Prof Assad ameonesha mfano kwa wasomi wetu

Prof Assad ameonesha mfano kwa wasomi wetu

So hizi figisu figisu za jiwe kwa mgongo wa spika zinalenga kufuta masalia ya Jeikei ?
 
Pamojs na usomi wake tusisshau jinsi nafasi yake inavyolindwa na katiba lakini licha ya kulindwa na katiba kwa nafasi ya jaji mkuu jamaa hajiamini kabisa
 
Kigwangala. Mkuchika, Makmba
Mwisho wa siku munamtuhumu tu Spika lakini CAG aliamsha ye mwenyewe huu mgogoro..!
Aliamsha ki vipi?hivi kama wewe unapaswa kufuatilia mapato na matumizi ya serikali halafu hufatulii ni udhaifu wa cag au spika???jibu tuu hapo
 
Prof Musa Assad Juma , ametoa fundisho la kutosha kwa tasnia inayo jiita ya wasomi hapa nchini.

Mbali ya kuonyesha jicho na fikra za msomi zinavyo stahili kuwa, lakini pia ameonyesha jinsi wacha Mungu wanavyo stahili kuusimamia ukweli.

Kuna kipindi fulani waliitwa hao wanajiita wasomi kwenda kuzungumzia ni jinsi gani serikali yetu inavyo weza kujiendesha na kutuletea mafanikio, mbona ilikuwa ni aibu , badala ya kushauri wao wabaki kutoa sifa za uongo uongo tu, kwa ukweli walitia aibu ya kupindukia.

Ni wazi kuwa awamu hii imekuja na kamtindo fulani ka kukataa kuambiwa ukweli, lkn Assad jipe moyo na watanzania wameona utendaji wako.

Ni wazi kuwa yajayo yanaweza yasifarahishe sana , lakini baki kuwa shujaa kwa kuto mpigia magoti shetani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Profesa Assad endelea KUBAKI MULE MULE, USIYUMBE WALA KUYUMBISHWA NA YEYOTE. WATANZANIA TUKO NYUMA YAKO!!!!
 
So far sijaona hoja yoyote ya CAG inayoelezea udhaifu wa bunge...huu sio usomi bali ni uropokaji ndio maana wanaoushangilia ni Nyumbu
Ukishakuwa JINGALAO huwezi kuelewa chochote. Na kama ukimtazama binadamu unaona NYUMBU, basi tatizo lako siyo UJINGA tu, bali MAGONJWA MTAMBUKA
 
Kuwa msomi haimaanishi wewe kuona wengine kazi zao ni dhaifu.Kilikuwa ni kitu kidogo tu cha kuomba radhi na kufafanua hilo neno lake la udhaifu wanavyolitumia kwenye kazi yao kama neno la kawaida.Vinginevyo alionyesha kuwa yeye ni anadharau na hata kuweka sifa mbaya kwa wasomi ni watu wenye dharau wakiwa makazini.Nchi haindeshwi kwa misifa na majivuno ya usomi bali ni kwa weledi na ustahimilivu na kufuata sheria basi.
Unastahili kufanyiwa tohara ya akili ndo ujitambue, bila ya hivyo utazidi kubaki gizani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwa msomi haimaanishi wewe kuona wengine kazi zao ni dhaifu.Kilikuwa ni kitu kidogo tu cha kuomba radhi na kufafanua hilo neno lake la udhaifu wanavyolitumia kwenye kazi yao kama neno la kawaida.Vinginevyo alionyesha kuwa yeye ni anadharau na hata kuweka sifa mbaya kwa wasomi ni watu wenye dharau wakiwa makazini.Nchi haindeshwi kwa misifa na majivuno ya usomi bali ni kwa weledi na ustahimilivu na kufuata sheria basi.
Hujui usemalo! We unajua kwenye kamati aliulizwa nini na alijibu nini? Unajua alitoa maelezo gani kuhusu maana ya neno "dhaifu" kama linavyotumika kwenye tasnia ya ukaguzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukishakuwa JINGALAO huwezi kuelewa chochote. Na kama ukimtazama binadamu unaona NYUMBU, basi tatizo lako siyo UJINGA tu, bali MAGONJWA MTAMBUKA
Kama kuna hizo hoja au taarifa zenye kuonesha udhaifu wa Bunge kwa mujibu wa Assad ziweke hapa ...mimi sina ujasiri wa mbwa hata siku moja
 
Siyo kweli kuwa wateule wa JK amebakia Prof Assad tu - ona aibu:-
(i). Dkt Albina Chuwa - Ofisi ya Taifa ya Takwimu si mteule wa JK?
 
Back
Top Bottom