Unapata wapi mamlaka ya kuhoji uumini wa akhy Mussa Assad??
Unajifanya mjuaji wa dini?? Ngoja tukufunze basi ili ujinga ukutoke.
Katika Uislam muongozo na mazingatio ya kwanza kabisa hufanywa kwenye Qur an. Yaani tutafuata maelekezo ya Qur an kabla ya hadith. Sasa nenda rudia Qur an 4:71 Allah anatuamrisha tuchukue tahadhari katika mambo.
Wewe unamuona mtu ni mjinga na anahistoria mbaya ikiwa utakinzana nae au kugombana nae au kubishana nae, Muongozo wa dini yetu ni kuchkua tahadhari usigombane nae maana ukigombana nae atakudhuru.
Ni jukumu la kwanza kabisa kwa Muislam kuilinda nafsi yake. Imtoshe mtu kuchukia ndani ya nafsi yake na kukaa kimya hata kama kuna ubaya unatendeka ikiwa ubaya huo hawezi kuuondosha kwa mkono wake au kwa mdomo wake.
Aliekutuma mwambie Prof. Assad anajitambua.
Muacheni mama afanye kazi
Kaka ngoja nikuweke sawa kidogo,naona umeandika haya uliyo yaandika kama Hadithi huwa ina pingana na Qur'aan vile (hii ni kwa mujibu wa siyaki ya maneno yako) wakati viwili hivi havipingani kama alivyosema imaam Shawkaniy (Allah amrehemu) na ukisoma kitabu cha Mwanazuoni Muhammad al Amiin ash-Shanqitwiy (Allah amrahamu).
Mimi,nakuuliza swali,kwani hiyo aya ilishuka kwa sababu gani ? Je hiki anachokifanya mzee wetu ametanguliwa na nani katika wasomi wa dini katika ufanyaji huu au kuna swahaba aliwahi kupita mapito haya ?
Kaka maiti haisemwi kwa ubaya haya ndiyo mafundisho yetu sisi Waislamu,kwani Mtume anasema ya kuwa maiti wanayaendea yale waliyo yatanguliza,ndiyo maana tunapokuwa makaburini,tuna himizwa sana kuwaombea msamaha ndugu zetu (hapa namaanisha kwa muislamu mwenzetu),lakini hurusiwi kwa maiti yoyote.
Ukweli ni kwamba hasa kwa ndugu zangu Waislamu nawausia kujizuia na hizi kadhia. Kwani sisi tuna muongozo tayari na unajitosheleza.
Lakini ukisoma hukumu za watawala waouvu katika Uislamu,haturuhusiwi kuwakosoa hadharani,seuze kuwasema kwa ubaya.
Mimi mzee wangu Profesa Assad (Allah amuhifadhi na amuongoze) nimempa udhuru kwa kumdhania kheri ya kuwa si msomi wa dini.
Uislamu ndiyo Sunna(Hadithi) na Sunna(Hadithi) ndiyo Uislamu,havitengani viwili hivi.