Presidential candidates.. CCM ilikua na utaratibu wa kuwaandaa viongozi wa nchi, hivi sasa kuna tatizo? Demokrasia?

Presidential candidates.. CCM ilikua na utaratibu wa kuwaandaa viongozi wa nchi, hivi sasa kuna tatizo? Demokrasia?

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,255
Reaction score
8,027
CCM MMEACHA NJIA MMEACHA KUANDAA VIONGOZI SASA UONGOZI NI KUENDANA NA UPEPO.

Wasalaam wanajukwaa!

Tokea enzi za Mwalimu CCM walikua na utaratibu wa kuandaa viongozi ambao baadaye tunawapata marais, speaker, Makamu wa Rais na mawaziri wakuu. Hivi sasa tuseme uongozi umekua ni kama zali hata mimi mkulima wa Mpunga huku Nzega nikikaa sawa naweza kua Rais wa nchi au waziri mkuu. Itategemeana na ushawishi wangu kwa anayegombea nafasi ya Urais kwa wakati uliopo akinichagua kua mgombea mwenza au hata Rais aliyepo madarakani. Tuseme labda ni kukua kwa Demokrasia ndani ya chama na nchi kwa jumla?

SIFA ZA PRESDENTIAL MATERIALS
1.Hua na hekima na busara
2.Hua na huruma na wananchi wa kawaida
3.Wazalendo wa kweli
4.Huzionea huruma rasilimali za nchi
5.Wavumilivu wanapokosolewa
6.Watu wa aina hii hujaribu hata kugombea mara nyingi nafasi ya Urais, hushindwa na kisha kurudia tena na mwishowe hushida.
7.Hua na mtazamo wa mbali zaidi kuhusu taifa.
8.Hua ni watu wa mageuzi
9.Hua tayari kuwajibika pale inapobidi


HASARA ZA KUTOANDAA PRESDENTIAL MATERIALS.
Hawa watu huandaliwa na mifumo ya vyama vya siasa na huanza kujitokeza kwenye kugombea nafasi za juu mapema.Kinyume na hapo watapatikana viongozi ambao kwa hua ni kama zali tu. Ukiwakosa watu wa aina hii utegemee kukutana na haya.

1.Hua siyo watu wa hekima na busara kwenye maamuzi.
2.Si wavumilivu kwenye kukosolewa
3.Hua ni watu wa visingizio hasa pale mambo yanapokwenda mrama
4.Si watu wa kuridhika na vyeo
5.Wengi hua watawala wa kiimla kwa maana ya kua na hofu na nafasi zao.
5.Wagumu kuwajibika
6.Hawana uchungu na rasilimali za taifa.
7.Uongozi kwao huja kama zali bila kutegemea, si watu wa kujaribu nafasi za juu kila mara.
8.Siyo wakweli mara nyingi

Hapa sizungumzii mtu wala kugusia cheo cha mtu ispokua nagusia mifumo yetu ndani ya vyama vya siasa tuna utaratibu wa aina hii
 
Subiri kwanza tukamilishe mamlaka kamili ya visiwani kwa gharama za vichogo
 
CCM MMEACHA NJIA MMEACHA KUANDAA VIONGOZI SASA UONGOZI NI KUENDANA NA UPEPO.

Wasalaam wanajukwaa!

Tokea enzi za Mwalimu CCM walikua na utaratibu wa kuandaa viongozi ambao baadaye tunawapata marais, speaker, Makamu wa Rais na mawaziri wakuu. Hivi sasa tuseme uongozi umekua ni kama zali hata mimi mkulima wa Mpunga huku Nzega nikikaa sawa naweza kua Rais wa nchi au waziri mkuu. Itategemeana na ushawishi wangu kwa anayegombea nafasi ya Urais kwa wakati uliopo akinichagua kua mgombea mwenza au hata Rais aliyepo madarakani. Tuseme labda ni kukua kwa Demokrasia ndani ya chama na nchi kwa jumla?

SIFA ZA PRESDENTIAL MATERIALS
1.Hua na hekima na busara
2.Hua na huruma na wananchi wa kawaida
3.Wazalendo wa kweli
4.Huzionea huruma rasilimali za nchi
5.Wavumilivu wanapokosolewa
6.Watu wa aina hii hujaribu hata kugombea mara nyingi nafasi ya Urais, hushindwa na kisha kurudia tena na mwishowe hushida.
7.Hua na mtazamo wa mbali zaidi kuhusu taifa.
8.Hua ni watu wa mageuzi
9.Hua tayari kuwajibika pale inapobidi


HASARA ZA KUTOANDAA PRESDENTIAL MATERIALS.
Hawa watu huandaliwa na mifumo ya vyama vya siasa na huanza kujitokeza kwenye kugombea nafasi za juu mapema.Kinyume na hapo watapatikana viongozi ambao kwa hua ni kama zali tu. Ukiwakosa watu wa aina hii utegemee kukutana na haya.

1.Hua siyo watu wa hekima na busara kwenye maamuzi.
2.Si wavumilivu kwenye kukosolewa
3.Hua ni watu wa visingizio hasa pale mambo yanapokwenda mrama
4.Si watu wa kuridhika na vyeo
5.Wengi hua watawala wa kiimla kwa maana ya kua na hofu na nafasi zao.
5.Wagumu kuwajibika
6.Hawana uchungu na rasilimali za taifa.
7.Uongozi kwao huja kama zali bila kutegemea, si watu wa kujaribu nafasi za juu kila mara.
8.Siyo wakweli mara nyingi

Hapa sizungumzii mtu wala kugusia cheo cha mtu ispokua nagusia mifumo yetu ndani ya vyama vya siasa tuna utaratibu wa aina hii
CCM sasaivi haiandai Viongozi inategemea CHADEMA iandae Viongozi alafu wenyewe iwachukue.

Ndo mana sasaivi anayeongoza kuandika Ilani ya CCM ni former mwana Chadema Prof. Kitila Mkumbo.

CCM sasaivi wana kazi moja tu. Kuandaa machawa na mafisadi.
 
CCM ya miaka 20 hii si chama cha siasa, ni genge la wachumia tumbo.

CCM hii ya sasa haina succession plan sababu sio tena chama cha siasa, hawapo hapo kwa ajili ya mustakabali mwema wa Tamzania, bali kwa manufaa yao.

CCM hawawezi kufanya research wao kama chama mpaka wanawatumia REDET.
Ilani ya CCM imeandikwa na watu ambao sio wana CCM, maana wao hawana watu makini na wenye weledi.
Ndio maana hata wakati Kitila Mkumbo anataka kuwataja waliohusika na kuandika ilani ya CCM ya 2025, mwenyekiti alikataza wasitajwe.
Kwa nini!!??
 
Back
Top Bottom