Ushasahau kuwa huyu Muhongo ni katika list ya wana CCM wanaopendwa hapa JF?
Wengine ni:
Magufuli
Mwakyembe
Ukitaka ugomvi na wana JF ambao husema kuwa CCM ni mafisadi bas wewe waguse hao waheshimiwa
Typical JF double standards
Kwa mtu asiye na technical background mgawoj maana yake ni kukosa umeme na si kukatika kwa umeme.
Kuna tofauti kubwa kati ya terminologies hizo mbili.
Mgawo is a more self centered assesment ya upatikanaji wa umeme, maana yake kwa vile mimi nakosa umeme basi kuna mtu mwingine anapata badala yangu, na pengine kwa kupendekewa!
Kukatika kwa umeme kuna maana nyingine, ambayo inaweza kumaanisha failure of the system, au dalili za matatizo ambayo hayajatatuliwa.
Wana JF lazima kuwa analytical na kulitazama tatizo kwa uwigo mpana zaidi ya kufikiria mgawo.
Ndiyo, kuna matatizo ktika upatikanaji wa umeme, hiyo diyo siri, ni tatizo la msingi lililomwondoa hadi Waziri Mkuu.
Umeme una pande tatu mpaka umfikie mtumiaji.
Kuna ufuaji kutoka kwenye vinu, iwe vya maji au majenereta.
Pili kuna usafirishaji wa huo umeme, kwa msongo mkubwa(high voltage)
Tatu, kuna kuupoza kwa vituo (kwa transformer)na kuugawa umeme huo kwa msongo mdogo(low voltage inayotumika majumbani).
Katika hatua zote tatu kuna matatizo makubwa, uzalishaji ni haba.
Usafirishaji wa umeme vile vile miundombinu yake ilijengwa na Awamu ya Kwanza ya Mwalimu.
Usambazaji vile vile una matatizo makubwa, kwa mfano hata kupata transformer huwa kazi kweli kweli.
Ni vema wana JF kutambua kuwa breakdown katika stage yoyote , na zinatokea tena sana, aidha uzalishaji, usafirishaji na ugawaji wa umeme kuna athari ambazo hata Muhongo hawezi kuzitatua.
Mbaya zaidi kuna taasisi ambazo hazilipii huduma hii na hivi karibuni deni la Zanzibar la Bilioni 50, lilikuwa written off!
Mafisadi nao hawako nyuma kuhujumu huduma hii na kujipatia pao la fasta, hatujawasahau NET GROUP SOLUTIOS ya South Africa.
Wakati wa utwala wa kampuni hiyo hapakuwepo uwekezaji wa aina yoyote katika kurepair mitambo wala distribution system.i
Hii ni pamoja na wale watumiaji wakubwa ambao wanaiba huduma hii.
Sasa hata tukiimba na kulibebea bango jina la Muhongo ni kazi bure.
Hakuna mgao wala nini, ila umeme hautoshi na miundombinu yake imechoka.
Period.