Prof. Ndalichako, kiatu kishampwaya!

Prof. Ndalichako, kiatu kishampwaya!

Hivi unafikiri kila mtu ni mboga saba km ww?

Njia ya kutatua matatizo ni kujibidisha ili kujikwamua na sio kukaa kuwa omba omba. Ukae ukijua sio wote wanahtaji misaada, baadhi yetu tupo hapo kwa kuwa hatujui kuwa ni wajibu wetu kupambana kufika pahali Zaidi. uombaje akakupa bila kukueleza ukweli ataendelea kukufanya kuwa mtumwa Zaidi. Ukweli unauma lkn matatizo ya serkali kushindwa kumudu loan yanatoka na wengine wenye Uwezo kidogo kutotaka kujituma wakataka favour na hata kupelekea kuwazibia hata wale ambao kweli ni wahitaji
 
Aliyekupa wewe na familia yako ni Mungu, usitutoe thamani sisi watoto wa wakulima na wavuvi. Mshukuru Mungu wewe ni mboga saba.

*Tunasomeshwa kwa tabu ada ya A'level mpk wazazi wanashindwa. Wazazi wetu hawawezi kutulipia ada ya vyuo, tukikosa mikopo tutakosa elimu.

*Taifa linahitaji wasomi hata kama watakuwa wengi.
kama unafikiria ninachoongea hapa ni classes, hatutaelewana hata iweje.
suala la kila mtu kwenda chuo nadhani yapasa waende ambao wamefika viwango otherwise tutapotezeana muda, wengine wangegundua mapema wangeshika njia zingine za mafanikio. Sio wote waliofanikiwa ni wasomi wa vyuo. Kwa sasa wapo wengi wamemaliza elimu za juu na hakuna ajira na wanasubiri. Time will tell, tutabadilika
 
WATANZANIA NA KUPENDA DEZO YA MTEREMKO,KUFYATUA MFATUE WENYEWE SHIDA MUILETEE SERIKALI NA KULI LIA MSSADA WA KUSOMESHEWA,KAMA HUWEZI KUSOMESHA MWANAO SI UMUOZE TU ,KILA SIKU MIKOPO MIKOPO MIKOPO,AHHHH KWENDEBI HUKO YANI MNAKOOPA KUANZIA BABU,BABA HADI MJUKUU HADI SERIKALI NAYO INAKOPA KOPA TU,YANI MTEREMKO KILA MAHALI,KWENDENI HUKO
 
Siku anateuliwa kuongoza Wizara ya elimu (wizara ambayo ndiyo 'backbone' ya ustawi wa Taifa), nilifurahi sana. Nikajisemea moyoni kwamba sasa gari limepata 'suka' na safari itakuwa salama.

Safari ikaanza suka akiwa imara. Lakini kadri safari ilivyoendelea, nikagundua kuwa kumbe suka wetu ni 'deiwaka' tu, na sio 'profesheno' !

Akaanza ubabaishaji. Siku akalala akaota GPA ya 3.5... na kweli kesho yake tu rukwili ikapitishwa GPA ya 3.5! Nikajisemea moyoni... ohooo sasa suka kaanza kuacha reli, ngoja ni-fasten my belt kabisa mapema.

Haijaisha week, akalala akaota GPA ya 3.0... na kweli kesho yake tu rukwili GPA ya 3.0 ikapitishwa! Nikasema "toba, suka kaanza kupiga ramli kwenye safari yetu?!!"

Yote tisa.... kumi kwenye mikopo ya chuo! Hapa sasa ndiyo nimeconclude kuwa kumbe Wizara ya Elimu bado haina suka, bali deiwaka tu!

75% kukosa mkopo hii ni ajabu ya mwaka!

Mtoto wa maskini kapanda ngorika kutoka sitimbi kijijini kaja mjini kusoma chuo, eti anapewa mkopo wa Tsh. 77,000 ajikimu chuoni! Seriously kabisa Officer mzima yupo Heslb kwenye kiti cha kuzunguka ana-approve Tsh 77,000 kwa ajili ya mkopo wa mwanafunzi wa chuo??!! Hizi ni dharau kwakweli. Otherwise naanza kuamini ule utafiti kwamba nchi hii wengi wana matatizo ya akili. Heslb wanastahili wachapwe bakora nyingi sana kama mvua!

Tanzania inahitaji overhaul ya hali ya juu sana. La sivyo, dharau hizi za viongozi zitazidi kuwafanya wananchi waishi kama mashetani kweli.

Mama Ndali, absolutely sasa kiatu kinakupwaya! Ubabaishaji kwenye elimu ya nchi, Taifa mnaliweka bondi.

Mhe. Rais Magufuli anahitaji kuona Tanzania ya viwanda. Ni jambo jema sana. Ili kuifikia Tanzania ya viwanda, basi tuacheni siasa na ubabaishaji kwenye sekta ya Elimu.

-Kaveli-

Mama huyu nadhani hakuchaguliwa kwa uwezo wake !!!!! ILA NI KUENDELEZA HUJUMA KTK WIZARA HII MAMA, she was a huge problem when she was there at once. Mr.JK akamfuta, lakini waliokua wanamtumia iliwaumiza sana kutimuliwa mama huyu.
Kwani ni nani ambaye hakuyaona MAAJABU ya figisufigisu za matokeo ya kidato cha IV mwaka 2012 akiwa kiongozi mwandamizi ktk wizara hiyo?

(a) anasifa ipi mpaka ikashawishi arudishwe tena ktk wizara hiyo wakati yeye alikua tatizo kubwa hapo?

(b) kwani kama ni tunu ya kupewa uwaziri kwa uprofesa wake hawezi kua waziri asiyekua na wizara maalum ?

(c) Kama Mr. Padlocks atamuacha hapo kwa interest fulani fulani mengi tutayashuhudia.
 
Njia ya kutatua matatizo ni kujibidisha ili kujikwamua na sio kukaa kuwa omba omba. Ukae ukijua sio wote wanahtaji misaada, baadhi yetu tupo hapo kwa kuwa hatujui kuwa ni wajibu wetu kupambana kufika pahali Zaidi. uombaje akakupa bila kukueleza ukweli ataendelea kukufanya kuwa mtumwa Zaidi. Ukweli unauma lkn matatizo ya serkali kushindwa kumudu loan yanatoka na wengine wenye Uwezo kidogo kutotaka kujituma wakataka favour na hata kupelekea kuwazibia hata wale ambao kweli ni wahitaji

Nafikiri kunatatizo la kuelewa, kwani hizo pesa za mkopo kwa wanafunzi ni makusanyo kutoka wapi ? kama ni kodi za wananchi huyo mwananchi mwenye uwezo halipi kodi? na huyo asiyekua na uwezo naye halipi kodi ? Kama wote wanalipa kodi kunahaki ipi ya kubagua ktk kuwakopesha?
Tena wenyeuwezo wanalipa kodi kiasi kikubwa kuzidi wasiokua na uwezo
Minafikir uungwana ni kuwomba jamani nyie wenzetu mliojaliwa kipato tunakuombeni msaidie ktk hili ili tuwasaidie nawale ambao hawakujaliw kipato kikubwa,
Sio kuona kama kwamba ni dhambi nawo kupata mkopo wakati jasho lao limo ktka mfuko huo.
 
Back
Top Bottom