Mwigulu Nchemba amvaa tena Spika wa Bunge.
Naibu waziri wa Fedha anayeshughulikia Sera ndg Mwigulu Nchemba ambaye anajulikana kama Sokoine wa Pili amemvaa Spika wa bunge na kupinga vikali njama za bunge za kuupinga tena mswaada wa kufuta misamaha ya kodi. Itakumbukwa wakati wa bajeti wakati spika wa bunge akiahirisha mswaada wa sheria ya kodi ya ongezeko la thamani Mwigulu alisimama bungeni na kumpinga Spika waziwazi na kusema anaweka kumbukumbu sawa kuwa hakubaliani na uamuzi huo kwakuwa hauna nia njema na watanzania masikini. Mwigulu alisema bungeni kuwa utaratibu kuwatoza kodi masikini na kuwasamehe matajiri ni utaratibu wa kinyonyaji wenye lengo la kukuza pengo kati ya walionacho na wasio nacho.
"Nimekuwa nikichukizwa na utaratibu wa kusamehe matajiri na kutoza kodi masikini tangu siku nyingi, nilifurahi nilipopata fursa ya kuwa wizara ya fedha ili niwe sauti ya masikini, tumeleta mswaada wa kufuta misamaha isiyo na tija, imepita ngazi zote, leo mhe Spika kusema mswaada huu haujajadiliwa na wadau sio sahihi, mimi napingana vikali na maneno yako, huko ni kuwatumikia matajiri. Hivi kama tunawafutia matajiri misamaha ambayo imekuwa ikiwanufaisha kwa gharama za wanyonge kuendelea kuwa masikini leo unataka ukawaulize , kwanza utawauliza swali gani kuwa tunataka kuwafutia misamaha ya kodi? Unategemea watajibuje? Huku ni kutokuchukua majukumu, ni kutokuchukua uongozi na nikutokutimiza wajibu alisema mwigulu kwa ujasiri na kwa sauti ya uongozi.
Hata hivyo pamoja na Mwigulu kuongea kwa ujasiri na kuungwa mkono na watanzania wengi hasa masikikini, rai yake ilipuuzwa na mswaada huo haukujadiliwa. Kitendo hicho kilionekana wazi kuwa matajiri walitoa rushwa kwa wenyeviti wa kamati, kwa wabunge na hata kwa baadhi ya mawaziri.
Alikaririwa mfanyabiashara mmoja akisema Mwigulu haeleweki, yaani jamaa hana tamaa ya fedha, yuko kama Nyerere vile, hana gari, hana nyumba, hana biashara lakini hataki kuengea na wafanyabiasha kitu chochote yeye anasema tulipe kodi basi. Jamaa hanunuliki kabisa, sijui JK amemtoa wapi. Wewe angalia anavyokamata wakwepa kodi unafikiri mawaziri wengine hawawajui wakwepakodi? No, wanachukua chao wanaondoka, wanatuliza boli, tazama alivyovalia njuga kufuta misamaha kwa matajiru, hana urafiki, wenzake wote wanasema misamaha iachwe tu mpk spika, lakini jamaa akasimama kumpinga hata spika waziwazi. Kwa mjibu wa sheria spika akiongea anatakuwa kuongea waziri mkuu lakini jamaa mzalendo sana jambo la watanzania hata haogopi popote wakati wowote kuwatetea watanzania.
Tulipomuuliza Mwigulu kwanini anakazania sana misamaha ya kodi kwa matajiri ifutwe na kwanini wenzake hawakuyaona hayo miaka yote? Mwigulu anasema
Kwanza, wafanyakazi wanatozwa kodi kubwa na wanaishi maisha magumu kwasababu mzigo mzito wameachiwa wao kwakuwa matajiri wanasamehewa kodi. Angalia nchi ya watu milion 45 wanaolipakodi milioni 1.8. Sio sahihi, tunawasamehe wafanyabiashara matajiri, makampuni makubwa halafu tunawanyonya walimu na wafanyakazi masikini,
Pili, wafanyakazi wakilipa kodi ndizo zibatoa huduma kwa matajiri hivyo tunawalipa wafanyakazi mishahara midogo kwakuwa kodi ndogo toka kwao inahudumia na matajiri waliosamehewa kodi. Hili sio sahihi hata kidigo. Hii nikuongeza pengo la aliyenacho na wasionacho, hatuwezi kuwa na nchi moja wengine wakiishi kama ulaya huku wengine wakiwa na maisha magumu kwa kukamuliwa.
Tatu, mimi nimetokana na masikini kabisa wa Tanzania, nawajua masikini na naujua umasikini, kuna watu wanakosa huduma kwa ajili ya ufinyu wa makusanyo. Haiingii akilini kwamba tuna watoto wa masikini zaidi ya elfu 40 wakose mikopo ya kuibgia chuo kikuu huku tukiwa tumesamehe kodi migodi, makampuni, matajiri na wafanyabiasha, tunataka tufute misamaha tukusanye kodi tuwasomeshe watoto wa masikini.
Haiwezekani tukasamehe kodi migodi, makampuni tajiri na matajiri halafu tukahangaishane na wajane, yatima, wazee na masikini kuhusu ada elfu 20 ya sekondani.
Nataka nikusanye kodi halafu ada hizi elfu 20 zifutwe. "Tutoze kodi kwa matajiri tuwasomeshe watoto wa masikini" huu ndio mchango wa uwepo wangu mtoto wa masikini kwenye nafasi nyeti kwa masikini wa Tanzania.
Kadhalika, haiwezekani masikini wanakosa dawa, wanalala chini, wajawazito wanajifungua gizani huku matajiri wakisamehewa kodi, matajiri wakiugua wanatibiwa ulaya kwa kodi za masikini, tunataka kutoza kodi ili masikini wapate huduma za matibabu. Tunafuta misamaha ya kodi kwa matajiri ili tutoe huduma za matibabu kwa masikini.
Haiwezekani masini wanakosa maji, akina mama wanabakwa wakutafuta maji usiku huku tukisamehe kodi, tunataka tutoze kodi ilituwape masikini maji safi na salama.
Pia tunatoza kodi ili Nchi yetu iache utegemezi kwenye misaada yenye mashart na masimango.
Hata hivyo dawati letu limepata taarifa kuwa Mwigulu anapigwa vita na matajiri na hata viongozi wenzake waliowekwa mifukoni na matajiri. Zipo taarifa kuwa kamati ya bunge inapinga mswaada huo usiingie tena bungeni. Mwigulu alimuulixa Spika kwa ukali unataka mswaada huu usiingie bungeni watanzania masikini wamekukosea nini hata usiwahurumie? Tazama wafanyakazi wanatozwa kodi kubwa hivi, wanalipwa kidogo, hata hawawezi kuwahonga wabunge, mswaada huu kukwama, misamaha kutofutwa ni wito wa matajiri, kwanini unaitikia wito wa matajiri? Nimechukizwa sana na hili. Zipo taarifa kuwa matajiri wanaxungusha fedha kwenye kamati, kw wabunge na kamati ya uongozi ili wazuie mswaada huu kupitishwa.
Watanzania wote , wafanyakazi, wanafunzi tuliokosa mikopo, wanyonge, masikini, wazalendo tumuunge mkono ndg Mwigulu Nchemba, (Sokoine wa Pili) Mzalendo wetu wa Vitendo kupigania kodi ilipwe na matajiri ili masikini wapate huduma. Hata kwa maadamano tushinikize bunge lipitishe sheria ya kufuta misamaha ya kodi kwa matajiri. TUNAIMANI NA MWIGULU