Prof. Mwandosya amchana Mkapa

Prof. Mwandosya amchana Mkapa

neno mpumbavu hutamkwa na MTU mpumbavu nakushangiliwa na wapumbavu wenyewe
Mkuu unakumbuka Sugu alisema PM ni mpumbavu akapelekwa mahakamani akitetewa na Tundu Lissu na mahakama ikaamua kwamba mpumbavu siyo tu?
 
We mtoto wa 86 Prof. Mwandosya anakuwaje schoolmate wako.
School mate is different from class mate!!!! Check well Ila hizi sheria za mitandao zingesimamishwa kipindi hiki cha kampeni tukashugulika na sheria za majukwaani ingesaidia kupata haraka watakaoenda The Hague
 
Hapa najua kuna wanafiki kibao, sasa hivi WANAMKUBALI Prof. Mwandosya sababu kasema wanachotaka kusikia, siku akisema kitu ambacho hawataki kusikia na kukikubali licha ya kwamba chaweza kuwa na ukweli ndani yake atageukwa na kuwa mchumia tumbo!

Ndio demokrasia ilivyo. Ukiona jamii fulani wanakubaliana kila kitu ujue hakuna demokrasia humo! Huo ni udikteta
 
Mkapa hana tofauti na teja wa kule tandale kwa tumbo.
 
Mkapa amejidhalilisha sana ameonekana ni kama jitu lisilo na heshima mbele ya jamii.
Huyu angepata kichapa kama cha kipindi kile cha kuchwapwa na sturi akatembelea magongo, huko lushoto kwenye maua hakuna nyoka mwenye sumu kali angalau akamtengua mguu mmoja.
 
Haki itabaki kuwa haki
Na ukweli itabaki kuwa ukweli
Hata kama wengi hawaujubali
Mwandosa aghalabu ni
mtu mkweli na muaminifu
kama alivyo lowasa.
 
Waite majina yote mabaya kadiri wawezavyo ila tunawapa pole maana wamechelewa. Watanzania wanajua wapumbavu na malofa ni akina nani! Mfa maji siku zote haachi kutapatapa ndivyo ilivyo CCM na viongozi wake. Tunamshukuru mzee Mkapa kwa kutuongezea mtaji wa kisiasa.
 
MWANASIASA mashuhuri nchini, Prof. Mark Mwandosya, amemtolea uvivu, Rais mstaafu Benjamin Mkapa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Prof. Mwandosya ambaye alikuwa mmoja wa wagombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ambaye jina lake liliondolewa katika hatua za awali za kinyang’anyiro hicho anasema, “ni muhimu kama viongozi, kuvumiliana na kuheshimiana,” ili taifa lisiingie katika machufuko.

Akiandika katika ukurasa wake wa facebook, Prof. Mwandosya amesema, taifa linapita katika kipindi kigumu, hivyo ni vema wanasiasa na wananchi wengine wakajenga utamaduni wa kuvumiliana.


Amesema, “katika kipindi hiki muhimu, kama taifa, inatupasa tuzingatie; kuvumiliana, kuheshimiana, kukubaliana, kukubali kutokubaliana, kushindana kwa hoja, na kutumia lugha yenye staha.”


Prof. Mwandosya anasema, “Msaafu Mtakatifu unatukumbusha ‘…vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao huvuna majivuno makuu.”


Andishi la Prof. Mwandosya limekuja siku tatu baada ya Mkapa kufungulia bomba la matusi kwa kuwaita viongozi wakuu wa upinzani nchini na wafuasi wao, kuwa marofa na wapumbavu.


Mkapa alisema wapinzani wanaosema vyao vyao ni vya ukombozi ni wapumbavu na malofa kwa kuwa Tanzania ilishakombolewa na vyama vya Tanganyika National Union (Tanu) na Afro Shirazi Party (ASP).


Bila kutaja jina la Mkapa, Prof. Mwandosya aandika kwa njia ya kuonya, “…angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana…”


Anasema, “Msaafu Mtakatifu unatuonya pia “…kwa maneno yako utahesabiwa haki na kwa maneno yako utahukumiwa….”


Tangu Edward Lowassa, kujiunga na upinzani na baadaye Fredrick Sumaye, kumfuata kwa lengo la kuongeza nguvu ya kuondoa CCM madarakani, kumekuwa na mihamko ya viongozi wakuu wa chama hicho na serikali kuzuia upinzani kushika dola.


Taarifa zinasema, mihamko hiyo, ndiyo iliyomsukuma Mkapa kutukana baada ya kuona kitumbua chake kinaingia mchanga.

Chanzo: MwanaHalisi Online

vitu vingine nikujiongeza nakufikiri nje ya box umesema mwanzo Prof Mwandosi amchana Mkapa, mwisho unakanusha hakutaja jina una akili kweli wewe mwandishi? Ndio maana mnafungiwa kwa njaa zenu. Mbona akina Lowasa na mambowe wanatukana kila siku au ndio akinya bata kaharisha? Mkapa haku2kana ila alikuwa na mengi moyon haku2ambia Lowasa na wenzake walipaswa kupigwa za kichwa mambo waliyo yafanya. Mungu awarehem
 
masikhara hayo mkuu, kuwa na wewe ushakuwa babu ama??

nimesema my school mate na sio my class mate..ila
kwa ufupi kaa ukifahamu mwandosya mpaka kafika kuwa
profesa kuna sehemu nyingi sana kasoma na miongoni
mwa sehemu hizo nami nimepitia ...sasa sina budi kumpongeza
kwa kupikika na kuiva kisawa sawa.
 
......huelewi nn sasa, kasema school mate na sio classmate; inawezekana moja kasoma enzi za ukoloni mwingine baada ya ukoloni, mfano wa shule kama hizi ni MALANGALI

Hata mtoto atakayezaliwa kesho anaweza kuja kuwa school mate wake endapo tu atasoma shule aliyoisoma Prof Mwandosya.

Classmate ndiyo suala lingine hapo...

Chunyakati Primary School au Malangali Secondary School?
May be Dar Institute of Technology?

Nashukuruni sana kwa kunielewa vema...nami pia nimewaelewa vema.
ninaamini kabisa nanyi ni wenzangu ambao tulisoma kipindi kile tulipokuwa
tunasema " I am going to school" na sio hawa vijana wa leo wanaosema kuwa
" I am going to the school".
 
Nashukuruni sana kwa kunielewa vema...nami pia nimewaelewa vema.
ninaamini kabisa nanyi ni wenzangu ambao tulisoma kipindi kile tulipokuwa
tunasema " I am going to school" na sio hawa vijana wa leo wanaosema kuwa
" I am going to the school".

Acheni ngonjera,
 
Nashukuruni sana kwa kunielewa vema...nami pia nimewaelewa vema.
ninaamini kabisa nanyi ni wenzangu ambao tulisoma kipindi kile tulipokuwa
tunasema " I am going to school" na sio hawa vijana wa leo wanaosema kuwa
" I am going to the school".

Punguza mbwembwe
 
Mwandosya ana sifa kuu moja nayo ni Kiongozi. Kumbuka hata issue ya ESCROW aliluwa kinyume na serikali kwa msimamo wake wa wazi uliokuwa ukisimamia ukweli. Hakika huyu ni mtu muhimu sana kwa siasa za mageuzi kwa sasa sijui anachelewa nini kuja UKAWA!!!!!!!!!! karibu sana Mwandosya
 
Back
Top Bottom