Prof. Mwamila anafanya mambo makubwa Nelson Mandela. Anastahili pongezi

Njaare

JF-Expert Member
Sep 26, 2010
1,081
275
Wana JF naomba niwashirikishe niliyoyakuta kwenye Chuo kikuu kipya kilichoko Arusha kinachoitwa Nelson Mandela African institute of Sciences and Technology. Chuo hiki kipya kiko katika hatua za mwisho za awamu ya kwanza za Ujenzi na kimedahili wanafunzi kuazia mwaka huu wa masomo.

Chuo hiki kiko chini ya Prof. Burton Mwamila aliekuwa Dean wa FoE na hatimaye Principle wa CoET ya UDSM. Professor huyu ameweza kusimamia vyema fedha za serikali na hatimaye chuo kikasimama. Kwa taarifa zaidi kuhusu Chuo vist The Nelson Mandela African Institute of Science and Technology.

Wito wangu kwa wakuu wa vyuo vingine waende wakatembelee NM-AIST wajifunze jinsi ya kujenga hoja na kusimamia vizuri fedha za maendeleo na sii kulipana posho za vikao tu.
 
Yaelekea nguvu yake sasa imepungua maana usimamizi wa fedha za serikali katika masuala yanayohusu utafiti wa wanafunzi (uzamili na uzamivu) unaonekana kwenda mrama, hali iliyosababisha wanafunzi kusimamisha shughuli za masomo na utafiti kwa muda wa siku mbili ili kujadili na kutafuta ufumbuzi wa changamoto hizo
 
Back
Top Bottom