Press Release TRA kuhusu VAT

Press Release TRA kuhusu VAT

Hii 18% italipwa na mlaji, angalia hii kauli "this will be collected by the bank or a Financial Institutions that supplied the service". Will be collected, not will be paid by a Financial Institutions that supplied the service.

Kwa maana nyingine Taasisi za kifedha ni Wakala wa TRA kukusanya hii 18% kutoka kwa mteja/mlaji.
 
Unatakiwa kufanya "Tax planning" kama ulikuwa unaenda kutoa pesa mara nne kwa mwenzi, andaa bajeti ya mwezi na ukatoe pesa mara moja kwa mwezi utaokea VAT ya miamala mitatu.

TULIPE KODI KWA MAENDELEO YA NCHI YETU
Naam unaweza kufanya hilo, lakini kwa jinsi nilivyo kadri pesa inavyokuwepo mfukoni ndivyo matumizi yanavyoongezeka. Kwa ufupi kuchukua pesa kidogokidogo hunisaidia kuwa na bakaa na kdri hiyo bakaa inavyoongezeka ndivyo inavyonisaidia kuwekeza kwenye shughuli nyinginezo.
 
Naam unaweza kufanya hilo, lakini kwa jinsi nilivyo kadri pesa inavyokuwepo mfukoni ndivyo matumizi yanavyoongezeka. Kwa ufupi kuchukua pesa kidogokidogo hunisaidia kuwa na bakaa na kdri hiyo bakaa inavyoongezeka ndivyo inavyonisaidia kuwekeza kwenye shughuli nyinginezo.
Ukichukua mara moja hutembei nazo bali unanunua mahitaji yote muhimu ya mwezi mzima; kwanza hii itakufanya kuwa na akiba kubwa zaidi kwa hutotoa pesa nyingine labda itokee msiba au ugonjwa. Nasikia siku hizi hata usafiri unaweza nunua kadi ya mwezi mzima shida iko wapi?

TULIPE KODI KWA MAENDELEO YA NCHI YETU
 
Kweli hii nchi inazidi kuwa na maajabu mengi. Baada ya kuletwa VAT kwenye huduma zinazotozwa na benki, benki waliwaarifu wateja juu ya mabadiliko hayo na kuonesha kuwa kwa sasa kutakuwa na ogezeko la tozo kwa 18%. Baada ya kuwa na mjadala kwenye mitandao na kwingineko,TRA wakajibu hoja kuwa mabenki yamekosea na kusema tozo zilipaswa kubaki vile vile ila hiyo 18% itatozwa kwenye kile kile walichokuwa wanapata benki. TRA wakasisitiza kabisa kuwa mteja hatapata ongezeko lolote na kuzitaka benki ziache mara moja kufanya vinginevyo.
Sasa leo hii TRA wale wale wanatoa maelezo yanayoendana na maelezo yalotolewa na benki zote pale mwanzo. Hivi hawa TRA tuwaeleweje? Wanapataje leo ujasiri wakusema kile walichokipinga mwanzo? Weledi wao ukoje? Hivi wanadhani watanzania hawajuii chochote au? Kwa kutaka kutulaghai wanachomekea kipengeli " Akiba ya mteja haitaathirika kutokana na sheria hii", Je ni lini benki zilisema akiba ya mteja itaathirika? Kama ilikuwa nikwate 1000 lakini sasa nakatwa 1180, hiyo 1180 si itapunguza akiba yangu?
TRA walipaswa kuja na kuomba radhi kwa kuwapotosha watu hapo mwanzo na wakiri kuwa benki zilikuwa sahihi ila wao ndio waliokosoa. Hili pia ni funzo kwa wale wanaopenda kushabikia tu na kusapoti kila kitu kwani wengine tulisema toka mwanzo hakuna kitu cha namna ile ila watu wkabisha. Sasa tuweni wakweli tu na vitu vya kiutaalum viongelewe vivyo hivyo na sio kishabiki.
 
wakuu mwenye taarifa za ukweli atoe.

Hilo bandiko mimi nimeweka tu, kama ni kweli mtu athibitishe.

Na kama ni kweli kwanini TRA walisema siku ile kwenye press conference kwamba mteja hatachajiwa. Nakumbuka vizuri walisema Bank ndo watalipa hii VAT.

Sasa iweje watoe directive kwa Kiingereza kwamba mteja ndo alipe. Lugha yenyewe iliyotumika hata msomi kuielewa inahitaji uwe na dictionary karibu.
benk wakilipa itakuwaje VAT? UNAJUA MAANA YA VAT?
 
Ukichukua mara moja hutembei nazo bali unanunua mahitaji yote muhimu ya mwezi mzima; kwanza hii itakufanya kuwa na akiba kubwa zaidi kwa hutotoa pesa nyingine labda itokee msiba au ugonjwa. Nasikia siku hizi hata usafiri unaweza nunua kadi ya mwezi mzima shida iko wapi?

TULIPE KODI KWA MAENDELEO YA NCHI YETU
Kununua mahitaji muhimu mara moja kwa mwezi mzima? Hiyo haiwezekani kwa jinsi hali ya hewa ilivyo. Utasema inawezekana kwa kuhifadhi kwenye friji wakati umeme wenyewe hautabiliki.
 
Mrembo! Tiririka vizuri, huu ni mjadala hauhitaji hasira wala papara, toa ufafanuzi kama tulivyofanya kwenye post za awali.
nilikosea sio benk wakilipwa ni wakilipa ! mimi nina kazi zangu bna kuandika maelezo marefu siwezi.
 
Asante kwa ufafanuzi na Mungu aibarki kazi ya mikono yako.
VAT bana ni kodi ya ongezeko la thamani na hapa kwetu tz ongezeko lake ni 18% ya bei husika
sasa basi ukisema uongeze Vat kwenye kitu flani.ina maana utajumlisha 18% kwenye bei husika na hyo 18% inatakiwa ilipwe na mlipaji sio mlipwaji
kwaiyo huko benk kama wanacharge 1000 na serikali ikataka VAT
itabidi waongeze 18%
bank wakitoa 18% kwenye elf yao hyo sio vat itakuwa kitu kingine sijui kiitweje?
ila as long as VAT is concerned HYO ITALIPWA TU NA MTEJA MKUU
SIJUI KAMA NIMEPATIA KUKUELEZA MI MVIVU SANA KUANDIKA HADI NIMECHOKA
 
Kununua mahitaji muhimu mara moja kwa mwezi mzima? Hiyo haiwezekani kwa jinsi hali ya hewa ilivyo. Utasema inawezekana kwa kuhifadhi kwenye friji wakati umeme wenyewe hautabiliki.
Unaweka "stock" ya vitu visivyoharibika na vile vinavyoharibika "perishables" unaweka bill kwenye magenge fullstop.

TULIPE KODI KWA MAENDELEO YA NCHI YETU
 
Kweli hii nchi inazidi kuwa na maajabu mengi. Baada ya kuletwa VAT kwenye huduma zinazotozwa na benki, benki waliwaarifu wateja juu ya mabadiliko hayo na kuonesha kuwa kwa sasa kutakuwa na ogezeko la tozo kwa 18%. Baada ya kuwa na mjadala kwenye mitandao na kwingineko,TRA wakajibu hoja kuwa mabenki yamekosea na kusema tozo zilipaswa kubaki vile vile ila hiyo 18% itatozwa kwenye kile kile walichokuwa wanapata benki. TRA wakasisitiza kabisa kuwa mteja hatapata ongezeko lolote na kuzitaka benki ziache mara moja kufanya vinginevyo.
Sasa leo hii TRA wale wale wanatoa maelezo yanayoendana na maelezo yalotolewa na benki zote pale mwanzo. Hivi hawa TRA tuwaeleweje? Wanapataje leo ujasiri wakusema kile walichokipinga mwanzo? Weledi wao ukoje? Hivi wanadhani watanzania hawajuii chochote au? Kwa kutaka kutulaghai wanachomekea kipengeli " Akiba ya mteja haitaathirika kutokana na sheria hii", Je ni lini benki zilisema akiba ya mteja itaathirika? Kama ilikuwa nikwate 1000 lakini sasa nakatwa 1180, hiyo 1180 si itapunguza akiba yangu?
TRA walipaswa kuja na kuomba radhi kwa kuwapotosha watu hapo mwanzo na wakiri kuwa benki zilikuwa sahihi ila wao ndio waliokosoa. Hili pia ni funzo kwa wale wanaopenda kushabikia tu na kusapoti kila kitu kwani wengine tulisema toka mwanzo hakuna kitu cha namna ile ila watu wkabisha. Sasa tuweni wakweli tu na vitu vya kiutaalum viongelewe vivyo hivyo na sio kishabiki.
Mkuu na Job K mko sahihi. Yaani TRA kwa sasa wamepita mle mle walimokuwa bank na financial institutions zingine kwamba 18% iliyopewa jina la VAT zitabebwa na mteja japo awali walidai zitabebwa na mtoa huduma. Hii ni aibu sana kwa TRA kwa kutoa ufafanuzi unaokinzana.

Kwa jinsi ilivyo hakuna kitakachokuja kubadilika juu ya gharama hizi ambazo kimsingi zimeshapitishwa rasmi japo kiaina kubebwa na mpokea huduma wakati wa kufanya miamala yake.
 
Mnnh...mbona niliona bandiko CRDB kuwa sasa kuna charge ya VAT karibu kwenye kila huduma except interest...
Mnatuchanganya...
Service charges/fee kwenye nini sasa?
Na VAT analipa nani? Si ni kodi ya mlaji?
 
Unatakiwa kufanya "Tax planning" kama ulikuwa unaenda kutoa pesa mara nne kwa mwenzi, andaa bajeti ya mwezi na ukatoe pesa mara moja kwa mwezi utaokea VAT ya miamala mitatu.

TULIPE KODI KWA MAENDELEO YA NCHI YETU
Ina maana wanacharge number of times au kiasi ulichotoa?
Na kama nina matumizi makubwa si ni kunilazimisha nikae na cash ndani sasa?
Yani hii consequence haikwepeki...mtu utaanza kutamani na mshahara upewe dirishani ...mshahara unafyekwa kodi..bado viela vyangu niweke benki vikombwe...nikinunua bidhaa nalipa VAT...shiider
 
Kwa maelezo hayo bado mzigo unabaki kwa mteja,bank wao wanabakia salama na hizo gharama zinalipwa na mteja,Kama ingekuwa inakatwa kwa bank basi katika 1000 TRA ingechukua 180 yake na bank ingebakiwa na 820 na kusingekuwa na effect yoyote kwa mteja.
 
VAT bana ni kodi ya ongezeko la thamani na hapa kwetu tz ongezeko lake ni 18% ya bei husika
sasa basi ukisema uongeze Vat kwenye kitu flani.ina maana utajumlisha 18% kwenye bei husika na hyo 18% inatakiwa ilipwe na mlipaji sio mlipwaji
kwaiyo huko benk kama wanacharge 1000 na serikali ikataka VAT
itabidi waongeze 18%
bank wakitoa 18% kwenye elf yao hyo sio vat itakuwa kitu kingine sijui kiitweje?
ila as long as VAT is concerned HYO ITALIPWA TU NA MTEJA MKUU
SIJUI KAMA NIMEPATIA KUKUELEZA MI MVIVU SANA KUANDIKA HADI NIMECHOKA
Nimekuelewa sana na ndivyo ilivyo, kinacholalamikiwa ni kuwa, awali Taasisi za kifedha zilitoa matangazo yenye ufafanuzi kama huu walokuja nao TRA.
TRA wakasema hizi Taasisi za kifedha zimepotosha mteta atakatwa pesa ile ile ya kawaida na sisi (TRA) 18% yetu tutaikata kwenye ile 1000 aliyotozwa na Taasisi ya fedha.
 
Nimekuelewa sana na ndivyo ilivyo, kinacholalamikiwa ni kuwa, awali Taasisi za kifedha zilitoa matangazo yenye ufafanuzi kama huu walokuja nao TRA.
TRA wakasema hizi Taasisi za kifedha zimepotosha mteta atakatwa pesa ile ile ya kawaida na sisi (TRA) 18% yetu tutaikata kwenye ile 1000 aliyotozwa na Taasisi ya fedha.
Kwa maneno mengine wanawalazimisha benki kushusha hizi charges ili hapo kwenye elfu wagawane ...au before walikuwa wanakwepa kuipelekea serikali chake
 
Unatakiwa kufanya "Tax planning" kama ulikuwa unaenda kutoa pesa mara nne kwa mwenzi, andaa bajeti ya mwezi na ukatoe pesa mara moja kwa mwezi utaokea VAT ya miamala mitatu.

TULIPE KODI KWA MAENDELEO YA NCHI YETU
Hata ukitoa pesa Mara moja bado mwisho wa siku vat itakuwa ileile,mfano ukitoa elfu 10 kwa mara moja utakatwa 1800 na Kama utataka kutoa elfu 10000 kidogo kidogo jumla ya vat itakayokatwa itakuja kuwa 1800
 
Press release ya kingereza inaenda kwa waswahili.
 
Hata ukitoa pesa Mara moja bado mwisho wa siku vat itakuwa ileile,mfano ukitoa elfu 10 kwa mara moja utakatwa 1800 na Kama utataka kutoa elfu 10000 kidogo kidogo jumla ya vat itakayokatwa itakuja kuwa 1800
hujanielewa ukitoa 10,000 utakatwa 180; lakini ukitoa 2500 mara nne utakatwa 720
 
Back
Top Bottom