Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Waungwana,
Maboksi yamenishinda, narudi nyumbani na narudi kuanzisha chama. John Tendwa naomba ajiandae kwa ujio wa Mchungaji.
Chama changu kinalenga kuleta maendeleo kwa Mtanzania na si kwa kauli tuu bali kwa vitendo.
Nimejifunza mengi kutoka kwa TANU, CCM, CUF, CHADEMA, TLP na hata katika kubeba maboksi.
Lengo kuu la kwanza ni kuelimisha Mtanzania ajue haki yake ya kiraia na kikatiba.
Pili ni kumpa Mtanzania si tegemeo au tarajio tuu kuwa anaweza siku moja kupata ngekewa na kuneemeka, bali ni kumfundisha njia bora za kujineemesha kwa kumpa uimara wa moyo, roho na kisha wa kufanya kazi atambue kuwa hakuna lisilowezekana.
Tatu, katika kumjenga Mtanzania huyu upya, Chama changu kitalenga kumjenga Mtanzania anayejitegemea kwa kutumia nyenzo na mazingira aliyomo.
Nne, Chama cha PPPT kitahakikisha kuwa Watanzania wanapewa kipaumbele katika shughuli zote za uzalishaji kwa kutoa elimu ya nadharia na vitendo kuelewa mifumo ya Uchumi iliyoko Tanzania na manufaa yake kwa jamii na maisha yao.
Tano, PPPT lengo lake la muda mrefu ni kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa si nchi yenye kuishi katika ndoto za Amani, Utulivu na Mshikamano, bali ni kwa vitendo ambavyo vitadhihirika kwa kumjenga Mtanzania aondokane na Umasikini, Ujinga na Maradhi. Katika lengo hili, PPPT itahakikisha kuwa inashirikiana na Wananchi wa Tanzania kuujenga mfumo mzuri na bora ambao ni adilifu wa uzalishaji mali na uchumi na kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2035, Tanzania itakuwa inazalisha na kulisha nchi zaidi ya 10 inazopakana nazo.
Sita, Maendeleo ya jamii, yatatokana na mfumo bora wa Elimu na Afya ambao ni chimbuko na msingi mkuu wa Ajira na Uzalishaji mali. Mfumo wa elimu na Afya utapewa kipaumbele ili kujenga Taifa la Watu walioelimika kwa dhati na wenye uwezo wa kufanyia kazi elimu na ujuzi wao kwa kuajiriwa au kujitegemea na Taifa lenye watu walio na afya bora inayoandamana na lishe.
Saba, PPPT ni chama chenye mrengo wa kati, kitajenga kwa kuchagua mfumo bora wa Uchumi unaowafaa Watanzania, kukiwa na nia ya kujenga nchi ambayo Serikali yake si kubwa na yenye kunenepa kwa utapiamlo, bali ni Serikali iliyo imara na yenye afya bora (lean and healthy) ambayo itapunguzwa ukubwa wake kwa asilimia 50 katika kipindi cha miaka 10 baada ya PPPT kuingia katika mfumo wa kisiasa kuanzia ngazi za Mtaa, Kijiji, Kata, Tarafa, Wilaya na hata Taifa.
Nane, kwa kuwa Tanzania iko njia panda kuelewa mfumo bora na sahihi kwa wakati (nyakati) na mazingira yetu kiuchumi, PPPT italenga kuelimisha na kutoa msukumo wa Ujasiriamali na kujitegemea kama mfumo mpya wa kiuchumi ambao utakuwa na vibwagizo (element) kutoka kwenye mfumo wa Kibepari, Kikabaila na hata kijamaa katika kuijenga upya Tanzania.
Tisa, PPPT itahakikisha kuwa inashirikiana na kwa ridhaa ya wananchi na dhamana kutoka kwa Wananchi kuwa shughuli za uzalishaji kutoka kwa wawezekaji wa nje, zinawanufaisha Watanzania kwa zaidi ya Asilimia 3 tunazopata leo hii. Lengo litakuwa ni kuhamasisha Watanzania kushirikiana na Wageni wawekezaji na kuwa washiriki na wabia katika shughuli za Uzalishaji mali na hivyo pato la Taifa kuongezeka kupitia viwango vipya vya kodi na ushuru ambavyo asilimia 50 ya mapato hayo yataelekezwa moja kwa moja kwa wananchi na sehemu husika zilizozalisha mali hizo na kujishughulisha kiuchumi.
Kumi, PPPT kina dhamira ya kurudisha heshima ya Mtanzania na Utu wa Mtanzania awe wa upande wowote ule wa Muungano, dini, kabila, umri, jinsia, kiwango cha elimu au aina ya Ajira. Kwa Tanzania kuwa nchi yenye uimara wa kiuchumi ambao ndio msingi mkuu wa kuhakikisha kuna Amani, Mshikamano na Utulivu wa kweli, kila Mtanzania atarudishiwa haki yake ya Kikatiba na aliyopewa na muumba kwa kuthaminiwa nafasi yake katika Taifa na zaidi, dhamana yake kupitia sanduku la kura.
Kumi na Moja, PPPT itahakikisha kuwa Demokrasia inajengwa upya, kwa kuwa na mfumo shirikishi wa Kiutawala, Kikatiba na Kiserikali ambao utatoa nafasi sawa kwa kila Mtanzania bila ubaguzi au kujali maslahi ya kundi fulani. Mfumo huu utatoa nafasi sawa kwa kila mtu kushiriki katika uzalishaji mali, kushiriki katika siasa na uwakilishi bila kuegemea kutoa upendeleo kwa kikundi kimoja au kwa chama kimoja chenye nguvu.
Mwisho, nawaomba mjiunge nami katika safari hii mpya na wote mnakaribishwa kujiunga mlete mawazo mapya ya kimapinduzi ikiwa tu, mtakuwa tayari kumtumikia Mtanzania na si kutumikiwa na Watanzania!
Akhsanteni,
Maboksi yamenishinda, narudi nyumbani na narudi kuanzisha chama. John Tendwa naomba ajiandae kwa ujio wa Mchungaji.
Chama changu kinalenga kuleta maendeleo kwa Mtanzania na si kwa kauli tuu bali kwa vitendo.
Nimejifunza mengi kutoka kwa TANU, CCM, CUF, CHADEMA, TLP na hata katika kubeba maboksi.
Lengo kuu la kwanza ni kuelimisha Mtanzania ajue haki yake ya kiraia na kikatiba.
Pili ni kumpa Mtanzania si tegemeo au tarajio tuu kuwa anaweza siku moja kupata ngekewa na kuneemeka, bali ni kumfundisha njia bora za kujineemesha kwa kumpa uimara wa moyo, roho na kisha wa kufanya kazi atambue kuwa hakuna lisilowezekana.
Tatu, katika kumjenga Mtanzania huyu upya, Chama changu kitalenga kumjenga Mtanzania anayejitegemea kwa kutumia nyenzo na mazingira aliyomo.
Nne, Chama cha PPPT kitahakikisha kuwa Watanzania wanapewa kipaumbele katika shughuli zote za uzalishaji kwa kutoa elimu ya nadharia na vitendo kuelewa mifumo ya Uchumi iliyoko Tanzania na manufaa yake kwa jamii na maisha yao.
Tano, PPPT lengo lake la muda mrefu ni kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa si nchi yenye kuishi katika ndoto za Amani, Utulivu na Mshikamano, bali ni kwa vitendo ambavyo vitadhihirika kwa kumjenga Mtanzania aondokane na Umasikini, Ujinga na Maradhi. Katika lengo hili, PPPT itahakikisha kuwa inashirikiana na Wananchi wa Tanzania kuujenga mfumo mzuri na bora ambao ni adilifu wa uzalishaji mali na uchumi na kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2035, Tanzania itakuwa inazalisha na kulisha nchi zaidi ya 10 inazopakana nazo.
Sita, Maendeleo ya jamii, yatatokana na mfumo bora wa Elimu na Afya ambao ni chimbuko na msingi mkuu wa Ajira na Uzalishaji mali. Mfumo wa elimu na Afya utapewa kipaumbele ili kujenga Taifa la Watu walioelimika kwa dhati na wenye uwezo wa kufanyia kazi elimu na ujuzi wao kwa kuajiriwa au kujitegemea na Taifa lenye watu walio na afya bora inayoandamana na lishe.
Saba, PPPT ni chama chenye mrengo wa kati, kitajenga kwa kuchagua mfumo bora wa Uchumi unaowafaa Watanzania, kukiwa na nia ya kujenga nchi ambayo Serikali yake si kubwa na yenye kunenepa kwa utapiamlo, bali ni Serikali iliyo imara na yenye afya bora (lean and healthy) ambayo itapunguzwa ukubwa wake kwa asilimia 50 katika kipindi cha miaka 10 baada ya PPPT kuingia katika mfumo wa kisiasa kuanzia ngazi za Mtaa, Kijiji, Kata, Tarafa, Wilaya na hata Taifa.
Nane, kwa kuwa Tanzania iko njia panda kuelewa mfumo bora na sahihi kwa wakati (nyakati) na mazingira yetu kiuchumi, PPPT italenga kuelimisha na kutoa msukumo wa Ujasiriamali na kujitegemea kama mfumo mpya wa kiuchumi ambao utakuwa na vibwagizo (element) kutoka kwenye mfumo wa Kibepari, Kikabaila na hata kijamaa katika kuijenga upya Tanzania.
Tisa, PPPT itahakikisha kuwa inashirikiana na kwa ridhaa ya wananchi na dhamana kutoka kwa Wananchi kuwa shughuli za uzalishaji kutoka kwa wawezekaji wa nje, zinawanufaisha Watanzania kwa zaidi ya Asilimia 3 tunazopata leo hii. Lengo litakuwa ni kuhamasisha Watanzania kushirikiana na Wageni wawekezaji na kuwa washiriki na wabia katika shughuli za Uzalishaji mali na hivyo pato la Taifa kuongezeka kupitia viwango vipya vya kodi na ushuru ambavyo asilimia 50 ya mapato hayo yataelekezwa moja kwa moja kwa wananchi na sehemu husika zilizozalisha mali hizo na kujishughulisha kiuchumi.
Kumi, PPPT kina dhamira ya kurudisha heshima ya Mtanzania na Utu wa Mtanzania awe wa upande wowote ule wa Muungano, dini, kabila, umri, jinsia, kiwango cha elimu au aina ya Ajira. Kwa Tanzania kuwa nchi yenye uimara wa kiuchumi ambao ndio msingi mkuu wa kuhakikisha kuna Amani, Mshikamano na Utulivu wa kweli, kila Mtanzania atarudishiwa haki yake ya Kikatiba na aliyopewa na muumba kwa kuthaminiwa nafasi yake katika Taifa na zaidi, dhamana yake kupitia sanduku la kura.
Kumi na Moja, PPPT itahakikisha kuwa Demokrasia inajengwa upya, kwa kuwa na mfumo shirikishi wa Kiutawala, Kikatiba na Kiserikali ambao utatoa nafasi sawa kwa kila Mtanzania bila ubaguzi au kujali maslahi ya kundi fulani. Mfumo huu utatoa nafasi sawa kwa kila mtu kushiriki katika uzalishaji mali, kushiriki katika siasa na uwakilishi bila kuegemea kutoa upendeleo kwa kikundi kimoja au kwa chama kimoja chenye nguvu.
Mwisho, nawaomba mjiunge nami katika safari hii mpya na wote mnakaribishwa kujiunga mlete mawazo mapya ya kimapinduzi ikiwa tu, mtakuwa tayari kumtumikia Mtanzania na si kutumikiwa na Watanzania!
Akhsanteni,