Kuzuia wizi wa kazi za wasanii ni zaidi ya kumlilia Rais... kwanza wao wenyewe wala hawaonekani kama kweli wapo tayari wao kama wao kupambana na uharamia... wengi ubishoo umewazidi! Hebu fanya kufikiria, endapo kungekuwa na Msama kama 20 tu hapa wangekuwa wamezuia wizi kwa kiasi gani kinyume chake, namuona Msama peke yake ndie anaepambana kwa vitendo huku wengine wakikalia kulia lia tu!
Hizi kazi zinauzwa mitaani mwetu... kwa Dar es salaam karibu kila kitu cha daladala kunauzwa kaz fake za wasanii na ndio vituo hivyo hivyo ndivyo vinatumika na hao hao wasanii! Kuna siku kwenye mtandao mmoja wa kijamii tulikuwa na mjadala mkubwa sana wa suala hili! Wakati ule, baadhi yao walikuwa wanaridhishwa kutokana na utendaji wa COSOTA pamoja na TRA katika kuzuia suala hili! Mleta mada, Producer na Director mmoja maarufu, nikamweleza wazi kwamba hamjui mnachoongea! Nikawauliza, ikiwa kweli mathalani, kazi kutoka Nigeria huwa zinapata kibali COSOTA kuonesha kwamba zimetoka mikono salama ambako zililipiwa kodi (huko zilikotoka) na hivyo sio one of the pirated materials zinazokuja ku-create competition na kazi za nyumbani, COSOTA wanatumia vigezo gani kujiridhisha kwamba kazi hizo ziliriripiwa kodi huko zilikotoka!!! Hakuna cha maana alichoongea zaidi ya kuendelea kuendelea kuongea kile ilichoonesha wazi kwamba hakifahamu! Kwa hasira, akaamua kuni-block ingawaje ametuma tena request baada ya hasira zake kumwisha!
Aina ya mikataba yenyewe haiwafanyi Crew Members kuwa na uchungu na kazi zinazouzwa mitaani! Chukulia Hollywood kwa mfano, tumwache mwigizaji ambae ndie anauza filamu... hata mwandishi wa script, si kwamba akishalipwa chake tu ndo basi tena, bye for good! Wapo wenye mikataba ambayo inasema wazi kabisa kwamba, pamoja na kuwa tayari umeshalipwa, Box Office ikifika kiasi fulani, utapewa bonus ya kiasi fulani! Sasa kibongo bongo, assume umeandika script ukalipwa sh. laki tano... hapo hata kama filamu itaingiza sh. bilioni tano, wewe huna chako... laki tano yako ulishalipwa! Sasa katika mazingira kama hayo usitarajie kwamba wasanii watakuwa na uchungu na kazi zinazouzwa kama njugu mitaani... chao walishalipwa na ndo imeshatoka hiyo!
Mifano ni mingi lakini linapokuja suala la wizi wa kazi za wasanii; kuna matatizo pande zote mbili! Mambo ambayo zamani niliwahikuwaeleza ndiyo yale yale ambayo kwa sasa ndiyo yanatokea!