Prof. Mlambiti wa SUA - Jiwe lililosahaulika

Prof. Mlambiti wa SUA - Jiwe lililosahaulika

Umenikumbusha hisia alizo nazo prof. Tarimo.
Katika Dept ya Eng. Pale sua. Inamuuma sana wanasiasa wanapoongea kuhusu miradi mbali mbali ya maji.ambayo mingi imekufa kwa uzembe wa hawa watu.

N hatarii prof tarimo naskia bado yupo ila sifa kwake haziishi na n mfuasi wa nyerere balaaa humwambii kitu
 
Mimi namkumbuka Dr. Augustine Lyatonga Mrema akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Naibu Waziri Mkuu miaka ya 90. Alikuwa ni mzee wa kutoa oda ya siku 7 na jambo linatekelezwa, alitatua migogoro sehemu mbali mbali za nchi na nina uhakika hata mgogoro wa Wafugaji na Wakulima uliopo sasa hivi pale Babati angeutatua bila tatizo. Sijui huyu Mzee yupo wapi sasa hivi. Shikamoo Dokta Augustine Lyatonga Mrema popote ulipo.
 
Prof. Pereka yuko wapi jamani. Physiologist wa kutisha. Amenijengea foundation ambayo haisahauliki kichwani kwangu. Nikienda hosp sipati shida na nikidanganywa naelewa

Uliiga na mikiki mikiki yake?
 
Kuna kipindi alikuwa anaogopwa kwamba anatema sumu.. Labda SUA waliogopa hilo... Maana ingekua enzi hzo chadema iko moto lazima angehusishwa nao
Nadhani siasa ndio zimesababisha nasikia hata uchaguzi uliopita aliwachachafya ccm katika ubunge kupitia chadema
 
Mkuu ki ukweli kuna mwaka alimuuliza mkapa swali pale freedom square.Mkapa what did i told you about re opening rural roads in my proposal?have you tried to sit with your convoy and give us the feedback.lakini wapambe wa rais walilivuruga.Lakini baadae ikaja julikana ya kuwa alimpa some proposal juu ya uchumi wa kilimo.Rais hakuwa na jibu,hakufuata ushauri wa prof Mlambiti.Kile kichwa bwana
 
Mkuu ki ukweli kuna mwaka alimuuliza mkapa swali pale freedom square.Mkapa what did i told you about re opening rural roads in my proposal?have you tried to sit with your convoy and give us the feedback.lakini wapambe wa rais walilivuruga.Lakini baadae ikaja julikana ya kuwa alimpa some proposal juu ya uchumi wa kilimo.Rais hakuwa na jibu,hakufuata ushauri wa prof Mlambiti.Kile kichwa bwana
Nakumbuka sana ile incidence mkuu na tena watu waliposikia Prof Mlambiti anauliza swali watu wote walishangilia sana na kiukweli walijua nini kitaulizwa
 
Mkuu ki ukweli kuna mwaka alimuuliza mkapa swali pale freedom square.Mkapa what did i told you about re opening rural roads in my proposal?have you tried to sit with your convoy and give us the feedback.lakini wapambe wa rais walilivuruga.Lakini baadae ikaja julikana ya kuwa alimpa some proposal juu ya uchumi wa kilimo.Rais hakuwa na jibu,hakufuata ushauri wa prof Mlambiti.Kile kichwa bwana

Mimi nimekuelewa lakini sidhani prof aliongea kiingereza hicho ulichokiandika au umemnukuu vibaya.
 
Mwaka 2005 katika maadhimisho ya Sokoine day, Profesa Mlambiti aliomba maiki na kumhoji mgeni rasmi maswali mawili, akihoji 'why' akajibiwa 'how' ilikuwa fora sana siku hiyo tukiwa kimya Freedom Square Mazimbu. Mgeni rasmi alikuwa Rais Mstaafu wa awamu ya tatu.
 
Prof. Mlambiti ni jembe, nakumbuka 2004 alikuwa anatoa story za kwenda kugombea ubunge 2005 kupitia chama chake flani hivi.
 
Gabagambi yupo REPOA. Alikosoa government ya Mkwere sasa Nondo hajalibiwi. Aidha Segerea au ukae kimya
Yupo SUA hivi sasa ndio mkuu wa school of agricultural economic and agribusiness baada ya mfumo wa chuo kubadilika.
 
Mwaka 2005 katika maadhimisho ya Sokoine day, Profesa Mlambiti aliomba maiki na kumhoji mgeni rasmi maswali mawili, akihoji 'why' akajibiwa 'how' ilikuwa fora sana siku hiyo tukiwa kimya Freedom Square Mazimbu. Mgeni rasmi alikuwa Rais Mstaafu wa awamu ya tatu.
Siku Ile Prof. Mlambiti alitia fora...!
 
Leo nimekua nikitafakari mambo mbalimbali yanayoikabili nchi hii na nikajikuta namkumbuka prof.Mlambiti kwa mambo mbalimbali na jinsi alivyokua anaonesha hisia zake anavyoumizwa na mustakabali wa nchi hii.

Kwanza hajawahi kuamini kama CCM inania ya dhati ya kuikwamua nchi hii kiuchumi na kimaendeleo japo anaamini kuna watu ndani ya CCM wangeweza kujilipua na kuifikisha TZ mbali sana na hawakuwahi kufanya hivyo na hawatofanya hivyo... Akiwemo Raisi wa sasa na aliyepita kabla yake (Mkapa).

Prof. Mlambiti (a.k.a Babu) alitufundisha pale SUA miaka ya 2000 mwanzoni ni mtu aliyethubutu mara kadhaa kupingana na Mwalimu Nyerere juu ya Sera za kilimo za nchi hii akiamini ubunifu juu ya kilimo ungekomboa zaidi 80% ya wananchi wa TZ kama serikali ikiamua kuwekeza katika tafiti na rasilimali zingine pamoja na ukuzaji wa viwanda na masoko ndani na nje ya nchi.

Prof. Mlambiti daima fikra zake haziwezi kufa kichwani mwa mtu yeyote aliyemfundisha kwa kuwa aliongea maono, ukweli, na hali halisi bila kujali itikadi zozote na alisema ni kizazi kingine ndicho kitaibadilisha Tanzania na ni kizazi kitakachokuja kuishangaa sana historia ya kizazi hiki cha sasa kwa uzembe na uvivu mkubwa wa kufikiri.

Prof. Mlambiti ambaye alitufundisha sana elimu ya ujasiriamali (japo ilikua kama kitu kigeni sana kwa jamii ya TZ) ni mzee aliyetuhamasisha sana vijana kuumiza akili na kujitengenezea ajira kuondokana na utumwa wa fikra ambao vijana wote wa wakati ule tulikua nao.. Na waliofuata aliyoyafundisha na kuthubutu si wenzetu tena leo hii kiuchumi.

Ni mtu pekee ambaye huja mara nyingi kichwani mwangu kila linapotokea vuguvugu la uchaguzi, scandal za kifisadi,migogoro ya ardhi, migogoro ya kidini na hata migogoro ya kiuchumi kwa sababu ya maono na mafundisho yake na mara zote huwa natamani nijue ni nini anafikiria kwa wakati huo.

Kiufupi mzee yule ni hazina kubwa iliyosahaulika..na yeyote aliyewahi kuhudhuria darasa lake hawezi kusahau maishani mwake mafundisho ya yule mzee.
Ni kweli kabisa prof Mlambiti, mzee wa Rural Economy, ni kichwa na alikuwa anapinga sana sera za mwalimu Nyerere. Yule mzee anaona mbali sana. Hv bado yupo SUA?
 
Bibi yupo bado anakimbiza cardiovascular kinoma! Alishastaafu ila kwa sasa anapiga kwa mkataba!!
Yule bibi ni kichwa. Hadi MUHAS walikuwa wanamuazima akawasaidie kufundisha. Yule mama achana naye kabisa.
 
Sembuche kwa sasa yuko kwao kigugu turian kastaafu hili n gwiji la mathematics sijawah ona alikua UDSM miaka ya 70s na akaenda Zimbabwe miaka ya 80s na baadae kwenda sua 1998 na sasa kastaafu
Mkuu we acha tu....yule baba anajua Hesabu sijapata kuona....ilitakiwa SUA wamuongeze mkataba...hawatakaa waje wampate mwalimu kama yule. Ni mzee lakini hesabu zimapanda utadhani amemeza calculator! Ile kichwa imesoma Warwick University (England).
 
Back
Top Bottom