Katika Makala aliyoiandika katika gazeti la Raia Mwema la leo tarehe 4/11/2015 yenye kichwa cha habari, "Jinsi wapiga kura wa vijijini walivyomwibia Lowassa" , Prof.Mkumbo anajaribu kuelezea sababu za Lowassa na CHADEMA kwa ujumla kushindwa katika kinyang'anyiro cha uraisi.
Hapa nitatoa summary tu ya kile alichoandika.
Prof.ameeleza mambo kadhaa yaliyochangia Lowassa kushindwa katika uchaguzi huu ikiwa ni pamoja na kupuuza tafiti alizoziita za kisayansi za Twaweza na IPSOS.
Prof.anasema kutokana na tafiti hizi kuonyesha kwamba Dr.Magufuli alikuwa anaungwa mkono zaidi na makundi manne makuu: vijijini,wanawake,wenye umri mkubwa na ambao hawajasoma sana.
Prof.katika makala yake anaendelea kusema kwamba,baada ya matokea hayo,alitarajia Ukawa na mgombea wao wangewekeza nguvu zaidi vijijini kuyalenga hayo makundu lakini wao waliendelea kuwekeza zaidi mijini.
Kwa maoni yake Prof.anasema, Lowassa amekosa kura za wapiga kura wa vijijini kwasababu kuu mbili.Mosi,ni wafuasi wa Lowassa kukataa kuyaona na kurekebisha makosa ya msingi katika kampeni zao.
Kwa mfano,Lowassa akifungua kampeni za kuomba kuteuliwa na CCM mjini Arusha alimwagia sifa lukuki Raisi Kikwete katika mkutano huo ambao ulionekana mpaka vijijini kupitia Television na baadae alipojiuinga Ukawa akageuka na kuponda utawala wa CCM na Kikwete kwamba ameua uchumi wa Taifa.
Pili,ni viongozi wa CHADEMA kubeba agenda ya ufisadi na kuja kumsimamisha Lowassa kuwa mgombea wao.
Prof.anasema,wapiga kura wa mjini waliokuwa wanataka mabadiliko hawakuona mkanganyiko wowote katika kauli za Lowassa.Lakini wapiga kura wa vijijini wana utaratibu wa kutunza kumbukumbu na kuzitumia wakati muafaka.
Prof. pia anasema wapiga kura wa vijijini, tofauti na wa mjini, waliona swala la viongozi wa CHADEMA kumsimamisha Lowassa ni ukigeugeu wa karne na kuuzingatia uamuzi wao wa Oktoba 25.
Prof.katika Makala yake hiyo,anaendelea kuwasifu watu wa vijijini kuwa eti ni wagumu kubadilika kirahisi kwa kudanganywanywa na ndio sababu hawakumpigia kura Lowassa.
Prof.ananishangaza zaidi pale anapoandika katika Makala yake hiyo kuwa,"wakati watu wa mijini waliamini mabadiliko na kuitoa CCM madarakani,wananchi wa vijijini walionekana kuzingatia zaidi sera na umakini wa wagombea katika kupiga kura".
Maswali yangu kwa Prof. na kwanini nasema amuogope mungu ni haya.
1.Prof. ni kweli una amini wananchi wa vijijini wanazingatia zaidi sera katika kupiga kura na kuchagua viongozi kuliko wananchi wa mijini?
2.Prof.kama kweli watu wa vijijini wanazingatia sera,je, kati ya CCM na vyama vya upinzani(Ukawa) ni chama kipi kilikuwa na sera rafiki zaidi kwa watu wa vijijini?
Je,ni yule aliehubiri elimu bure mpaka chuo kikuu au yule aliehubiri elimu bure mpaka kidato cha nne?
3.Prof.sera ya elimu bure ya mwaka 2010 ya CHADEMA ilikuwa rafiki zaidi kwa mwananchi wa kijijini au mjini?Na je kati ya Dr.Slaa na Kikwete ni nani alipata kura nyingi za vijijini?
4.Prof.kama watu wa vijijini ufisadi kwao ni issue,mwaka 2010 ni nani kati ya Dr.Slaa na Kikwete aliepata kura nyingi kutoka kwa watu wa vijinini?
4.Prof.unataka kuniambia kama Lowassa angepitishwa na CCM katika uchaguzi wa mwaka huu, watu wa vijijini wasingempaka kura kwasababu ya tuhuma za ufisadi zinazomkabili na badala yake wapiga kura wengi wa vijijini wangempigia kura mgombea wa UKAWA?
Prof. are you seriuos abaout this article?
I wonder!!