Prof. Mwandosya kugombea Urais 2015

Prof. Mwandosya kugombea Urais 2015

Lowassa mzima ana nguvu kabisa nimemuona jana kwenye kikao cha wabunge wa Mkoa wa Arusha
 
Wagombea wote wa Uraisi kabla ya mchujo wowote wa kichama kila moja apimwe afya na kuwa na cheti cha uthibitisho kuhusu hali ya afya yake k.m. ukimwi, kisukari,kiwango cha ukichaa,usahaulifu, magonjwa ya moyo, n.k. Sii vyema kuwa na Raisi ambaye muda mwingi anautumia kwa matibabu. Tupate Raisi mwenye afya njema na kama ataanza kuugua akiwa tayari amechaguliwa hilo ni shauri jingine, tutamvumilia aendelee. Lakini kuchagua Raisi ambae tayaari ana mgogoro wa afya ni hatari kwa mustakabali wa taifa.

Pendekeza wakapimwe wapi lakini siyo bongo!
 
Na vijana zaidi ya saba wamejitokeza kuliwania jimbo la RUNGWE MASHARIKI baada ya yeye kuaga jimboni.
ko mtifuano utakuwa mkali kati ya ukanda wa mwakaleli na rwangwa ambako vijana wameonyesha nia.
 
Prof. Mark Mwandosya mbunge wa jimbo la Rungwe Mashariki na Waziri asiyekuwa na wizara maalum amesema kuwa hatogombea tena ubunge bali urais. Ni mwendelezo wa wimbi la watangaza nia linaloshika kasi.
Source : Mtanzania gazeti la leo.


Labda awe Raisi wa Apolo India lkn SIYO wa Nchi Yangu!
 
Kupunguza hii long list wangeweka kigezo cha kupima ukimwi hawa wagombea ..nina imani tutapata watu wachache sana
Mzee kwa nini ukimwi usiseme afya kwa ujumla. Huu ni ubaguzi!
 
Hivi ukipewa urais ukiwa mzima wa afya ndiyo huwezi kuugua baada ya kupata urais?
 
Iwe mandatory kwa wale wote wanaotaka kugombea kiti cha URAIS wapimwe afya zao; hilo hufanyika nchi nyingi na hufanywa na jopo la madaktari wenye maadili ya kizalendo. Hili in fact linatakiwa liingizwe kwenye katiba ya nchi kuhusu afya za wagombea wa nafasi za uongozi wa nchi. CCM kwavile viongozi wao wengi ni wagonjwa watalipinga hili kufa na kupona lakini hawatakuwa wanaitendea haki nchi!!

Mkuu katiba inasemaje kuhusu hilo la afya? Afadahri kuwa na rais ambaye afya yake siyo nzuri lkn anaweza kuitetea katiba ya nchi na kutawala kutokana katiba iliyopo. Haina maana kabisa kuwa na rais mwenye afya wakati hayuko tayari kutawala kufuatana na katiba. Angalia hotuba ya mwl kuhsu nyufa tatu katika taifa letu. Anasema hawa watu hatuwaitaji hii ni pamoja na huyu DHAIFU!!!
 
Tanzania Afya ya mgombea sio tatizo hata ukiwa na ugonjwa wa kuanguka anguka tutaweka mabaunsa wa kumbeba na gari la hospitali (mobile hospital) tea
Afya yake hairuhusu. Apumzike.
 
Hii ni faida ya kuwa na hazina! Nadhani CDM wakijitokeza wawili watakaofuata watakuwa --- ester lissu, mariamu mbowe, n.k kweli hazina ya CCM ni balaaa!
 
Jamani wabaki akina January, Ngeleja,Lowassa na Nchimbi wenye afya njema na uwezo mkubwa na wako makini kuliko Prof!
 
Prof. Mark Mwandosya mbunge wa jimbo la Rungwe Mashariki na Waziri asiyekuwa na wizara maalum amesema kuwa hatogombea tena ubunge bali urais. Ni mwendelezo wa wimbi la watangaza nia linaloshika kasi.
Source : Mtanzania gazeti la leo.
Hta angegombea asingepata
 
Back
Top Bottom