BABA E's
JF-Expert Member
- Dec 25, 2012
- 354
- 136
Nimemsikiliza Prof. Tibaijuka vizuri Star-TV asubuhi hii, namuona anatapatapa. Kwa wachache tunaoijua shule hii ufadhili ulishafutwa muda mrefu na wanafunzi wapya wanaojiunga kwa muda mrefu wamekuwa wakilipa kiasi chote cha fedha. Napata wasiwasi kama kweli hizo hela alizopokea zililenga hasa ufadhili huo anaouongea. Kama kweli hizo hela zilikuwa za shule, nafikiri shule yenyewe ilikuwa ina uwezo wa kufungua account yake katika bank ya mkombozi, kwanini afungue account yake binafsi. Nadhani kuna haja ya kutafuta taarifa kamili kutoka kwenye shule yenyewe.