Prof. Kitila Mkumbo, muogope Mungu!

Prof. Kitila Mkumbo, muogope Mungu!

Hili swali ni ushahidi mwingine huyu mh.kwenye hii makala alikuwa na agenda yake.

Honestly tungetarajia aanze kutoa kibanzi kwenye jicho lake then ndipo aweze kutoa boriti kwa wenzake. Atueleze was it logical kusimamisha mgombea urais na kuishia kupata kura walizopata? Was it logical kusimamisha wabunge nchi nzima na kuambulia only one? Yaani Wameshindwa kupata hata kiti kimoja cha viti maalumu? Why wasingewekeza all their energy kwenye baadhi ya majimbo ili angalau wapate viti vitano? Huyu prof ana maswali mengi ya kutolea unafafanuzi. Sasa ni maajabu kuanza kujadili ubovu wa gari la jirani yako wakati la kwako liko juu ya mawe.
 
Na kama watu wa vijijini waliuona mkutano wa Lowassa Arusha akiwa CCM kupitia televisheni, iweje hawakuona mikutano mingine ya Lowassa akiwa UKAWA? Hakuwafikia watu wa vijijini kivipi sasa kama hawa watu waliweza kuuona mkutano wa Arusha? Mgombea aliyeshinda alifika vijijini? Lini? "The problem with Africa is that too many intellectuals have become political sycophants just to go ahead" Prof. K. K. Mwenda
 
Na kama watu wa vijijini waliuona mkutano wa Lowassa Arusha akiwa CCM kupitia televisheni, iweje hawakuona mikutano mingine ya Lowassa akiwa UKAWA? Hakuwafikia watu wa vijijini kivipi sasa kama hawa watu waliweza kuuona mkutano wa Arusha? Mgombea aliyeshinda alifika vijijini? Lini? "The problem with Africa is that too many intellectuals have become political sycophants just to go ahead" Prof. K. K. Mwenda

Maswali mazuri sana haya

CC: Kitila Mkumbo
 
Last edited by a moderator:
aibu... hiki kiprofesa si kingetafuta mtu amsaidie kuhariri andiko lake?
 
Maswali mazuri sana haya

CC: Kitila Mkumbo

Hizi sababu anazotoa Kitila zinaakisi zile zilizotolewa na January kwenye makala yake katika gazeti/jarida la Mail&Guardian Africa. Makala ile ilitoka siku chache kabla ya uchaguzi. Anachofanya Kitila ni ku regurgitate alichoandika January. I suspect some sort of coordination here.
 
Last edited by a moderator:
Katika Makala aliyoiandika katika gazeti la Raia Mwema la leo tarehe 4/11/2015 yenye kichwa cha habari, "Jinsi wapiga kura wa vijijini walivyomwibia Lowassa" , Prof.Mkumbo anajaribu kuelezea sababu za Lowassa na CHADEMA kwa ujumla kushindwa katika kinyang'anyiro cha uraisi.

Hapa nitatoa summary tu ya kile alichoandika.

Prof.ameeleza mambo kadhaa yaliyochangia Lowassa kushindwa katika uchaguzi huu ikiwa ni pamoja na kupuuza tafiti alizoziita za kisayansi za Twaweza na IPSOS.

Prof.anasema kutokana na tafiti hizi kuonyesha kwamba Dr.Magufuli alikuwa anaungwa mkono zaidi na makundi manne makuu: vijijini,wanawake,wenye umri mkubwa na ambao hawajasoma sana.

Prof.katika makala yake anaendelea kusema kwamba,baada ya matokea hayo,alitarajia Ukawa na mgombea wao wangewekeza nguvu zaidi vijijini kuyalenga hayo makundu lakini wao waliendelea kuwekeza zaidi mijini.

Kwa maoni yake Prof.anasema, Lowassa amekosa kura za wapiga kura wa vijijini kwasababu kuu mbili.Mosi,ni wafuasi wa Lowassa kukataa kuyaona na kurekebisha makosa ya msingi katika kampeni zao.

Kwa mfano,Lowassa akifungua kampeni za kuomba kuteuliwa na CCM mjini Arusha alimwagia sifa lukuki Raisi Kikwete katika mkutano huo ambao ulionekana mpaka vijijini kupitia Television na baadae alipojiuinga Ukawa akageuka na kuponda utawala wa CCM na Kikwete kwamba ameua uchumi wa Taifa.

Pili,ni viongozi wa CHADEMA kubeba agenda ya ufisadi na kuja kumsimamisha Lowassa kuwa mgombea wao.

Prof.anasema,wapiga kura wa mjini waliokuwa wanataka mabadiliko hawakuona mkanganyiko wowote katika kauli za Lowassa.Lakini wapiga kura wa vijijini wana utaratibu wa kutunza kumbukumbu na kuzitumia wakati muafaka.

Prof. pia anasema wapiga kura wa vijijini, tofauti na wa mjini, waliona swala la viongozi wa CHADEMA kumsimamisha Lowassa ni ukigeugeu wa karne na kuuzingatia uamuzi wao wa Oktoba 25.

Prof.katika Makala yake hiyo,anaendelea kuwasifu watu wa vijijini kuwa eti ni wagumu kubadilika kirahisi kwa kudanganywanywa na ndio sababu hawakumpigia kura Lowassa.

Prof.ananishangaza zaidi pale anapoandika katika Makala yake hiyo kuwa,"wakati watu wa mijini waliamini mabadiliko na kuitoa CCM madarakani,wananchi wa vijijini walionekana kuzingatia zaidi sera na umakini wa wagombea katika kupiga kura".

Maswali yangu kwa Prof. na kwanini nasema amuogope mungu ni haya.

1.Prof. ni kweli una amini wananchi wa vijijini wanazingatia zaidi sera katika kupiga kura na kuchagua viongozi kuliko wananchi wa mijini?

2.Prof.kama kweli watu wa vijijini wanazingatia sera,je, kati ya CCM na vyama vya upinzani(Ukawa) ni chama kipi kilikuwa na sera rafiki zaidi kwa watu wa vijijini?

Je,ni yule aliehubiri elimu bure mpaka chuo kikuu au yule aliehubiri elimu bure mpaka kidato cha nne?

3.Prof.sera ya elimu bure ya mwaka 2010 ya CHADEMA ilikuwa rafiki zaidi kwa mwananchi wa kijijini au mjini?Na je kati ya Dr.Slaa na Kikwete ni nani alipata kura nyingi za vijijini?

4.Prof.kama watu wa vijijini ufisadi kwao ni issue,mwaka 2010 ni nani kati ya Dr.Slaa na Kikwete aliepata kura nyingi kutoka kwa watu wa vijinini?

4.Prof.unataka kuniambia kama Lowassa angepitishwa na CCM katika uchaguzi wa mwaka huu, watu wa vijijini wasingempaka kura kwasababu ya tuhuma za ufisadi zinazomkabili na badala yake wapiga kura wengi wa vijijini wangempigia kura mgombea wa UKAWA?

Prof. are you seriuos abaout this article?

I wonder!!
Nafikiri wewe ndie unatakiwa kumuogopa Mungu sijui nyie watu mna matatizo gani mnataka kusikia mazuri tu au kusifiwa tu,ningekuelewa kama ungejibu hoja badala ya kuja na sentensi ya kusema Kitila amuogope Mungu kwa kosa gani au kwa uongo upi ,jirekebisheni,na mkubali pia mawazo kutokaupande mwingine
 
Yuko sahihi ndo masna wa 'vijinini' ndio waliomchagua Magufuli kwa wingi kwa kutumia hivyo vigezo vya Prof. Hapo juu!
 
mkiambiwa ukweli mnatoa kashfa TWAWEZA na wengineo kwenye kura za maoni walisema ukweli mkawapa kashfa matokeo yake mkapata wabunge 35 halafu unadai umeibiwa kura.

wataalamu wakiwashauri fuateni ushauri wao mkoa wa Ruvuma una majimbo 9 mgombea wenu alienda majimbo 2 ya mjini mkoa wenye majimbo 9 unaenda majimbo 2 halafu unategemea kupata kura za watu wa vijijini kweli watu wa vijijini walimwibia kura Lowassa.
 
Prof.you must be kidding!

Hilo prof. ni moja la maprof wapumbavu wa Tanzania. Sioni ajabu majitu kama Mkumbo (prof. makombo), Banna na maprof. wengine wakihororoja maneno yasiyokuwa na tija. Hivi hili tutusa nani kaliambia kwamba Lowassa kashindwa uchaguzi? Useless prof.
 
Nani asiyejua kuwa Prof. Mkumbo anatumika?
 
Tibaijuka ngeleya chenge na kingwangala wameshinda mjini eheh
 
Mleta mada muogope Mungu....yaani wewe ulikuwa mpinga ufisadi ghafla ukageuka na kuanza kumshabikia...acheni unafiki !
 
Huyo profesa zwazwa aandike sababu ya ACT kupata kiti kimoja cha ubunge.
 
Pia tumuulize Profesa amepitia matokeo yote ya uchaguzi ya kura zilizopigwa vijijini na kukuta Magufuli anaongoza?

KwAni mpinzani alikuwa Lowas? tu? ACT hawakushinda popote mjini wala vijijini. Kafulila shujaa Wa taifa juu ya Ufisadi kashindwa kwao vijijini wanakotunza kumbukumbu. Chenge Na Tibaijuka wameshinda vijijini, wananchi hawakumbuki mboga ya million kumi. The Professor can not be serious he has hate speech towards Lowasa
 
Jamani hawa ni wale adhabu ya kupigwa mawe inawafaa ni wanafki kupitiliza !! Prof. Anawafanyia unafiki watanzania zaidi ya mil 40 na kuharibu maisha na matumaini yetu.
 
Back
Top Bottom