PreGE2025 Prof Lipumba: CUF Kitawakomboa Watanzania

PreGE2025 Prof Lipumba: CUF Kitawakomboa Watanzania

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Wakuu Prof. anadai CUF itawakomboa Watanzania, au G55 waende huko tu

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

===

Mwenyekiti wa chama cha Wananchi, Prof. Ibrahim Lipumba, amesema chama chake kina sera za kuwakomboa watanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii na kujenga nchi yenye haki sawa na furaha kwa Watanzania wote.

Amesema katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu anatoa wito kwa wananchi kuendelea kujiunga na CUF na kujitokeza kugombea nafasi za udiwani, uwakilishi, ubunge, pamoja na urais Zanzibar na Tanzania bara.

Prof. Lipumba amesema hayo jana, Dar es Salaam, Aprili 6, mwaka huu, katika taarifa yake kwa umma kupitia vyombo vya habari juu ya mtazamo wa CUF kisiasa na kiuchumi.

“Ili kupambana na umasikini CUF imependkeza kuanza kutekeleza hatua kwa hatua sera ya Kipato cha Msingi (Universal Basic Income) ni Haki ya kila Mtanzania.
1744030250774.png

“Huduma za afya bado hafifu. Eneo moja la mafanikio ni kupunguza vifo vya kina mama waja wazito kutoka 556 katika kila wajawazito laki moja mwaka 2016 na kufikia 104 mwaka 2022.

“Vifo vya watoto wachanga chini ya mwaka mmoja vimepungua toka 99 kati ya watoto 1000 mwaka 1999 na kufikia 43 mwaka 2022. 32. Hata hivyo Sera ya serikali kuwa wanawake wajawazito, watoto na wazee watatibiwa bure ni danganya toto.

“Hakuna tiba ya bure. Hali halisi kwenye shule za msingi za umma kote nchini ni nzito sana kwa wazazi na walezi. Kila siku kila mwanafunzi hulazimishwa kupeleka baina ya shilingi 800 na shilingi 1,500 hususan maeneo ya mijini kwa michango mbalimbali.
 
Wakuu Prof. anadai CUF itawakomboa Watanzania, au G55 waende huko tu

===

Mwenyekiti wa chama cha Wananchi, Prof. Ibrahim Lipumba, amesema chama chake kina sera za kuwakomboa watanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii na kujenga nchi yenye haki sawa na furaha kwa Watanzania wote.

Amesema katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu anatoa wito kwa wananchi kuendelea kujiunga na CUF na kujitokeza kugombea nafasi za udiwani, uwakilishi, ubunge, pamoja na urais Zanzibar na Tanzania bara.

Prof. Lipumba amesema hayo jana, Dar es Salaam, Aprili 6, mwaka huu, katika taarifa yake kwa umma kupitia vyombo vya habari juu ya mtazamo wa CUF kisiasa na kiuchumi.

“Ili kupambana na umasikini CUF imependkeza kuanza kutekeleza hatua kwa hatua sera ya Kipato cha Msingi (Universal Basic Income) ni Haki ya kila Mtanzania.
View attachment 3295873
“Huduma za afya bado hafifu. Eneo moja la mafanikio ni kupunguza vifo vya kina mama waja wazito kutoka 556 katika kila wajawazito laki moja mwaka 2016 na kufikia 104 mwaka 2022.

“Vifo vya watoto wachanga chini ya mwaka mmoja vimepungua toka 99 kati ya watoto 1000 mwaka 1999 na kufikia 43 mwaka 2022. 32. Hata hivyo Sera ya serikali kuwa wanawake wajawazito, watoto na wazee watatibiwa bure ni danganya toto.

“Hakuna tiba ya bure. Hali halisi kwenye shule za msingi za umma kote nchini ni nzito sana kwa wazazi na walezi. Kila siku kila mwanafunzi hulazimishwa kupeleka baina ya shilingi 800 na shilingi 1,500 hususan maeneo ya mijini kwa michango mbalimbali.
Kimkomboe kwanza yeye kabla ya kuwakomboa watanzania
 
Yaaaani sasa hivi nchi inapitia wakati mgumu sana. Yaani huwezi kutofautisha nani hajakwenda shule, nani kaishia STD 7, nani wa secondary, nani wa cheti, nani wa diploma, NANI WA DEGREE, NANI MWENYE MASTERS, KWENYE UDOCTOR NDIO USISEME KABISA, kwa maprofesa nako ni hoi been taabani.
Hivi hakunaga Masters ya heshima na mimi nikaiombe
Kila kukipambazuka ni vioja kwa kwenda mbele
 
Mkuu unamaanisha, bado hajakomboka?
Hukusikia ile story ya uchaguzi wa 2015? Aliahidiwa fedha nyingi ili ajiondoe UKAWA na akafanya hivyo. Kweli wakamwingizia zote kwenye account yake na akaziona. Akaamua kwenda kula maisha kidogo akaenda Burundi au Rwanda sikumbuki vizuri na akaweza kutumia kiasi kidogo. Kurudi akakuta account iko kavu. Akaamua kwenda Ikulu kwa Magufuli kwenda kuulizia na akajibiwa hamna fedha. Unaambiwa alitoka ikulu amelowa nguo jasho kama amenyeshewa mvua ya masika.
1744033987672.jpeg
 
Nadhani Tanzania ni mojawapo ya nchi kituko kwenye sayari ya Dunia.
 
😄😄😄😄😄😄🤣🤣🤣🤣 huyu mzee japo tupo mkoa mmoja ila simkubali akili zake zimezeheka sijui haoni aibu chama kufa mikononi mwake. Chama hakina ushawishi wowote hakina tofauti na CHAUMA au UDP
 
Back
Top Bottom