Prof. Ndalichako anafaa kuwa Rais 2025

Prof. Ndalichako anafaa kuwa Rais 2025

Mwanamke hapana kwa kweli ata sizonje hawezi kukubali
 
Unaweza kumsababishia aingie kwenye target aliyoingia prof na Lowasa. Ukitangaza nia unaweza kujikuta unaugua yabisi baridi!
 
Ndalichako hawezi jaman tangu ameingia walimu ambao ndo wawezeshaji wamewekwa benchi
Angeweza afanye haya;
i. Masters & PhD ipewe madaraja ya mishahara kama kwenye sector nyingine afya ni mfano mzuri
ii. Ahakikishe taaluma ya ualimu sio tu inarudishiwa hesma yake lakini maslai yaboreshwe hasa posho kama manjagu
iii. Ahakikishe sio tu bodi ya taaluma ya elimu inaanzishwa lakini bia kinaanzishwa chombo maalumu cha kusimamia elimu kama walivyopendekeza haki elimu.
Kinyume cha hapo the madam has insufficient legancy in comparison to her professionalism.
Walimu ingawa ni fani inayodahili wanafunzi wenye ufaulu mkubwa sana katika ngazi ya cheti na stashahada ila ndio fani inayolipa mishahara midogo isiyo na package ya aina yoyote ukilinganisha na fani nyingine kama ma.njagu au
 
Huyu mama hana tofauti na Makonda matamko mengi sana
Mie sina tatizo naye ila mwanamke kuwa rais siko tayari hata nikiamliwa kupigwa risasi hadharani niko tayari ...mwanamke ni msaidizi wa mwanaume, over!
 
Mmmhu hapo nihatareee maana marekebisho yake yanawaumiza pia wanyonge,ona leo watu wanalalamika mikopo hakuna chuoni.
 
<<<< MTOA mada Umepata Boom NN mbona MENO chenyuuuuu chi maputa hayooo>>>
 
Mbarawa naye pia

Ananyimwa fungu la miradi ya ujenzi
Bse he is muslim
 
Sizonje ndiye alitoa maagizo ya
Kufukuza UDOM
Kupunguza wanufaika wa mikopo
Kufutia usajili baadhi ya vyuo vikuu
Huyu mama Ni tarishi tuu
 
Kwa speed ya huyu Mh. Waziri, umakini na uzalendo anaouonesha katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku katika kuisimamia wizara nyeti ya elimu pamoja na taaluma za wanataaluma wengine, waziri huyu anastahili kuwa Rais 2025. (2020 Rais atabaki huyuhuyu tuliyenae).

Mtaje wa kwako unaemuona anafaa pia bila kujali anatoka chama gani.
Hafai. Anaenda kuua ajira za watu walioajiliwa ktk vyuo vikuu mbalimbali kwa kutangaza kuvifuta. Angejikita zaidi kwenye kuviboresha, siyo kuvifuta.
 
Kwa speed ya huyu Mh. Waziri, umakini na uzalendo anaouonesha katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku katika kuisimamia wizara nyeti ya elimu pamoja na taaluma za wanataaluma wengine, waziri huyu anastahili kuwa Rais 2025. (2020 Rais atabaki huyuhuyu tuliyenae).

Mtaje wa kwako unaemuona anafaa pia bila kujali anatoka chama gani.
Hapana usihemke kwa mambo madogo madogo yaliyo kufurahisha wewe, ambayo hata wewe ungeweza kuyafanya tena nadhani kwa ustadi zaidi ya hapo tambua uraisi siyo sawa na uchaguzi wa mwenye kiti wa wacheza kigodoro .
 
2015? mbona hujaeleweka na mwaka ulishapita
Isijali mkuu hawa ndio wale wenye mihemko bila tafakari ukimyang'anya kiwanja chake analalamika lakini ukijemga nyumba na ukampa chumba kimoja ndani ya kiwanja ulicho mnyang'anya atafurahi na kukushukuru kama wewe mungu wake. NI UJINGA TU!
 
Tatizo maamuzi yake ya kukurupuka,leo nimemwona kwenye taarifa ya habari Chanel 10 anasisitiza waalimu kujenga nidhamu kwa kuwazibiti wanafunzi wasiokuwa na maadili,nikajiuliza amesahau alivyokurupuka kuwafukuza Chuo vijana wa field kwa kumwazibu kijana aliyekosa nidhamu! Urais sio umwenyekiti wa mtaa kwamba kila mtu anaweza mudu.
 
Maprofesa na madokta wa kusomea (Phd) huwa wanakuwa sio wazuri sana kwenye nafasi ya urais. Wao wanafaa kwenye zaidi nafasi za utendaji sio maamuzi
 
Back
Top Bottom