mTZ_halisi
Member
- Oct 26, 2007
- 82
- 2
Habarini za mchana
Jamani mimi kuna kitu kinanitatiza, nashindwa hata kuelewa. Kwa kawaida mtu unapokata ticket ya ndege as RETURN TICKET si huwa inaandika unaondoka lini na kurejea lini?
Sasa nimekuwa nashangazwa na baadhi ya ndege eti unapofika huko uendako say unatoka DAR umekwenda MWZ ukitaka kurudi lazima ufanye confirmation. Nijuavyo mimi baada ya kusafiri ndani na nje ya nchi kama sikupiga simu kwa airline nina maana kuwa nitarudi as per schedule. Nways, nimeshaona hata ndege za nje zinazotaka confirmation uwe unarudi on the day au unabadili schedule yako... SIIKUBALI ila ndio hivo tena.
Sasa tatizo lililonifanya niandike ni kuwa baada ya kufika MWZ kwa shuguli za kikazi, nimekaa kule nikapeleka ticket siku 3 kabla ya safari kuconfirm kuwa narudi siku hiyo iliyoandikwa. Tulikuwa group wakatupa OK kuwa tutaondoka na ndege ya Precision Air ya saa 2.35 asubuhi.
Tunafika airport kucheck IN eti wanasema kati yetu kuna watu kadhaa hawakutakiwa kuondoka na ndege ya asubuhi wataondoka saa 8 mchana. Kwa kweli habari hiyo haikukaa vizuri masikioni. Baada ya kubishana kwa muda kwamba kwa nini watupe OK tulipoconfirm na kutupa hata ticket kuonyesha tutaondoka asubuhi kisha siku ya safari tuwe tumekatwa?
Ati wakasema ilikuwa ije ndege ya watu 72, tumebadilisha kwa hiyo inabidi mwende mchana. Hivi unawezaje kuamua tu kubadili ndege gafla wakati unajua una wasafiri zaidi ya idadi ya hiyo ndege uliyoileta? Tukaja kugundua kuwa kuna wazungu walikuja kuconfirm baadae wakaamua kuwaweka wao kama 20 hivi na kuamua randomly kukata waswahili oh wana connection Dar... aliyekwambia hao uliowakata hawana commitment huko waendako ni nani?
Kwa kweli Precision hiki mfanyacho si sawa. Ticket mnatutoza karibia laki 4 return kisha mnatunyanyasa kama tunapanda dala dala haiko sawa. Hapo hapo mnafika Dar mizigo imebaki Mwz hivi kwa nini mnashindwa kufanya kazi zenu sawa sawa
HALAFU TUNASHANGAA KWA NINI HATUENDELEI TANZANIA. hivi vitu vidogo vidogo vinatufanya tuonekane hopeless na tunaendeleza upuuzi ktk maamuzi yetu ya kila siku.
Jamani samahanini kwa habari ndefu ila iliniuma sana, na wenyewe niliwambia MWZ na hata hapa Dar. Na for me I guess I will never waste my time with your airline again.
Jamani mimi kuna kitu kinanitatiza, nashindwa hata kuelewa. Kwa kawaida mtu unapokata ticket ya ndege as RETURN TICKET si huwa inaandika unaondoka lini na kurejea lini?
Sasa nimekuwa nashangazwa na baadhi ya ndege eti unapofika huko uendako say unatoka DAR umekwenda MWZ ukitaka kurudi lazima ufanye confirmation. Nijuavyo mimi baada ya kusafiri ndani na nje ya nchi kama sikupiga simu kwa airline nina maana kuwa nitarudi as per schedule. Nways, nimeshaona hata ndege za nje zinazotaka confirmation uwe unarudi on the day au unabadili schedule yako... SIIKUBALI ila ndio hivo tena.
Sasa tatizo lililonifanya niandike ni kuwa baada ya kufika MWZ kwa shuguli za kikazi, nimekaa kule nikapeleka ticket siku 3 kabla ya safari kuconfirm kuwa narudi siku hiyo iliyoandikwa. Tulikuwa group wakatupa OK kuwa tutaondoka na ndege ya Precision Air ya saa 2.35 asubuhi.
Tunafika airport kucheck IN eti wanasema kati yetu kuna watu kadhaa hawakutakiwa kuondoka na ndege ya asubuhi wataondoka saa 8 mchana. Kwa kweli habari hiyo haikukaa vizuri masikioni. Baada ya kubishana kwa muda kwamba kwa nini watupe OK tulipoconfirm na kutupa hata ticket kuonyesha tutaondoka asubuhi kisha siku ya safari tuwe tumekatwa?
Ati wakasema ilikuwa ije ndege ya watu 72, tumebadilisha kwa hiyo inabidi mwende mchana. Hivi unawezaje kuamua tu kubadili ndege gafla wakati unajua una wasafiri zaidi ya idadi ya hiyo ndege uliyoileta? Tukaja kugundua kuwa kuna wazungu walikuja kuconfirm baadae wakaamua kuwaweka wao kama 20 hivi na kuamua randomly kukata waswahili oh wana connection Dar... aliyekwambia hao uliowakata hawana commitment huko waendako ni nani?
Kwa kweli Precision hiki mfanyacho si sawa. Ticket mnatutoza karibia laki 4 return kisha mnatunyanyasa kama tunapanda dala dala haiko sawa. Hapo hapo mnafika Dar mizigo imebaki Mwz hivi kwa nini mnashindwa kufanya kazi zenu sawa sawa
HALAFU TUNASHANGAA KWA NINI HATUENDELEI TANZANIA. hivi vitu vidogo vidogo vinatufanya tuonekane hopeless na tunaendeleza upuuzi ktk maamuzi yetu ya kila siku.
Jamani samahanini kwa habari ndefu ila iliniuma sana, na wenyewe niliwambia MWZ na hata hapa Dar. Na for me I guess I will never waste my time with your airline again.