father-xmas
JF-Expert Member
- Mar 23, 2010
- 982
- 1,127
Wasanii wetu wa bongo movie wamekua na majina makubwa huku wengi wao wakiwa na hali mbaya kiuchumi.Wengi wamekua wakiitupia lawama kampuni ya muhindi ya Steps kuwa ndio inayowanyonya wasanii.Msanii Batuli alikiri kuwa filamu hazilipi,na ili msanii aweze kijikimu inabidi kutafuta pedeshee la kumuweka mjini.Wasanii wa kiume kama Dr Cheni wako vizuri kiuchumi kwa sababu wanajituma kufanya shughuli nyingine nje ya uigizaji.
Sasa hivi kuna hii kampuni mpya iliyotoa filamu ya Lulu ya Folish age iitwayo Proin.Hawa jamaa wanaonekana kwa kila namna wana lengo la kuimeza Steps.Mpaka dakika hii tayari imeshasaini mikataba na wasanii wakubwa wa filamu akiwamo Lulu na Steve Nyerere na wengine wengi.
Ni vizuri Steps akapata mpinzani,maana upinzani unaweza kuwasaidia vijana waliojikita katika sanaa.Ni vyema wasanii wetu wakafaidi matunda ya vipaji nyao.Inasikitisha kuona dada zetu wakiuza miili yao kwa wazee wa rika la baba zao ilimradi wajikimu na maisha wakati wana majina na vipaji vinavyoweza kuwapa maisha mazuri.
Nimefurahi kuona Proin wakileta upinzani kwa STEPS lakini hofu yangu ni je hawa PROIN wana nia ya kuwakomboa wasanii wetu au lengo lao ni kuendeleza unyonyaji.
Wasanii kwa vile PROIN bado ni changa na inawanyenyekea ili muende upande wao ningewashauri na nyie kutumia hii fursa kuonesha thamani yenu katika kusaini mikataba itakayowanufaisha.
Sasa hivi kuna hii kampuni mpya iliyotoa filamu ya Lulu ya Folish age iitwayo Proin.Hawa jamaa wanaonekana kwa kila namna wana lengo la kuimeza Steps.Mpaka dakika hii tayari imeshasaini mikataba na wasanii wakubwa wa filamu akiwamo Lulu na Steve Nyerere na wengine wengi.
Ni vizuri Steps akapata mpinzani,maana upinzani unaweza kuwasaidia vijana waliojikita katika sanaa.Ni vyema wasanii wetu wakafaidi matunda ya vipaji nyao.Inasikitisha kuona dada zetu wakiuza miili yao kwa wazee wa rika la baba zao ilimradi wajikimu na maisha wakati wana majina na vipaji vinavyoweza kuwapa maisha mazuri.
Nimefurahi kuona Proin wakileta upinzani kwa STEPS lakini hofu yangu ni je hawa PROIN wana nia ya kuwakomboa wasanii wetu au lengo lao ni kuendeleza unyonyaji.
Wasanii kwa vile PROIN bado ni changa na inawanyenyekea ili muende upande wao ningewashauri na nyie kutumia hii fursa kuonesha thamani yenu katika kusaini mikataba itakayowanufaisha.