Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Ndiyo kawaida ya serikali ya awamu ya nne inabwagwa kila sehemu. Tatizo ni kuwa kila jambo inafanya pupa tu kwa lengo la ku-win mass kwamba inapelekwa hata vigogo mahakamani kama jk anavyozungumza majukwaani.
Hata suala la mgombea binafsi lilifanywa kwa jazba tu. JK afahamu kuwa uongozi wake una dalili zote za kupwaya angeachia ngazi mapema huenda tungempatia heshima kubwa kuliko hivi sasa. Dr. Slaa akishinda urais, tumtarushia JK vilago vyake aende Chalinze.
Si ndio utendaji haki jamani? Hii sio kesi ya msingi bali ni suala la dhamana ambalo linaonekana kuleta ubaguzi kwa washtakiwa wenye fedha na wasio na fedha!
Sasa pupa ya serikali iko wapi hapa?
Ndiyo kawaida ya serikali ya awamu ya nne inabwagwa kila sehemu. Tatizo ni kuwa kila jambo inafanya pupa tu kwa lengo la ku-win mass kwamba inapelekwa hata vigogo mahakamani kama jk anavyozungumza majukwaani.
Hata suala la mgombea binafsi lilifanywa kwa jazba tu. JK afahamu kuwa uongozi wake una dalili zote za kupwaya angeachia ngazi mapema huenda tungempatia heshima kubwa kuliko hivi sasa. Dr. Slaa akishinda urais, tumtarushia JK vilago vyake aende Chalinze.
Hapa nashindwa kiielewa mahakama. Mbona kwenye kesi ya mgombea binafsi hawakutoa uamuzi kama huo!!!?MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, imetamka kuwa kifungu cha 36(4)(e) sura ya 200 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Sambamba na hiyo, mahakama hiyo, imetoa maelekezo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndani ya mwaka mmoja kuanzia jana, awe amefanyia marekebisho kifungu hicho.
na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, imetamka kuwa kifungu cha 36(4)(e) sura ya 200 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Sambamba na hiyo, mahakama hiyo, imetoa maelekezo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndani ya mwaka mmoja kuanzia jana, awe amefanyia marekebisho kifungu hicho.
Hukumu hiyo ya Kesi ya Kikatiba ya mwaka 2008, iliyofunguliwa mahakamani hapo na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ilitolewa jana na jopo la majaji watatu lililokuwa likiongozwa na Jaji Kiongozi, Fakhi Jundu, aliyekuwa akisaidiwa na Jaji Agustine Mwarija na Projest Rugazia ambaye hakuwepo mahakamani hapo wakati hukumu hiyo ikisomwa.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji Jundu alisema kimsingi Mahakama Kuu inakubalina na hoja za mawakili wa mlalamikaji (Mahalu), aliyekuwa akitetewa na mawakili wa kujitegema, Alex Mgongolwa na Cuthbert Tenga kwamba kifungu hicho cha 36 (4)(e) sura ya 200 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi, kinakwenda kinyume na Katiba ya nchi na kinaleta ubaguzi.
Alisema wanakubaliana na hoja za mawakili wa Mahalu, kwamba uwepo wa kifungu hicho unafanya mshtakiwa mwenye fedha ndiye apate dhamana na mshtakiwa ambaye hana fedha hawezi kutimiza masharti hayo ya dhamana hivyo kuishia kusota gerezani.
Hata hivyo, Jaji Jundu alisema kwa mujibu wa Ibara ya 30 (5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mahakama Kuu inapoona kifungu chochote cha sheria kinakiuka ibara za Katiba , ina mamlaka ya kutoa maelekezo kwa Mwanasheria Mkuu kukifanyia marekebisho kifungu hicho.
Hii ni kesi ya pili ya Kikatiba kufunguliwa na wananchi katika mahakama hiyo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na mwisho wa siku, wanashinda tangu serikali ya awamu ya nne iingie madarakani.
Mahalu alilazimika kufungua kesi ya Kikatiba Mahakama Kuu, ikiwa ni muda mfupi baada ya mwaka 2006, kufikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ya sh bil. 3.
Kesi hii ilifunguliwa kwa shinikizo la kikwete kutaka kumkomoa mzee huyu aliyekuwa mwadilifu katika utumishi wake akiwa balozi italy.Walitaka kumuingiza katika ufisadi wa kutafuta pesa za kampeni 2005 akawatolea nje. Wakaamua kumkomoa lakini mwisho wa siku serikali hoi.Ndugu zake wasukuma wanahasira sana na mkwere watammalizia kwenye sanduku la kura mwaka huu.
na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, imetamka kuwa kifungu cha 36(4)(e) sura ya 200 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Sambamba na hiyo, mahakama hiyo, imetoa maelekezo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndani ya mwaka mmoja kuanzia jana, awe amefanyia marekebisho kifungu hicho.
Hukumu hiyo ya Kesi ya Kikatiba ya mwaka 2008, iliyofunguliwa mahakamani hapo na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ilitolewa jana na jopo la majaji watatu lililokuwa likiongozwa na Jaji Kiongozi, Fakhi Jundu, aliyekuwa akisaidiwa na Jaji Agustine Mwarija na Projest Rugazia ambaye hakuwepo mahakamani hapo wakati hukumu hiyo ikisomwa.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji Jundu alisema kimsingi Mahakama Kuu inakubalina na hoja za mawakili wa mlalamikaji (Mahalu), aliyekuwa akitetewa na mawakili wa kujitegema, Alex Mgongolwa na Cuthbert Tenga kwamba kifungu hicho cha 36 (4)(e) sura ya 200 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi, kinakwenda kinyume na Katiba ya nchi na kinaleta ubaguzi.
Alisema wanakubaliana na hoja za mawakili wa Mahalu, kwamba uwepo wa kifungu hicho unafanya mshtakiwa mwenye fedha ndiye apate dhamana na mshtakiwa ambaye hana fedha hawezi kutimiza masharti hayo ya dhamana hivyo kuishia kusota gerezani.
Hata hivyo, Jaji Jundu alisema kwa mujibu wa Ibara ya 30 (5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mahakama Kuu inapoona kifungu chochote cha sheria kinakiuka ibara za Katiba , ina mamlaka ya kutoa maelekezo kwa Mwanasheria Mkuu kukifanyia marekebisho kifungu hicho.
Hii ni kesi ya pili ya Kikatiba kufunguliwa na wananchi katika mahakama hiyo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na mwisho wa siku, wanashinda tangu serikali ya awamu ya nne iingie madarakani.
Mahalu alilazimika kufungua kesi ya Kikatiba Mahakama Kuu, ikiwa ni muda mfupi baada ya mwaka 2006, kufikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ya sh bil. 3.
Mwanakijiji,Ukisoma hukumu ya suala la wagombea binafsi endapo mabadiliko ya Katiba yamepitishwa kihalali na Bunge yanaweza vipi kuwa kinyume cha Katiba? Kwa sababu majaji wa rufaa walichosema ni kuwa sehemu ya Katiba itakuwa kinyume cha Katiba endapo kimepitishwa kinyume cha utaratibu wa kufanyia mabadiliko ya Katiba.
Mwanakijiji,
Kinachonittiza mimi ni kwamba katiba hapa ndio inaonekana shida. Tuna lidude linaitwa katiba ambalo ni shida tupu katika kutoa haki kwenye nchi yetu na sehemu nyingi tu zinapingana katika katiba hii.
Lakini zaidi ya hayo nikiangalia hapa hukumu hii na hukumu ile ya mahakama ya rufani ya mchungaji Mtikila naona ingawa zote zina point kwenye katiba kuwa ina matatizo lakini humu hizo mbili zinakuwa na tofauti.
Utaona hukumu hii inamuagiza mwanasheria wa serikali katika mwaka mmoja awe amepeleka mswada bungeni kubadilisha vifungu vinavyokinzana wakati hukumu ile ya mahama ya rufani ya mchungaji Mtikila inasema kwenye jambo hilo hilo kuwa mahakama ilikosea kuliagiza bunge kubadilisha kifungu cha katiba. Ikiwa na maana bunge lenyewe ndilo lenye uamuzi wa kubadilisha likipenda tena bila kulazimishwa na mahakama.
Najiuliza kuwa kama hukumu ya mahakama ya rufaa iliona kuwa mahakama ilikosea kuliagiza bunge (kwa kumuagiza mwanasheria wa serikali ni sawa na kuliagiza bunge kwa kuwa naye ni mbunge kwa mujibu wa katiba) sasa hii hukumu si bado ni kama inakinzana na hukumu ya mahakama ya rufani?
Haiwezi kuwa ile hukumu ya mahakama ya rufani litolewa na watu hawakwenda shule kiasi kwamba hata majaji wa mahakama za chini bado hawataki kuiangalia kama reference?
Halafu kuna watu(hapa Njb Kaskazini) wanataka eti wachague mtu aliyeishia darasa la nne(ingawa anatudanganya kafika la saba) awe mbunge wasijue kabisa kuwa hatakuwa na mchango wowote zaidi ya kupigia kura miswada kwa minajili ya kuvutia upande wao.Nadhani muwalaumu wawakilishi(wabunge) wabovu wanaolala usingizi na kushindwa kujadili miswada,matokeo yake ndo kupitishwa kwa sheria kandamizi.Msifanye kosa sasa,chagueni wawakilishi makini.