Profesa Baregu: Watanzania Wanajiaandaa Kukikabithi CHADEMA Dola.

Profesa Baregu: Watanzania Wanajiaandaa Kukikabithi CHADEMA Dola.

Nadhani alitaka kufikisha ujumbe huu kwa Padre Slaa na Mbowe.
Nimekuwa msuluhishi ndani ya chama, nakwambia ndani ya chama haiwezekani fikra moja ikaendelea kudumu, kwa msingi huo lazima watu watofautiane mtazamo, si kila jambo kupinga.
 
Ubarikiwe mzee wetu Baregu hizi ndio hekima tunazo ziitaji katika Chadema hekima na busara uzidishiwe na miaka mingi ili uturidhishe kizazi cha dot com
 
Matumaini ya wanachadema hayatapotea.. kamwe

Asante sana Professa

Kama watazingatia huu ushauri alio usema;
“Nimekuwa msuluhishi ndani ya chama, nakwambia ndani ya chama haiwezekani fikra moja ikaendelea kudumu, kwa msingi huo lazima watu watofautiane mtazamo, si kila jambo kupinga.
 
PROF. ameongea bila ushabiki wa pande fulani nashangaa comment za wadau zinakosa mashiko: tujiwekee utamaduni wa kufikiri kwanza sio kusoma thread nusu na kukurupuka ku comment shame that behavior!!!
 
Prof. Baregu pamoja kuwa nakuheshimu sana kwenye ili nakupinga tanzania hakuna chama mbadala wa CCM.

Nakubaliana na wewe hakuna chama mbadala wa ccm kwa kuua tembo wetu kwa kushirikiana na serikali ya China, pia hakuna mbadala wa ccm kwa kuwatesa na kuwauwa wananchi wanyonge kwa kisingizio cha operesheni tokomeza na kuwaacha majangiri yakitamba
 
"Nilimkubali sana Zitto, lakini katika hili la kuchagua kati ya Zitto au chama changu, bila kusita nimechagua chama changu"
 
Mjumbe wa Kamati Kuu ya chadema, Profesa Mwesiga Baregu, amesema viongozi wa chama hicho wanapaswa kulinda kauli zao ili kuepuka mvuragano unaoweza kutokea wakati huu.

“Wakati huu ambao chama kimekuwa na mambo mengi, nawasihi viongozi kuchunga kauli zao ili kuepuka matatizo ambayo yanaweza kujitokeza.

“Nimekuwa msuluhishi ndani ya chama, nakwambia ndani ya chama haiwezekani fikra moja ikaendelea kudumu, kwa msingi huo lazima watu watofautiane mtazamo, si kila jambo kupinga.

“Katika hali hii, msimamo wangu ni kwamba changamoto inayotukabili tupunguze makali ya maamuzi, kwa sababu Watanzania wengi wanakitegemea chama hiki.

“Hivi sasa Watanzania wanajiandaa kukikabidhi CHADEMA dola,
ni wakati mzuri wa viongozi kufikiria maisha ya chama kwanza na baadaye ukweli wa mambo utajulikana,” amesema.

source: wavuti.com




Akamwambie mzee Mtei, jana katoa tamko kuhusu zito kuwa hana nafasi ndani ya CDM. matamko km haya bila vikao vya chama ni hatari.
 
Wendawazimu pekee ndio wanaamin kuwa sisiem itatawala milele so licha ya huyu zzk kukbusu chadema huku anakisalt cdm ina nafac ya kutawala nchi hii.nadhan huyu mbwa mwitu hata akienda sisiem hana nafasi ya kupewa agombee urais cv ya usalt ameipata zzk.cdm cyo zitto wala slaa au mbowe.
 
Touch-Log Out

Forum-New Posts-Settings-Search


->-Forum->-General Forums->-Jukwaa la Siasa

Topic:-nape wa ccm ni sawa na zito wa chadema

longinos-12:00 Today-

Ukifuatilia siasa za hawa dogo zinafanana, nape alipoleta ukorofi kuhusu jengo la uvcccm alijifanya ni mpambanaji, mtetezi wa vijana nakujifanya ccm anaijuwa kuliko akina EL eti kwa sababu baba yake alikuwa kwaya masta wa ccm(kama komba)kilichompa nafasi moses nnauye ni kuimba si weledi wa siasa.Nepi aliporudishwa kundini na jakaya alirudi na kauli mbiu KUFUKUZA MAGAMBA NDANI SIKU 90 naamini ni siku 90000.Kinachojitokeza ni kunenepeana kwa Nepi bila majibu ya siki 90.
Zito nae kaja na gear hiyo hiyo, nilijiunga cdm nikiwa na miaka16 so what oh wengine wametoka ccm wanajifanya wanakijua chama, hizi ni kauli na kijuha ambazo hazina mshiko sijui zito alitaka watu watokee mwandiga au kwa ndugu zake wa asili Bujumbura? Kama unakipeleka chama mahakamani unategemea huruma gani kwa wana cdm? Tamaa na kutaka sifa ndiko kunakowasumbua waili hawa na hawatafika popote kisiasz maana WANAFIKI walilaaniwa hata kwenye vitabu vya dini mwisho wa zito na nape 2015 sababu Kikwete akitoka Nepi inabini akajiunge na Frelimo ya msumbiji na MM Zito mahakama itakulinnda mpaka 2015 baada ya hapo utatupwa chali,

Mkuu kwa vyovyote vile itakuwa vigumu ZZK kuwa mwanachama wa CDM. Natumaini na yeye anajua. Ila anachokifanya ni kutaka kuleta vurugu. Kwa wabunge wote wa CDM ningeomba kuanzia sasa swala lake waachane nalo. watalizungumzia endapo watakapoulizwa kwenye mikutano na hapo ni kutuo summary tu.
 
CDM in agenda kukabidhiwa Dola. CCM imekufa haiwezi tena kuongoza....!!!
 
Kwani magamba huwa mnakiri ukweli? Wajuuzi wa mambo wanajua CDM mwakani inatimba magogoni.

wewe wewe wewe wewe wewe wewe wewe wewe!!!!!!!!!!! magogoni ni mbali pale usipaone karibu ukishuka kwenye pamtoni!!! muulize LYATONGA NA LIPUMBA mpaka leo bado hawajafika, mbowe kapanda helicopter 2005 mpaka leo hajafika.

CDM bado sana kaka, hata CUF 2005 Walijiaminisha hivyo mpaka wakakimbilia china zilikochapwa karatasi za kupigia kura..

USHAURI; MWANASIASA HAWEZI KUIKOMBOA TANZANIA HATA SIKU MOJA.
 
Hivyo ndivyo ninavyojua cdm 2013 kushika dola. Watanzania wako tayari na magamba wanaendelea kuandaliwa kisaikolojia.
 
Back
Top Bottom