Prof. Muhongo: Nimeshafanya uamuzi

Prof. Muhongo: Nimeshafanya uamuzi

Yaani hii nchi ni kama kituko hivi, ingekuwa hao wanafunzi wamefanya hivyo kusupport upinzani ungesikia wanachanganya siasa na masomo, lakini kwa ajili huu upuuzi unafanywa na wanaccm hakuna shida. Juzi hapa tumesikia maaskofu wanasema waumini wao waipigie katiba pendekezwa kura ya hapana, viongozi wa serekali mishipa juu kwa povu lakini hatuoni hata mmoja akikemea kitendo cha mashehe kwenda monduli kumuomba Lowassa. Tunaomba viongozi wa dini muwe makini na siasa za nchi yetu na muhakikishe mnakuwa chachu ya elimu ya uraia kwani mkikaa kimya kuna uhuni mkubwa utakuja kulikumba taifa letu na tushindwe pa kutokea.
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Hapo ni kutaka kupunguza kura za Lowasa,lakini hamuwezi
 
Nasikitika sana nikiona make ya wasomi wetu! Nchi zote zilizopata maendeleo duniani zilisaidiwa na mawazo yenye ubunifu ya wasomi wake. Sisi hapa Bongo badala ya watoto kuchimba matabu wanashinda wanazunguka katika nyumba za wagombea kuomba hela ya lunch na maji ya kunywa! Watasoma saa ngapi???Hii ni aibu kwa taifa. Tutabaki nyuma kwa miongo mingi kama aina za wasomi tunaowasubiri watukwamue ni hii!! Very sorry
 
Huyu Mhongo dawa yake ni Reginald Mengi wa IPP basi. Hapo kwisha kabisa.
alimdharau sana Mengi bila Mengi ni mtu makini sana hata JK anamjua .dharau na kiburi vya Prof.Muhongo leo yuko wapi ndo ameshakufa kisiasa tayari
 
yetu macho kuna nani kachota pesa za kampeni maaana hawa watu ni mchwa
 
qKwenye hiyo orodha huwezi kuwakosa Wajita!! Kama mwendo wenyewe ndo huu na sisi Usukumani ngoja tuandamane tulitume jembe letu Joka lenye Makengeza lijiandae kuchukua fomu ya U-Rais!!
 
Nchi hii ni ya ajabu sana. Hasa katika kipindi cha miaka kumi iliyopita imepanda chati sana katika maajabu yake. Ukitaka kuwa maarufu hapa ni kuhujumu nchi na kutengeneza mjadala wa kukujadili na mwisho hata kama utafukuzwa au kujiuzulu basi wewe ni shujaa na unastahili kujinadi kuwa waweza kuongoza nchi. Maana yake ni nini? Maana yake ni kuwa ni nchi ya mazuzu ambao kwao mwizi na mfisadi maarufu ni mtu makini. Mfano ni hata ule wa Lowasa, hao hao CCM walimwita fisadi,gamba na majina mengi lakini leo ndio wanapigana vikumbo kwenda kumbeba eti awe kiongozi!
TUMELOGWA.

Ndio wamerogwa na uchawi wa Kizungu huo kaka...FEDHWA RUSHWA...na akiupata Urahisi (URAIS) mbona kazi mpaka airudishe gharama yake ya haya yote anayoyafadhili yeye na MARAFIKI ZAKE kwa mgongo wa Ameombwa Ameombwa..tutakuwa tumechoka..tutakuwa wa mwisho katika kila kituuuu
 
"Nimeshafanya uamuzi kuhusu suala la Urais katika uchaguzi ujao. Ninachosubiri ni chama kutangaza ratiba"

Mmh! Urais wa mwaka.huu tutasikia mengi. Atakayechuana naye in the event anachaguliwa ana uhakika wa kupita bila shida kwa kuwa huyu anafaa tu kuwa mhadhiri chuo kikuu tena akisimamia wanafunzi wa uzamili na uzamivu kwa kuwa kauli zake ni mbovu.
 
"Nimeshafanya uamuzi kuhusu suala la Urais katika uchaguzi ujao. Ninachosubiri ni chama kutangaza ratiba"

Akituambia UKWELI juu ya sakata la ESCROW na nani alimshawishi wajichotee kwenye hiyo account,tutamfikiria kidogo.
 
OMG!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Ama kweli Tanzania imekuwa kichwa cha mwendawazimu! Hata Muongo anataka kugombea Urais?! kama ni hivi; Sitashangaa kusikia hata Livingstone Lusinde; Assumpta Mshama; Hawa Ghasia; Aden Rage na Maji Marefu nao wakijitosa ulingoni! Ama kweli Tanzania yangu umekuwa hivyo mpaka uongozwe na watu kama hawa?! God save my country!
 
Akituambia UKWELI juu ya sakata la ESCROW na nani alimshawishi wajichotee kwenye hiyo account,tutamfikiria kidogo.

Suala la Escrow mpaka sasa bado haujilielewa mkuu!!! Kwani aliyekuwa anazitunza ni nani??? Na umeme ulifuliwa na nani? Na sasa nani anaendelea kuzalisha?? Ukifikiria zaidi utaona Muhongo alikuwa mchapakazi sana.
 
Back
Top Bottom