania. Mikopo ya aina hii inaanzia US$ 200,000 na kuendelea. Kwa hiyo miradi husika lazima ya gharama hizo. Details zote zitatolewa kwa wale tu watakaomba wapewe taarifa zaidi na wawe wahitaji kweli kwa sababu ni vema waonyeshe kuwa wana miradi hiyo kweli. Hii ni kwa sababu hatuna nafasi ya kupotezeana muda.
Thanks
02.12,2010


Anza kutafuta ardhi ya kufanyia huo mradi,mradi huu unalipa kuanzia small scale,maana yangu ni kwamba unaanza kupata abc za mradi wako kwa kuanzia chini kidogo.Unaweza kupata donors halafu ukashindwa kupata ardhi nzuri kwa wakati,watakuona mzushi.

Je umewahi kufikiri juu ya sehemu nzuri ya kupata ardhi,je unajua aina za mihogo ambayo inalipa ktk masoko yote(local na viwandani), si kila mhogo unaweza kumea po pote.

Je unafahamu tatizo la manpower kwa nchi yetu kwa sasa ie outsorcing,je matatizo yanayoambatana na mradi unayajua,ili ujue namna ya kuyakabili pindi yakikutokea.

Je wewe mwenyewe umewahi kulima mihogo? Nisaidie hayo maswali kidogo ili tuendelee kupeana maarifa.
 
Bravo Mzuzu. Pia jaribu kuongea na jamaa wa TCCAA (sina uhakuka na acronym) kwa kirefi Tanzania Chamber of Commercy ......... kuhusu masuala ya soko nk.
 
Kama kuna makampuni yanahitaji mikopo, naomba wawasiliane nami kwa njia ya email yangu
<donald.asheri@mail.com>
Kampuni yetu inawakilisha watoaji mikopo kutoka nje ya nchi ambao wanapenda sana kuwekeza pesa zao hapa Tanzania. Mikopo ya aina hii inaanzia US$ 200,000 na kuendelea. Kwa hiyo miradi husika lazima ya gharama hizo. Details zote zitatolewa kwa wale tu watakaomba wapewe taarifa zaidi na wawe wahitaji kweli kwa sababu ni vema waonyeshe kuwa wana miradi hiyo kweli. Hii ni kwa sababu hatuna nafasi ya kupotezeana muda.
Thanks
02.12,2010

Hao jamaa zako wangeshuka kidogo ili watupate wengi ingekuwa poa US $ 200,000 kwa sisi Watz wa kawaida ni hatari. Au nyie ndo akina grow-fin?
 
kama kuna makampuni yanahitaji mikopo, naomba wawasiliane nami kwa njia ya email yangu
<donald.asheri@mail.com>
kampuni yetu inawakilisha watoaji mikopo kutoka nje ya nchi ambao wanapenda sana kuwekeza pesa zao hapa tanzania. Mikopo ya aina hii inaanzia us$ 200,000 na kuendelea. Kwa hiyo miradi husika lazima ya gharama hizo. Details zote zitatolewa kwa wale tu watakaomba wapewe taarifa zaidi na wawe wahitaji kweli kwa sababu ni vema waonyeshe kuwa wana miradi hiyo kweli. Hii ni kwa sababu hatuna nafasi ya kupotezeana muda.
Thanks
02.12,2010

am interested in this.nimeku pm mkuu,plz reply. I will email too.
 
safi san shay ,nimevutiwa sana ....unataka kuinvest ktk social work,nafanya ktk eneo hili lakini serikali imetulemaza sana .nimevitiwa sana na wazo hilo
 
safi san shay ,nimevutiwa sana ....unataka kuinvest ktk social work,nafanya ktk eneo hili lakini serikali imetulemaza sana .nimevitiwa sana na wazo hilo

Yah mkuu tuangalie tunaweza kufanya nini bila serikali kwani tayari tunaijua serikali yetu haitafanya kitu! Haijasema kuna mabadiliko yoyote yatafanyika so tusitemee mabadiliko. Kwa vile tumeshajua imetulemaza, basi tuchukue hatua kwa ulemavu wetu tuweze kufanikiwa angalau kidogo!! Tusikae chini sasa kulia na ulemavu tuliolemazwa tayari, tujue tunautumiaje huo ulemavu mkuu!!

Tusaidiane mawazo na tushikane mikono tutaweza naamini!
 
Kwanza napenda nikupongeze kwa hatua nzuri uliyofikia hadi sasa;kwanza mtazamo wa haraka haraka ni kweli mradi huo unalipa kama ulivyoonyesha mahitaji ya huyo mteja na pato litakalopatikana kwa mwaka.Kweli hadi hivi sasa hata mimi ninashawishika kufanya kitu kama hicho kwaajili ya maslahi yangu na Taifa langu kwa ujumla.
Mzuzu,inamaana huyu mteja anahitaji muhogo wowote bila kujali ni wa ubora gani,aina gani ya mbegu au kuna viwango fulani vinatakiwi ili kukidhi mahitaji yake?Ningependa kusikia kutoka kwako ili nijue;ambapo nitahitaji kiasi gani niwekeze katika kilimo hicho ilitusaidiane kufikisha hizo tani 24,000 kwa mwaka au hata zaidi ya hapo kwaajili ya chakula au wateja wengi wa starch kama watajitokeza.
 
Mzuzu na wadau wengine,

mm sio mteja wa siku nyingi hapa janvini, nilijiunga halafu nikapotea, recently I have collected myself back after realising i have lost alot from this forum. Hiki ni kisima cha mambo yote, hakika!!.
Asanteni san kwa michango mingi yenye manufaa san kwa watu wa Tanzania.
Nilishtuka sana nilipooona hii thread ilivyo anza na ilipofia sasa, kweli FOCUS ni kitu cha muhimu sana, FOCUS and love to be determined... utafika popote unapotaka. Mzuzu Hongera sana, sana sana kwa hatua hii muhimu uliyofikia na na wazo zuri la kuleta manufaa kwa nchi yetu. To bring $$$ nchini tena kwa kutumia zao lilizodharaulika na kusahaulika hapa kwetu TZ sio kazi nyepesi. Nawaombea sana mfike mnakokusudia. Mtangulizeni Mungu na utashangaa atakavyo washangaza. Kweli TZ hakuna kitu kisicholipa ni mipango tuu!
Maandiko yanacema "Aonavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo, na Binadamu anakula maneno ya ulimi wake!!!" nenda baba hata Biblia inakutia moyo, go go!!
Tutakutafua wakati mwingine utupe uzoefu ili tufanikiwe wengi. endelea kufanya mambo ya msingi.

Kila la heri
 
Mkuu naona siasa zimekolea sana sasa hapa! Sisi wajasiriamali pia tunaendelea na mikakati.

Update, wakuu tumemaliza mikataba na docs zote muhimu sasa tunaingia kwenye implementation. Mradi mzima utakuta $4M kwa investment ya miaka mitatu, sept hii tunaanza na kuagiza mitambo ya kuanzia tunaanza na pilot project kwa miezi 6 then tutafanya major expansion baada ya kudemonstrate viability.

Nashukuru sana wanaJF hiki kweli nikisima cha hekima, ilikuwa kama utani wakati naanza kuja kuomba ushauri hapa na leo hii ni hatua kubwa tumefikia

Sasa nimeamini kuwa waTZ hatujiandai kufanya plan tunazotaka na kama tunaandaa maandiko yanakuwa too theoritical. Hii proposal ilipata partners kwa kuisoma tu na kujustify uwezekano pia kwa kuwa feasiblity study nilifanya kwa muda mrefu na kujiandaa kutoa maelezo kwa maswali yote yatakayoibuka. Investor kasoma tu kapeleka University of California kwa Professor mmoja consultant akaikubali kila kitu kikaisha. Ukiandaa docs vizuri na kwa data sahihi bila usanii utapata funds bila hata hiyo colatera wanayopigia kelele kila siku, mi sina kitu maskini tu mtz wa kawaida huyu tajiri wala sikumjua na sikuunganishwa na mtu. Kapatikana online na hadi sasa tumeshachoma $20,000 kwa ground work

Tutakuwa na Cereplast inc ubia unaweza kuiona kwa www.cereplast.com ambayo tutazalisha pamoja na itanunua products zote kufeed viwanda vyake US na France. Baadaye tutaweka viwanda hapahapa vya plastics, biofuels, spirits etc lengo ni kusaidia wakulima wasiuze mazao ghafi wananyonywa mno na hawana tumaini lolote

Tena nashukuru sana hili jamvi mchango wa watu si haba. Namshukuru kwa dhati Malila, Tiger, Sikonge, Lazydog, Ntemi, newmzalendo na wengine wote, japo tulianza kwa challenge na kufikiri haitawezekana, kwani kuna wengine walisema ni mradi wa kufikirika. Hii haitusogezi mbele kwani tunakatishana tamaa mapema kikubwa ni kuthubutu, bora ukakwame ulipojaribu na sio mtu akwambie nenda SIDO wakati SIDO yenyewe ilikufa, kweli kuna mtu anayetaka kujifunza kwa aliyefeli??? Mawazo haya hata SIDO wenyewe hawana, nimepita EPZ wakabaki wanashangaa wanauliza umesomea wapi?? Sielewi majengo ya shule yana mchango gani hapo?? Nikasema hapahapa sijawahi kwenda nje zaidi kuja kusign mikataba na hawa jamaa! Elimu inatafutwa na mtu kwa plan ya mtu anavytaka mwenyewe na sio majengo. Wapo wengi waliosomea shule zenye majina makubwa na wanafanya nini au wana impact gani kwa jamii zao?? Nikisema elimu yangu wengine watashangaa lakini haina contribution on this plan tena haina uhusiano hata kidogo

Pamoja tutafika tukiwa na uchungu na nchi yetu. Tunataka tulete $$$$$$ sio kutoa tu kila siku na kuingiza kwa mikopo, kama nilivyoplan tunaanza na mihogo then mazao mengine, walengwa wakubwa ni wakulima maskini na tuboreshe income ya vijijini vijana watarudi kuzalisha tu na sio kuuza vitambaa vya makamasi pale magomeni barabarani


More to come, lets learn and put in practice

hongera sana mkuu WISHING U ALL THE BEST! NIMEJIFUNZA MENGI SANA TOKA KWAKO! NA MALILA
 
Heshima mbele wana JF,

Nimekuwa nahangaikia kupata habari au msaada wa mawazo kutoka sehemu mbalimbali nafikiri na hapa jamvini lazima kuna msaada mkubwa wa mchango naweza kupata kwani naamini hapa ni kitovu cha taaluma na ujuzi wa mambo.

Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikifikiria na kutafuta njia mablimbali za kuweza kufanya sisi kama vijana wa kitanzania katika mambo ya kiuchumi (nikimaanisha kuwa na biashara kubwa) tunazoweza kuanzisha vijana na kutufanya kuondokana na mawazo ya kuajiriwa hasa kwa vijana wenye elimu ya chuo kikuu. Lakini ninasikitika sana kuona watanzania wengi tunagombea nafasi za kuajiriwa tu na serikali yetu haina msaada wowote wa kuwezesha kuleta mafanikio. Serikali yetu inatafafsiri ujasiriamali ni kumwezesha mtu kupata rizki, mi naamini bila viwanda vidogo vya kati huo ujasiriamali hautakuwa na manufaa yoyote, wazalishaji wanatakiwa wajue soko na processing ikifanyika thamani ya mazao yao inaongezeka kwenye masoko ya kimataifa.

Kwa mtazamo wangu nimekuwa nikiamini watu wenye elimu ya chuo kikuu wanatakiwa kuwa na mtazamo wa kuanzisha ajira kwani wao wamepevuka upeo tofauti na waliokosa elimu hiyo.

Kwa wanaJF wanaojua jinsi ya kupata resources jamani ninaomba msaada wa mawazo.

Nimefanya feasibility study kwa miaka kadhaa sasa na hatimaye nimeaandaa business plan ya kufanya processing ya cassava (mihogo) kutengeneza starch. Mali ghafi hakuna asiyejua inapatikana nchi kwetu popote pale unahitaji kuwahakikishia wakulima soko tu na watakufanyia mambo ya kutosha. Hii itainua uchumi wa wakulima wadogo sana na hasa kwenye maeneo ambayo kilimo cha pamba kimeanguka na mikoa kame kama ya kati isiyo na zao la biashara kwani popote inastawi

Soko lipo juu sana na lengo ku export tayari kuna watu wanahitaji sana kuimport kutoka Tanzania nimejaribu kutangaza na kupata response nzuri sana. Kuna soko kubwa sana nchini (yote inaagizwa toka nje esp SA) kuna soko kubwa sana pale TBL na viwanda vingine vinavyotengeneza madawa, nguo, bia, tambi, biscuits, noodles, almost viwanda vyote vinavyotengeneza vyakula (canned na bottled) vinahitaji starch.

Tatizo kubwa nililonalo ni kwamba natafuta source ya funds kuanzisha kamradi haka ambacho profit margin yake ipo juu sana. Nipo tayari kwa mazungumzo specific ya jinsi ya kufanya ili mradi niweze kutimiza hii ndoto. Mradi huu unaweza kuwa expanded katika muda wa miaka 2 au 3 ukawa na plant nyingine ya kuzalisha ethanol kwa kutumia waste materials baada ya kuprocess cassava na tayari nimeanza kudraft plan yake. Nimejaribu kupita Tanzania investment bank na kuongea nao wakawa na interest ya kusaidia ila nikawa sina colateral wala mdhamini mwenye assets nzuri (mimi mtoto wa mkulima tu hata elimu yangu ni ya kuungaunga tu) ninaweza kuraise kidogo tu. Nimepita na NBC ikawa vilevile tu na mradi unakubalika na tatizo siaminiki tu kwa vile sina historia ya kushika pesa kubwa.

Ninaweza kusimamia hii kazi na ikawa juu kiasi cha kuridhisha na kushindana na biashara kubwa tu hata kuanzisha zingine safi zaidi.

Haya wadau naomba reference kwenye source au tujiunege na kuona nini cha kufanya. Nipo kwa wazi nasikiliza mawazo yenu na ushauri! unaweza kuchangia au kuniPM vyovyote utakavyoona

Ahsanteni sana
NOTE: make sure you have written legal right whenever you are searching the funding... to avoid idea embesslement...! hope u get it!!
SUA/Technoserve/COOSTECH may give u some leads!!
 
NOTE: make sure you have written legal right whenever you are searching the funding... to avoid idea embesslement...! hope u get it!!
SUA/Technoserve/COOSTECH may give u some leads!!

Mkuu unaweza kutufafanulia zaidi kwenye hii point?
 
kama kuna makampuni yanahitaji mikopo, naomba wawasiliane nami kwa njia ya email yangu
<donald.asheri@mail.com>
kampuni yetu inawakilisha watoaji mikopo kutoka nje ya nchi ambao wanapenda sana kuwekeza pesa zao hapa tanzania. Mikopo ya aina hii inaanzia us$ 200,000 na kuendelea. Kwa hiyo miradi husika lazima ya gharama hizo. Details zote zitatolewa kwa wale tu watakaomba wapewe taarifa zaidi na wawe wahitaji kweli kwa sababu ni vema waonyeshe kuwa wana miradi hiyo kweli. Hii ni kwa sababu hatuna nafasi ya kupotezeana muda.
Thanks
02.12,2010

mbona email imefail au imekosewa? Plz check it and kama ulikosea uicorrect. I sent u pm and email but it failed.
 
Mzuzu,
Mkuu wangu nashukuru sana kwa jitihada zako ambazo sii rahisi kuzipata toka kwa vijana wetu wa Kitanzania. Hakika soko la mhogo lipo ila kuweza kupata mashirika ambayo yapo tayari kumwaga mtaji inakuwa kazi ngumu kidogo isipokuwa mimi nafahamu Foundation moja ambayo hujishughulisha zaidi ya kilimo hasa nchi maskini...Ila wao wamejikita ktk kilimo cha Kahawa kwa sababu mwanzilishi wa foundation hii ana own mashirika makubwa ya kahawa ikiwa ni pamoja na shirika la uuzaji na migahawa lijulikanalo kwa jina la Tim Hotons.

Jaribu kuwasiliana nao ila kama ingekuwa ni kahawa ningekwambia fanya kazi moja kubwa..kuwaunganisha wakulima wote wa Kahawa ktk eneno lako muunde chombo kimoja ambacho kitawakilisha mawazo ya wakulima wadogo wadogo halafu kwa kutumia jina la chombo hicho ndio wasiliana na viongozi wa Foundation hiyo..
Hata hivyo, jaribu huwezi jua, pia inawweza kuwasaidia wanabodi wengine ambao watakuwa interested. Inaitwa Hanns R. Neumann Stiftung Foundation.

asante sana
 
NOTE: make sure you have written legal right whenever you are searching the funding... to avoid idea embesslement...! hope u get it!!
SUA/Technoserve/COOSTECH may give u some leads!!

Tuna NDA na pia tayari tushaincorporate a company Tanzania na kila mtu ana stok certificate kwa percent zake! Nafikiri sio mbaya kwa kuanzia
 
Back
Top Bottom