Prof. Tibaijuka ashauri wabunge wasiwe Mawaziri!

Prof. Tibaijuka ashauri wabunge wasiwe Mawaziri!

Aliyekuwa waziri wa ardhi na makazi wa tanzania mh anna tibaijuka anaitaka serikali kubadirisha utaratibu wa mbunge kutokuwa waziri ili wabunge waweze kuwahudumia wapiga kura wao badala ya kutumia muda mwingi kufanya kazi za serikali.

Wadau kama sio uchizi ni nn hiki au ndio kapagawa baada ya kufutwa kwake?

Hilo lilikuwemo ktk rasimu ya katiba mpya kwa wingi wao ccm wote walilipinga sasa imekuwaje baada ya kutolewa alione ni suala la msingi,hiyo inaonyesha kuwa ccm wengi wameburuzwa kumbe wana matakwa yao binafsi na sio kufuata matakwa ya chama hata kama huridhii.[/

mbona ndio msimamo wake toka bunge la katiba?/alichangia kipengele icho na akataka mawaziri wasiwe wabunge,tatizo lako sio mfatiliaji ila ni mshabiki wa matukio na siasa chafu,wewe una hila sana umekaa kaa kishirikina,wewe ni zaidi ya mwanga muuaji ,sumu unazo panda zitakurudia,acha unafiki
 
Ulikuwa hujui? Tena wizara ya ardhi!!
Hapana mkuu sio kiasi hiki maana wakifukuzwa naona kama vile wanakuwa wanaongea hovyo sana Maige, Nundu na lile shairi lake la 'silent of the lamb' na sasa huyu mama.

Lakini mbona ana maisha mazuri tu tayari.
 
Mwambie ahamasishe kusema NO TO KATIBA PENDEKEZWA hapo tutamuelewa anamaanisha nini.Kama anaisapoti katiba pendekezwa basi ni wivu tu unamsukuma kusema hivyo
 
Afrika haina elimu,hebu jiulize huyo ni Profesa na juz tu aliyapinga mazur kwenye rasim ya mzee warioba.yuko nje ameona
 
Aliyekuwa waziri wa Ardhi my.Anna Tibaijuka, amesema serikali inapaswa kubadilisha mfumo wa uongozi akimaanisha kwamba mawaziri wasiwe wabunge kwa sababu wanajikuta kufanya kazi za serikali bila kuwatumikia wananchi waliowatuma.

-Hii kauli yake ni sahihi kabisa maana 95% ya wabunge ambao ni mawaziri mda mwingi hawaendi majimboni kusikiliza kero za wananchi waliowachagua na kuwapa ahadi lukuki ambazo hazina hata utekelezaji.

-Upande mwingine naona anasema hivyo kwa kuwa ameachishwa madaraka maana kipindi yuko madarakani mbona alikuwa hasemi hivyo?

-Hawa viongozi wakiwa madarakani hawaoni kama wanafanya makosa na pindi wanapoacha kazi ndo wanagundua mabaya.

-Watu kama hawa hawafai kabisa. Yaani NYANI HAONI KUNDULE.
 
Mbona alisema haya kwenye bunge la katiba. Tatizo mijitu haifatilii mambo inaishia kuropoka tu.
 
Huyu mm prof ni chizi. Mbona wakati wa kijadili rasimu ya katiba ua Warioba alifunga mdomo au kwakua alikua waziri. Mapendekezo hayo yalikuwemo , yy na ma ccm wakayatupilia mbali wakaja na hoja zakwao.
 
Mama amevurugwa yaani tutaona na kusikia mengi ni kama vile yuko mahabusu anatiwa ule umeme kwa chini sasa maneno yanamtoka tu.
 
Huyo ni mfa maji hana jipya arudishe hela alizokula asituzingue mbona hakuongea hivyo akiwa bado yuko ndani ya serikali (Waziri).
 
Warioba na katiba yake ilipendekeza hivyo wakamuona 'fa.la' leo hii katemwa anaona hilo wazo linafaa.
Hakuna kitu kibaya kama kuwa na viongozi wanaofikiria kwa kutumia TUMBO.
 
Wakati Yesu akiwa hapa duniani akifundisha na kuonya aliwakemea sana mafarisayo kwa sababu ya 'UNAFIKI WAO' na hakuogopa mtu yeyote wala kuangalia uso wa mtu wala cheo cha mtu, nimejua ni kwa nini Yesu alikuwa mkali sana kukemea unafiki, Prof. Tibaijuka alitakiwa aongee hayo wakati wa Constituent Assembly(Bunge Maalum la Katiba-BMK) na siyo leo, huu ni unafiki mkubwa sana kwa sababu anaona kwa vile yeye amekosa uwaziri na wengine wakose(ingawa yuko sahihi kwa 100%) lakini wao walikuwa wakitupinga siku nyingi tunaotaka kutenganisha uwaziri na ubunge, huo ni unafiki mama bora unyamaze tu kimya huo unafiki wako hautakuwa dhahiri
 
Namkumbuka huyu mama siku ile ya MDAHALO WA UDASSA na anachozungumza leo ni TOFAUTI Kabisa.ULAJI BLINDS PEOPLE
 
mbona huu ushauri hakuutoa kabla hajafukuzwa na JK kwa hiyo hapo atakuwa anampa presha mwinzi mwenzake Prof.Muhongo aliteuliwa na kupewa uwaziri ..ccm ina viongozi wanafiki sana wasiofaa kuamini
 
Kwa hili nitamsaidia Prof Tiba. Kwenye bunge la katiba, wakati akichangia aliunga mkono hoja ya mawaziri kutokuwa wabunge. Nilimsikia mwenyewe
Lakini akapiga kura kukiunga mkono kinyume na ushauri/imani yake!!!
 
Back
Top Bottom