Prof Lipumba azidi kumshambulia Mengi

wewe ndio hauchambui mada vizuri, lazima ujue lipumba alisema nini mara ya kwanza juu ya mengi

RA, manji na wenzake wanamatatizo siku nyingi mbona huyo Lipumba hajawahi kumuhimiza JK awachukulie hatua, DR Slaa amekuwa akilia peke yake utasema yeye ndio yuko kwenye chama cha upinzani peke yake

Lipumba amesema huo ugomvi hauna tija kwa taifa, halafu baadae akasema RA amesema mambo ya maana juu ya NBC kuhusu mengi. Mengi alivoongea juu RA, manji et al LIPUMBA AKAMWAMBIA MENGI ANASABABISHA UBAGUZI NA ANAJIPENDEKEZA KWA RAIS WALA HAKUMWOMBA RAIS AYASHUHULIKIE YALE ALIYOSEMA MENGI, LAKINI RA ALIVYOONGEA YA MIKOPO YEYE AMEYAONA YA MAANA, JE KWA NINI?????????
LIPUMBA NI KAMA VILE SOFIA SIMBA ALIVYOMUAMBIA MENGI KACHEMSHA NA RA ALIVYOONGEA AMEKUA BUBU, "BUBU AMBAYE ATAKI KUSEMA" ANGALAU WA JF ANASEMA

Samahani wakuu, nimeona walau niyaongezee fonti ili wale wasio ona tatizo la Lipumba, labda wana matatizo ya macho kama mimi!

Mkuu Semilong ubarikiwe sana
 
kutoka mwananchi

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba amesema malumbano ya wafanyabiashara yanayoendelea kushika kasi nchini kuhusiana na ufisadi, hayana tija kwa taifa badala yake yanalitoa katika harakati zake ya kukabiliana na changamoto za maendeleo.

Profesa Lipumba alisema hayo jana katika mahojiano na gazeti hili kuhusiana na kauli ya mfanyabiashara maarufu nchini, Rostam Aziz aliyemtuhumu Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi kuwa ni ‘nyangumi wa ufisadi’.

Alisema malumbano hayo yanawafanya Watanzania wengi kuacha kujadili mambo muhimu ya kimaendeleo na kubaki kwenye fitina zinazosambazwa na wafanyabiashara hao.

Aliitaka serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukomesha tabia ya wafanyabiashara kukamiana kupitia vyombo vya habari, kwa lengo la kuwashirikisha wananchi kwenye chuki zao ambazo zinaotesha mbegu za rangi na ukabila, hivyo kutishia amani ya nchi.

“Tanzania ni nchi maskini ingawa tuna rasilimali nyingi. Tumekuwa na tatizo kubwa la kushindwa kujipanga vizuri katika kuzitumia. Kwa jinsi suala hili la ufisadi linavyokwenda, linazidi kutuvuruga,” alisema Lipumba na kufafanua: “Mijadala (malumbano) hii inazidi kututoa kwenye mstari.”

Hata hivyo, alisema katika maelezo ya Rostam, ambaye pia ni Mbunge wa Igunga, kuna hoja nzito alizozitoa na ambazo zimewafumbua macho Watanzania, hivyo Rais Kikwete hana budi kuzishughulikia kikamilifu.

Alitaja miongoni mambo hayo kuwa ni tuhuma kuwa Mengi alikopa mabilioni Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kabla haijabinafsishwa na hakurejesha na vile vile alichukua mabilioni mengine kwenye mfuko unaochangiwa na wahisani; Kuagiza Bidhaa kutoka Nje (CIS) ambazo pia hakuzirudisha serikalini kama ilivyo utaratibu wa mfuko huo.

Aliitaka Wizara ya Fedha na Uchumi kuutangazia umma wote waliokopa NBC na CIS na kuwaamuru walipe na kwamba, wachukuliwe hatua kama ilivyokuwa kwa mafisadi wengine waliochota mabilioni ya fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Profesa Lipumba, alisema kama nyaraka zinazohusu fedha za CIS zitakosekana Hazina, serikali iwasiliane na nchi wahisani wa mfuko huo, kwa sababu wana kumbukumbu za kampuni zote zilizokopa.

Alimtaka Rais Kikwete kuonyesha dhahiri nia yake ya kupambana na ufisadi kwa kutowaonea huruma wafanyabiashara wote wawili ambao kila mmoja anaonekana yuko karibu naye (rais).

Profesa Lipumba alisema anamtambua Rostam kuwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mengi ni mwanachama wa CCM ambaye amekuwa akijinadi kuwa anamsaidia Rais Kikwete kwenye vita dhidi ya mafisadi; hivyo akasisitiza wote wako karibu na Rais Kikwete.

Alisema fedha za Mfuko wa CIS hutolewa na wahisani ili kuwasaidia wafanyabiashara kuagiza bidhaa nje na hutakiwa kurejeshwa serikalini kwa shughuli nyingine za maendeleo, hivyo kama hazikurudishwa, huo utakuwa ni wizi wa mali ya Watanzania.

Kuhusu EPA, Profesa Lipumba aliendelea kusisitiza kuwa ripoti ya awali ya ukaguzi ilionyesha kampuni ya Kagoda ilighushi nyaraka ili kuzichota hizo fedha, hivyo haoni sababu ya serikali kutowapeleka mahakamani wahusika au wamiliki wake ambao mpaka sasa wanafichwa.



lipumba unataka kikwete amshughulikie mengi je marafiki zako RA, manji(nssf). tanil, jetu et al vipi.

Mengi ameshamaliza hizo kesi zote mahakamani!

Kweli RA payroll yake ni kubwa mpaka Lipumba....!

Yaleyale ya Kipofu na Jogoo! Wacha kujifanya kipofu. Hebu soma para ya mwisho ya maelezo uliyotuletea, kwani si mnasema Kagoda ni Rostam? Akili zenu ziwe macho kuliko ushabiki!!!!!!!
 
kela72,

..mara ya mwisho nilisikia Prof ameoa mwanamke toka lile kabila linalochukiwa kabisa hapa jamii forums.

..pia mwanamke huyo ni alikuwa muumini wa dini inayochukiwa na chama cha CUF.
Joka Kuu ktk Pumba ulizozitoa ni hizi...kama upenzi wako wa Chadema ili CUF ionekane inawachukia wakristo endelea....huku ni kufilisika kifikra....

Labda utueleze kwanini CUF inawachukia Wakristo na nani kakuhabarisha hizo habari...au Mkutano gani wa ndani au wa Nje wa CUF..ulizungumza hayo....kinyume chake tunaomba ufute KAULI yako mara moja!!!
 
Nimesoma post huku nimebana pumzi, siamini Lipumba kama anakuja na mashambulizi namna hii dhidi ya mtu aliyejitoa mhanga kuwataja mafilisi wa nchi hii!

Sasa naanza kuamini kuwa Lipumba si tu kwamba yupo ktk payroll ya mafilisi bali pia zile kelele zake alizokuwa anapiga dhidi ya mafisadi ni kwamba alijua hakuna hatua zitakazochukuliwa dhidi yao na alikuwa tu anatimiza wajibu ili kupata reputation ya kisiasa. Wanasiasa bwana ni kama upepo vile.

Anyway sasa naamini kuwa CUF si chama makini kama alivyosema Prof. Safari na wanajua wanachokifanya, they just stir in order to survive and who knows, may be wanasiasa wa kulipwa.


Tatizo lenu kuwa hamko tayari kupokea ukweli na msipokuwa tayari kuwa wakweli hamna hoja moja mtakayoijibu kwa hoja bali shutuma tu.
Binafsi nashangaa na majigambo ya wengine humu na kumbe ni zobazoba.
 
Yaleyale ya Kipofu na Jogoo! Wacha kujifanya kipofu. Hebu soma para ya mwisho ya maelezo uliyotuletea, kwani si mnasema Kagoda ni Rostam? Akili zenu ziwe macho kuliko ushabiki!!!!!!!

Vita ya ufisadi inarudishwa nyuma na watanzania wenyewe...Yani ni crabs in a bucket pulling each other down.
Mbona hamjibu kuwa RA alienda benki kwa niaba ya Kagoda kama nani? Position yake ilikuwa ipi kwenye hizo kampuni feki alizoziwakilsha wakati wa kuchota pesa?
Nyie watanzania wenye njaa kali mmeshaliuza Taifa na mtakiona cha mtema kuni. Mnadhai ni watanzania wote wenye mawazo ya kitumwa? Mnafananisha issue ya mikopo na wizi? Wapi na wapi? Mnaugeuza mjadala kama mko kwenye payroll,rahisi sana kutype upuuzi na wakati Taifa liko njia panda.
 
Msiumize vichwa sana, kama alivyofanya nyakati za DOWANS ndivyo anavyofanya nyakati hizi.

Inabidi hawa wanasiasa uchwara na wapenda hela bila kuangalia maslahi ya taifa wawe wanaangalia timing. Si kila jambo kubwa utie domo ili kutafuta umaarufu, tumeni makanjanja wenu waboronge tutaacha lakini kwa mwendo huu nazidi kumwona Lipumba kilaza tu, anajaribu kutafuta jinsi ya kusikika upya.

Nonesense!!!!!!!!!!!!!!!!!

Ukweli utabaki ukweli mbele ya unazi na alichosema Lipumba ni sahihi. Anaetuhumiwa haki yake ni kujitetea au kuchunguzwa na kinachofuata ni kusafishwa au kuhukumiwa iwapo ana hatia. Kwani alichosema Lipumba ni kipi? kuwa Mengi achunguzwe na shituma? Nini wasiwasi wenu ikiwa yu msafi? Alichosema wa Kagoda wapelekwe mahakamani na kila mmoja hapa tunajidai kuwa Kagoda ni Rostam sasa kaenda wrong wapi Lipumba.
Tatizo lenu mkishasoma heading na kuona kua "shujaa, mwenzetu" katajwa basi hamna wakati wa kusoma au kusikia nini kinasemwa, Mwe! ivyo ndivyo tulivyo humu, KAAAZI Pevu.
 
mbona hakumtaja na slaa ashughulikiwe? kwa kuwa naye aliwataja tena kwa mapana na kina kama alivyowataja Mengi.
mkuu nomba ku-differ hapo

AS far as this debate concern bado tuko kwa Mengi na Rostam. Slaa si mpumbavu kama Mengi, Slaa ana data na bado ni msafi hatujapata maovu yake na KAMA yatatolewa naye ataandamwa.
 
Ndio hivyo hakuna tija kwa Taifa ,kwa sababu mazoea tuliyonayo yanaonyesha hivyo ,kuwa tunakwamishwa kwenye mambo na hakuna hata moja linalokuwa zaidi ya ahadi hewa, hivi chukulia mmoja anaonekana na hatia .anafungwa na mwengine anaendela anatanua mitaani na zaidi atakuwa anajigamba. Sisi walala hoi tutakuwa tumefaidika vipi?
Hata mimi naona hakuna faida hapa ,si kwa hawa bali kwa mafisadi wote ,kwa kweli hakuna faida hata moja au mnataka kutueleza kuwa faida ni ile ya kujiuzulu ,hadi hii leo sijaona faida ya watu wale kujiuzulu ,atokee mtu hapa atueleze faida iliyopatikana kwa WaTanzania kuhusiana na kujiuzulu kwa akina Lowasa na wenzake ,tupeni faida tuone hata hili la leo likawa kubwa ,aidha ninawahesabu wale wote wanaoshangilia hili wamo ndani ya kambi za watu hawa ni si wapinzani wanaoitakia mema Tanzania kwa ujumla,tatizo si watu hawa ,ninapenda mulielewe hilo ,Tatizo kubwa nilionalo ni mtawala Sultani CCM na wafuasi wake ,sasa kukaa chini ya miti na kumjadili Mengi na Rostamu ni kutupotezea muda wa kupambana na Sultani CCM ,maana wote hao ni watu wenye kambi zao humo ndani ya CCM ,sasa wewe mpinzani unajumuika vipi na kumtetea mmoja wao ?
 
Inaonyesha kuwa Lipumba ameanza kuonekana tishio kwani dili zake ni kupambana na mtawala CCM pamoja na kuwachanganya wafuasi wake ,kitu kinachoonyesha kuwa kinasababisha maumivu makali kwa wengine ambao wamekuwa wakionekana kujipendekeza kwenye kambi za CCM.
 
as far as this debate concern bado tuko kwa mengi na rostam. Slaa si mpumbavu kama mengi, slaa ana data na bado ni msafi hatujapata maovu yake na kama yatatolewa naye ataandamwa.

WEWE NDIO MPUMBAVU NA SIO MENGI

kuna mtz gani binafsi anyepambana na ccm ambaye si mwana siasa
leo hii wewe unamuona mengi mpumbavu, mengi akiamua kukaa kimya kutaka ippmedia iimbe ccm, inchi itakuwa wapi?
Mengi ameweka biashara yake hatiani kwa ajili ya wa tz, mengi got so much to loose than any tanzanian in this saga....
Mengi akitaka ccm wanampa mafao na anakaa kimya na magazeti yake hayaandiki habari yeyote ya ufisadi, kaa chini ufikirie kidogo...
He is putting his personal wealth at risk because of you people..
 
kela72,

..mara ya mwisho nilisikia Prof ameoa mwanamke toka lile kabila linalochukiwa kabisa hapa jamii forums.

..pia mwanamke huyo ni alikuwa muumini wa dini inayochukiwa na chama cha CUF.


Wadini na Wakabila ni sawa na.................... hata wakitiwa ndani ya chupa watatoa japo vidole. Vyereje dini na kabila iwe issue kwa hili. Poleni nyie kumbe mna watu fulani mnaowachukia kutokana na kabila zao na dini? Shame on you all whoever mwenye tabia hiyo humu.
 
Wadini na Wakabila ni sawa na.................... hata wakitiwa ndani ya chupa watatoa japo vidole. Vyereje dini na kabila iwe issue kwa hili. Poleni nyie kumbe mna watu fulani mnaowachukia kutokana na kabila zao na dini? Shame on you all whoever mwenye tabia hiyo humu.

bwa ha ha hahah ha ha haa
 
Huyu Lipumba naye yumo mifukoni mwa mapapa mafisadi akitafuna mapesa yao taratibu. Ama kweli viongozi wetu wa nchi yetu ni mandumila kuwili wa hali ya juu na pia ni viongozi uchwara.

Kwa wewe juu ya Mengi sistaajabu chochote kwani kufika hata kumtetea kwa uzinifu bila shaka mko kundi moja na Lipumba isipokuwa pande tofauti.
 
wewe ndio hauchambui mada vizuri, lazima ujue lipumba alisema nini mara ya kwanza juu ya mengi

RA, manji na wenzake wanamatatizo siku nyingi mbona huyo Lipumba hajawahi kumuhimiza JK awachukulie hatua, DR Slaa amekuwa akilia peke yake utasema yeye ndio yuko kwenye chama cha upinzani peke yake

Lipumba amesema huo ugomvi hauna tija kwa taifa, alafu baadae akasema RA amesema mambo ya maana juu ya NBC kuhusu mengi. Mengi alivoongea juu RA, manji et al LIPUMBA AKAMWAMBIA MENGI ANASABABISHA UBAGUZI NA ANAJIPENDEKEZA KWA RAIS WALA AKUMWOMBA RAIS AYASHUHULIKIE YALE ALIYOSEMA MENGI, LAKINI RA ALIVYOONGEA YA MIKOPO YEYE AMEYAONA YA MAANA, JE KWA NINI?????????
LIPUMBA NI KAMA VILE SOFIA SIMBA ALIVYOMUAMBIA MENGI KACHEMSHA NA RA ALIVYOONGEA AMEKUA BUBU, "BUBU AMBAYE ATAKI KUSEMA" ANGALAU WA JF ANASEMA


Kama wakati ni issue mbona huyo Mengi alinyamaza muda wote huo? Naona kama tutakaa na kujiuliza kwanini sasa na kuogopa kusema basi hiyo kwanini sasa itazidi kuwa ya kipindi kikubwa.
Jiulize pia kwanini sasa ndio Rostam kaamuwa kulipa mapigo na jiulize kwa nini tunajadili hili la Lipumba? Jawabu ya yote ni mlolongo wa matukio. Ukisoma alichoeleza Lipumba anazungumzia mapambano ya Wafanyabiashara na hatima ya Taifa, jee unaweza kuniambia hili limetokea wakati gani hata Lipumba alisemee huo wakati muafaka unaotaka. Wacheni UNAZI Mengi ana tuhuma ya kujibu kama tulivyomtaka Rostam afanye kipindi kirefu.
 

WEWE NDIO MPUMBAVU NA SIO MENGI

kuna mtz gani binafsi anyepambana na ccm ambaye si mwana siasa
leo hii wewe unamuona mengi mpumbavu, mengi akiamua kukaa kimya kutaka ippmedia iimbe ccm, inchi itakuwa wapi?
Mengi ameweka biashara yake hatiani kwa ajili ya wa tz, mengi got so much to loose than any tanzanian in this saga....
Mengi akitaka ccm wanampa mafao na anakaa kimya na magazeti yake hayaandiki habari yeyote ya ufisadi, kaa chini ufikirie kidogo...
He is putting his personal wealth at risk because of you people..

MENGI NI MPUMBAVU KAMA ULIVYO WEWE< SEMILONGO

Hivyo Mengi alikwambia wapi kuwa anapambana na CCM? Umeisahau kauli yake kuwa anamsaidia JK? Nimeamini sasa ujinga wako upo wapi.Upo katika kusahau haraka hata kile SHUJAA wako anakisema.
Ama kwa ujinga wa Mengi upo kwa vile hana msimamo. Hebu niambie Mengi anasaidia CCM au anamsaidia nani hasa iwapo anatowa misaada kwa mgongo wa CCM na kufuatana na viongozi wa CCM wakati hao viongozi wa CCM wanapanga kummaliza kwa mujibu wa taarifa zenu humu humu. Ondowa Jazba na uwe na hoja tafadhali.
 
Lipumba si Mnyamwezi? Chuma usimtetee. Hajaanza leo wala jana.

Alikuwa mshauri wa Mwinyi wa Uchumi. Matokeo yake mnayakumbuka.

Ha haaaaaaaaaaaaaaaa umenifurahisha sana hapa. Kweli jamaa darasani pale mlimani alikuwa kichwa lakini applicability ya taaluma yake ?????????
 
MENGI NI MPUMBAVU KAMA ULIVYO WEWE< SEMILONGO

Hivyo Mengi alikwambia wapi kuwa anapambana na CCM? Umeisahau kauli yake kuwa anamsaidia JK? Nimeamini sasa ujinga wako upo wapi.Upo katika kusahau haraka hata kile SHUJAA wako anakisema.
Ama kwa ujinga wa Mengi upo kwa vile hana msimamo. Hebu niambie Mengi anasaidia CCM au anamsaidia nani hasa iwapo anatowa misaada kwa mgongo wa CCM na kufuatana na viongozi wa CCM wakati hao viongozi wa CCM wanapanga kummaliza kwa mujibu wa taarifa zenu humu humu. Ondowa Jazba na uwe na hoja tafadhali.

Wewe nawe, khaaa!!!!! Mengi alikuchukulia kimwana nini?
 
Katika Uchunguzi wangu wa Kina , nimegundua kuwa Tatizo sio Vodacom Hapa, Tatizo ni UKABILA NA UKANDA ndio unatusumbua kwasasa.

Wachaga walikuwa very influencial katika siasa za Tanzania, but they lost that stutus as the time was passing on. Ukiangalia utawala wa Mkapa uliwanufaisha sana wachaga. which has lost in kikwete leadership.On other hand kwa Kuangalia political Map Rostam Aziz ni influencial kwasabu alikuwa na good ties with the lake zone which politically always is a very big decider of Tanzania politics.

Ndio maana ukianza kutaja majina yote ya watu ambao wako associated na Rostam AZiz na vodacom wote wanatoka kanda ya ziwa., mpaka unakuta hata Lipumba hawezi kuongea against RA

Rostamu aziz ni mnyamwezi, ukiangalia Tabora, Mwanza na shinyanga mpaka msoma ukweli ni kwamba kuna waarabu wengi sana ambao ni wafanyabiashara maarufu katika maeneo yao and they have helped those communities for many years.

Why Rostam Aziz anakiburi? Rostam Has legitimate business for so long and if you look back at Mirambo Holdings is one of very reputable investment company in tanzania for so long. Kilichoenda kombo ni kwamba Rostam alikuwa ni njia tu ya kujusitify uchotaji wa fedha za CCM ,

why KIKWETE YUKO KIMYA,?

Since he druged RA in this shit hawezi kumsaliti, COST ya yeye kumsaliti is equal to the lose of political map. RA anafahamika Mwanza, Shinyanga, Tabora na msoma and he is very influencial there, calculation ni kura za NEC Mzee, na kanda ya ziwa ndio imempa JK ushindi.

MENGI

Tatizo la mengi ni kwamba he have been a big fish for so long , akiangalia mwelekeo wa biashara na political influence ilivyopotea kwa wachaga anaogopa.But he has legitimate claims panapo haribika ni kwamba waarabu wengi wenye ugomvi na mengi ni kutoka kanda ya ziwa, wanajiita wasukuma. so mengi he is in bettle to retain his powership/chaga but at the same time anasidia kupambana na ufisadi

mwisho tulipofika sasa.

JK Anaangalia his political future.
Wasukuma wameshikiria justice depertment
wasukuma,wanyamwezi hawawezi kumwachia RA afe maji
JK hawezi kuwatosa wasukuma
wachaga they see it is the time for them to gain their political influence
wasukuma wanawafunga mafisadi wachaga
 
Back
Top Bottom