Prof. Lipumba arejea nchini

Prof. Lipumba arejea nchini

Kwa Bahati nzuri CCM hawatakuwa madarakani baada ya mwezi wa 10 kwa hiyo ataishia kuukodolea uwaziri mkuu kwa macho.
 
alishiriki kumkaribisha,anashriki kumponda,kweli amevuta mpunga,aende zake ccm
 
Mtu huwa anatumia hakiri zake kuji chagulia maisha anayo taka kuishi lipumba si mtu wa kubuluzwa na slaa si mtu wa kubuluzwa na ndio mana hawako tiali kua ukawa
 
Yampasa ajitafakari kisha achukue tahadhari, kama ndo kaenda huko ssm ajue hata udiwani hapati labda ubunge viti maalumu atapata...!!!
 
Lipumba kula hizo bilions kisha uwapige chini urudie tena CUF. Faked by Lipumba. Umefurahishwa na pole ya ngeo za mbagala
 
....pesa limeshaweka nje sasa limerudi na mipumba...tusubiri mipovu.....aibu sana hili prof la maji taka....
 
Pamoja na kutwangwa kote kule na vyombo vya dola vinavyoongozwa na maccm bado kasahau?.kweli ela ni mwana haramu .na huyu kweli mambo anayoyafanya ni pumba kama jina lake.
 
Jamani mwacheni nae apumzike ataongea muda ukiwadia nafikiri wakati wa kampeni
 
washabikia siasa na fikira zao .... ni sheeeeda kweli kweli!!! Ishinde CCM au UKAWA hakuna kitakachobadilika, kipondo cha ukali wa maisha pale pale, kipondo cha polisi pale pale solution kila mshabikia siasa badala ya kutoa povu kumshabikia mwanasiasa as if ni baba yako mzazi haitakutoa hapo ulipo, jitafakari na ujipe jibu "ni mipango gani ya maisha ulijipangia na umefanikiwa kiasi gani?" kinyume cha hapo jiesabu wewe ni mburula unatumika kama mtaji wa wanasiasa na familia zao.

Heko Lipumba kama kweli ulivuta bingo ili uachane na ndoa ya ukawa. Nani mwenye mkataba na Mwenyezi Mungu kwamba ataishi hapa mile mile? Prof kapata fursa, ameitumia - Big UP!!
 
Mwache ayashuhudie mafanikio makubwa ya UKAWA lakini hatafaidi matunda yake.
 
Mbona alichagua wakati usio muafaka kufanya utafiti wa maendeleo ya Rwanda. Wakati shughuli za uchaguzi hapa kwetu ni apevu yeye anaelekeza nguvu zake kufanya utafiti wa jinsi Rwanda walivyofanikiwa kiuchumi? Very odd! Wagombea wanachujwa na NEC wanatoa fomu za kugombea yeye anafanya utafiti wa mambo ya rushwa Rwanda? Very awkward! Huo utafiti wake atauendeshea wapi wakati anajiondoa katika siasa za TZ? There is something fishy!!!
 
Ukiisoma historia ya Ulutheri utakuta kuwa neno kujikomboa na mageuzi kutoka Vatikan lilitumika sana kuonesha kama vile wanadhalilishwa na Kanisa Katoliki lakini ilikuwa ni uchu tu wa madaraka.

Hilo neno halitumiki kwa bahati mbaya ni mfumo kamili na wanaelewa kwanini wanalitumia.

Chama kikubwa na wafadhili wakubwa wa chadomo ni cha Kidemokrasia cha Ujerumani CDU (Walutheri).

Lowassa? Kaskazini?

Jiulize, Slaa yuko wapi? Na kwanini?

muulize mzee Khamisi Mgeja
 
Asema haungi mkono UKAWA.
attachment.php


Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Rwanda jana. Picha na Said Khamis

Kwa ufupi

Asisitiza kutokubaliana na uamuzi wa Ukawa kumsimamisha Lowassa kugombea urais.

By Goodluck Eliona, MwananchiDar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba alirejea nchini jana jioni akitokea Kigali, Rwanda alikokwenda mara tu baada ya kujiuzulu wadhifa huo siku nane zilizopita.

Profesa Lipumba aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) saa 10.10 jioni kwa ndege ya Rwanda Air.

Akihojiwa na Azam Tv kwa simu akiwa Kigali, siku tatu baada ya kuondoka nchini, Profesa Lipumba alisema alikuwa nchini humo akifanya utafiti kuona namna gani Tanzania inaweza kujifunza mambo ya kiuchumi kutokana na nchi hiyo kupiga hatua kubwa katika sekta hiyo.

Alipoulizwa jana, Profesa Lipumba alisema akiwa huko alikuwa na mazungumzo na Bodi ya Maendeleo ya Rwanda (RDB), wadau wa masuala ya rushwa, waziri wa fedha wa nchi hiyo na makamu mwenyekiti wa Bodi ya Utawala.

“Wenzetu wamepiga hatua kubwa katika kukuza uchumi ndani ya kipindi kifupi, hivyo safari yangu ilikuwa ya kujifunza mbinu walizotumia kufikia malengo yao,” alisema.

Akizungumzia hatima yake kisiasa, licha ya kusema ataendelea kuwa mwanachama wa CUF, alisema hatashiriki kufanya kampeni kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kuwa umoja huo umemsimamisha mwanachana wa CCM, Edward Lowassa.

“Kisiasa hatima yangu ni kama ya Mtanzania mwingine yeyote, Ukawa tuna mgombea kutoka CCM, amehama juzi tu, pia mle ndani ya Bunge la Katiba hakuunga mkongo Rasimu ya Katiba na ndiyo maana nikasema dhamira yangu inanisuta,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema wanachama wa CUF hawana sababu ya kuona kama amewaacha kwa kuwa bado yupo nchini.

Awali, akitangaza kujiuzulu, nguli huyo wa uchumi, alisema alifikia uamuzi huo kutokana na Ukawa kumkaribisha Lowassa kugombea urais kupitia umoja huo, hivyo dhamira yake inamsuta.


Chanzo;
Mwananchi


Msaka tonge
 
Asema haungi mkono UKAWA.
attachment.php


Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Rwanda jana. Picha na Said Khamis

Kwa ufupi

Asisitiza kutokubaliana na uamuzi wa Ukawa kumsimamisha Lowassa kugombea urais.

By Goodluck Eliona, MwananchiDar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba alirejea nchini jana jioni akitokea Kigali, Rwanda alikokwenda mara tu baada ya kujiuzulu wadhifa huo siku nane zilizopita.

Profesa Lipumba aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) saa 10.10 jioni kwa ndege ya Rwanda Air.

Akihojiwa na Azam Tv kwa simu akiwa Kigali, siku tatu baada ya kuondoka nchini, Profesa Lipumba alisema alikuwa nchini humo akifanya utafiti kuona namna gani Tanzania inaweza kujifunza mambo ya kiuchumi kutokana na nchi hiyo kupiga hatua kubwa katika sekta hiyo.

Alipoulizwa jana, Profesa Lipumba alisema akiwa huko alikuwa na mazungumzo na Bodi ya Maendeleo ya Rwanda (RDB), wadau wa masuala ya rushwa, waziri wa fedha wa nchi hiyo na makamu mwenyekiti wa Bodi ya Utawala.

“Wenzetu wamepiga hatua kubwa katika kukuza uchumi ndani ya kipindi kifupi, hivyo safari yangu ilikuwa ya kujifunza mbinu walizotumia kufikia malengo yao,” alisema.

Akizungumzia hatima yake kisiasa, licha ya kusema ataendelea kuwa mwanachama wa CUF, alisema hatashiriki kufanya kampeni kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kuwa umoja huo umemsimamisha mwanachana wa CCM, Edward Lowassa.

“Kisiasa hatima yangu ni kama ya Mtanzania mwingine yeyote, Ukawa tuna mgombea kutoka CCM, amehama juzi tu, pia mle ndani ya Bunge la Katiba hakuunga mkongo Rasimu ya Katiba na ndiyo maana nikasema dhamira yangu inanisuta,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema wanachama wa CUF hawana sababu ya kuona kama amewaacha kwa kuwa bado yupo nchini.

Awali, akitangaza kujiuzulu, nguli huyo wa uchumi, alisema alifikia uamuzi huo kutokana na Ukawa kumkaribisha Lowassa kugombea urais kupitia umoja huo, hivyo dhamira yake inamsuta.


Chanzo;
Mwananchi


Nae mwandishi ni kanjanja tu yaani hakuweza hata kumhoji mbona vikao vyote vya kumkaribisha na kumteua vilivyoendeshwa na ukawa alishiriki iweje leo atoe sababu hizo?Hivi si upo ushahidi jukwaani humu kuwa hata kabla ya kujiunga chadema Lipumba alishamfuata Lowassa ofisini kwake kumshawishi kujiunga chadema? Upo ushahidi pia jamvini humu kuwa ukumbi aliotumia Lipumba kuachia kwake ngazi cuf ulilipiwa siku moja kabla na tiss. Hivyo hivyo upo uzi unaozungumzia Lipumba kuwepo ofisi za ccm Lumumba usiku wa J'mosi na J'pili kabla ya kwenda kutoa tamko lake kwa waandishi wa habari.
 
Hapa tulipo Fika Kweli twahitaji Mabadiliko na tunapo gundua mtu au kikundi kina tuangusha Inatuhuma sana sana. Tulipo fika hakuna Mtz anaye hitaji Elimu kubwa kujua twahitaji mabadiliko Yeye azunguke na kujifurahisha tu sisi mbele kwa mbele
 
Back
Top Bottom