Prof Kabudi: Ufafanuzi kuhusu makubaliano kati ya Serikali na Barrick

Michael Amon

JF-Expert Member
Dec 22, 2008
8,775
3,610
Ningependa kufafanua kuhusu makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kampuni ya madini ya dhahabu ya Barrick, na hasa kuhusu swala zima la mgao wa faida wa 50/50. Jambo limekuwa kwa watu wengine halifahamiki vizuri.

Serikali itapata 16% ya hisa ambazo zinapatikana bila malipo yaani free credit interest kwa mujibu wa sheria ya madini kama ilivyobadilishwa. Kwa maana hiyo basi, Barrick wanabaki na asilimi 84% ya hisa.

Kwa hali ya kawaida katika mgao wa faida serikali ilitakiwa ipate 16% na Barrick ipate 84%. Lakini badala ya Serikali kupata 16% sasa serikali itapata mgao wa faida wa asilimia 50% ingawa hisa zake ni 16% na Barrick nayo itapata mgao wa faida wa 50% ingawa hisa zake ni 84%.

Na hiyo 50/50 itapatikana baada ya kampuni ya Barrick kuwa imelipa kodi zote za serikali. Mapato ya kodi ambayo serikali inayachukua kisheria hayahesabiwi kwenye mgao wa faida wa 50/50. Ile faida iliyosalia baada ya kampuni kulipa kodi zote ndicho kinachogawana na serikali 50/50. Kwa maana hiyo basi, ukijumlisha kodi zote zilizolipwa kabla ya kugawana kwa 50/50 hapo serikali na Watanzania wanakuwa hawapati mgao wa faida wa 50/50 bali wanapata 70/30.

Kwa hiyo ningependa hilo lieleweke wazi kabisa kwamba tulihakikisha kwamba yale mapato stahili ya serikali yanabaki pale pale kama yalivyo ndani ya sheria na kinachokuja kugawanywa 50/50 ni kile kilichobaki baada ya kodi zote na ushuru wote wa serikali kulipwa.

Sasa ukitizama hapo serikali yenye hisa ya 16% inakuja kupata mapato ya kodi ya 70% na mgawanyo wa 50/50, atakayesema hayo sio mafanikio basi tumuombee Mwenyezi Mungu ampe akili na macho na masikio ya kuona na kufahamu yaliyofanikiwa. Na hilo halijawahi kutokea kokote duniani.

Kampuni ya Barrick inatumia mgawanyo wa faida wa 50/50 nchini Dominika, Saudi Arabia na Argentina. Lakini mgawanyo wa faida wa 50/50 wa nchi za Dominika, Saudi Arabia na Argentina unajumlisha pamoja na kodi ambazo serikali inazikusanya ila sisi kipengele hicho tulikikataa na ilikuwa ni moja kati ya mambo ambayo yalikuwa na mvutano mkubwa wakisema kwa nini Tanzania tunataka tuwe tofauti na nchi za Dominika, Argentina na Saudi Arabia. Lakini tumefanikiwa kuwafikisha kwenye makubaliano katika mazungumzo haya. Na sisi tunahesabu haya kuwa ni mafanikio makubwa kuliko ambavyo wenzetu wa Argentina, Venenzuaela, Dominika na Saudi Arabia wameyapata kutoka kwa Barrick. Kwa hiyo kwa Tanzania tuna kila sababu ya kusema tumepiga hatua kuliko wale ambao walitutangulia katika swala hili.

Na kwa hali hiyo kabisa naomba nirudie tena kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuliamsha hili dude. Baada ya hili dude kuamka ambalo lilianzia kwenye makinia na wengi walidhani shughuli yetu ni makinia. Sisi tulipokwenda kwenye majadiliano tulikuwa tunajadili mambo makuu 5 nje ya makinia. Lengo letu lilikuwa ni kuyatumia mazungumzo haya kama alivyotuelekeza mwenyewe Mh. Rais, kufungua muelekeo mpya wa usimamizi wa maliasili za nchi yetu na madini.

Kwa hiyo wengi walidhani kuwa hoja ni ya makinikia lakini katika akili na mipango ya Mh. Rais alivyotuagiza nendeni zaidi ya makinia ili Taifa liweze kuweka muelekeo mpya katika matumizi na usimamizi wa rasilimali zake ambao ni pamoja na madini na ndio maana umeona katika mazungumzo yetu hatukujikita tu kwenye makinia. Tungejikita tu kwenye makinikia tungeishia kupata malipo ya fedha tu. Lakini sasa tumepata zaidi ya hayo kwa sababu yeye mwenyewe Rais katika mkakati wake lengo lilikuwa tunaanza na makinikia lakini tunafungua mambo mengine zaidi kuhakikisha sheria yetu inatekelezwa na ndio maana katika mazungumzo haya sheria zote zilizotungwa na bunge hivi karibuni; zimeheshimiwa na kuzingatiwa kikamilifu katika muafaka tulioufikia.

 
Barrick


Ningependa kufafanua kuhusu makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kampuni ya madini ya dhahabu ya Barrick, na hasa kuhusu swala zima la mgao wa faida wa 50/50. Jambo limekuwa kwa watu wengine halifahamiki vizuri.

Serikali itapata 16% ya hisa ambazo zinapatikana bila malipo yaani free credit interest kwa mujibu wa sheria ya madini kama ilivyobadilishwa. Kwa maana hiyo basi, Barrick wanabaki na asilimi 84% ya hisa.

Kwa hali ya kawaida katika mgao wa faida serikali ilitakiwa ipate 16% na Barrick ipate 84%. Lakini badala ya Serikali kupata 16% sasa serikali itapata mgao wa faida wa asilimia 50% ingawa hisa zake ni 16% na Barrick nayo itapata mgao wa faida wa 50% ingawa hisa zake ni 84%.

Na hiyo 50/50 itapatikana baada ya kampuni ya Barrick kuwa imelipa kodi zote za serikali.



Barrick wanamiliki 63% ya shares za acacia, sasa hizo 16% za shares barrick watabakisha 47% ya shares

50/50 ya faida wakati shares zao ni 63%?
 
Kwa kweli haya ni maajabu! Mwenye shares kidogo apate mgawo mkubwa zaidi was faida. Anyway, hii ni lugha imaekaa kisiasa zaidi na utekelezaji bado utategemea sheria zetu wenyewe. Acacia walete mtaji, wafanye uzalishaji, masoko na mauzo, walipe mrahaba 6%, waipe serikali 16% free shares, walipe kodi za halmashauri na barabara, halafu serikali ipate mgawo wa faida sawa sawa na Barick/Acacia!!!

This too good to be true! Time will tell me when to celebrate!
 
Yaani ukilipa kodi zote

Running cost zote

Other originated and disturbances cost zote

Wakati huo unatake care ya gharama zote kama kampuni.

Alafu kwenye profit huyu wa vipande 16 vya mgao anapata sawa na yule wa vipande 84.....sijawahi ona hesabu ya namna hii....

Basi hakuna maana ya mgawanyo washare kwa maana nani kabeba mzigo mzito kila siku halafu mwisho wa safari mnagawana pasu.....is a ridiculous stand and non sense.
 


Ningependa kufafanua kuhusu makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kampuni ya madini ya dhahabu ya Barrick, na hasa kuhusu swala zima la mgao wa faida wa 50/50. Jambo limekuwa kwa watu wengine halifahamiki vizuri.

Serikali itapata 16% ya hisa ambazo zinapatikana bila malipo yaani free credit interest kwa mujibu wa sheria ya madini kama ilivyobadilishwa. Kwa maana hiyo basi, Barrick wanabaki na asilimi 84% ya hisa.

Kwa hali ya kawaida katika mgao wa faida serikali ilitakiwa ipate 16% na Barrick ipate 84%. Lakini badala ya Serikali kupata 16% sasa serikali itapata mgao wa faida wa asilimia 50% ingawa hisa zake ni 16% na Barrick nayo itapata mgao wa faida wa 50% ingawa hisa zake ni 84%.

Na hiyo 50/50 itapatikana baada ya kampuni ya Barrick kuwa imelipa kodi zote za serikali. Mapato ya kodi ambayo serikali inayachukua kisheria hayahesabiwi kwenye mgao wa faida wa 50/50. Ile faida iliyosalia baada ya kampuni kulipa kodi zote ndicho kinachogawana na serikali 50/50. Kwa maana hiyo basi, ukijumlisha kodi zote zilizolipwa kabla ya kugawana kwa 50/50 hapo serikali na Watanzania wanakuwa hawapati mgao wa faida wa 50/50 bali wanapata 30/70.


Kama hili la 50/50 likipita, nitatembea bila nguo kutoka Ubungo stendi ya daladala (Simu 2000) mpaka Kivukoni kwenye pantoni.

Wanatuona wajinga sana hawa jamaa, eti 50/50.
 
Duh, huu ni uongo wa wazi kabisa! Yaani Tufurahie dividend ya 16%
Tufurahie kodi..
Tufurahie 50% Kavu kavu!
Hapo achilia mbali "posho" ya 700mil

Hakuna Mzungu chini ya jua anakubali hiyo! Hatakama ni Mimi siwezi kukubali huo upuuzi..

Kumbe ndo tunaongozwa na watu wa hivi? Doh salaaaleh..!!
 
Sawa ila ni mapema sana kuzungumzia kuhusu utekelezaji wake, inawezekana na kuna uwezakano mkubwa kwamba hii migodi inayomilikiwa na barrick life spine yake inaelekea kuisha au wameshapata faida vya kutosha kwa hiyo hata wakikubali hawana cha kupoteza, anyway is a good move.
Lazima yatakuwepo masharti ya utekelezaji ambayo watanzania hatutayajua.

Time will tell me when to celebrate.
 
Back
Top Bottom