Posho mbili, Spika Sitta, Takukuru na Maadili yake!

-
- One of this day, nitachukua waya wa umeme na kupitisha ndani ya vichwa vya wa-Tanzania wengi sana, maana huu usingizi hauna mfano, I mean man amuka hawa Hosea na Sitta wote they belong to Segerea, sasa peleka them now garademiti!

- And yes, I said it they all belong to Segerea!, sasa peleka them now! kwa kutuletea wananchi this foolish Comedy, Sitta alitakiwa at this time awe anatayarisha kikao maalum cha bunge cha kumuwajibisha Hosea, kwanza kwa kuhukumiwa na kamati ya bunge ya Mwakyembe kwa kuhusika na ubadhirifu wa hela za wananchi walipa kodi, pili kwa kulidanganya taifa kwamba Lowassa na Richmonduli hawama makosa yanayo-amount to a crime against our Republic, na tatu kwa kuwatishia nyau wabunge, Full Stop!

Respect.

FMEs!
Hii ya kupeleka wasanii wote Segerea ni nzuri, waonaje kama tungeanzia na wasanii waliochota fedha za EPA kuingilia madarakani, pamoja na hao waliofaidika na matunda hayo ndio kisa wanalindana?.

Waonanaje hata tungewajumuisha na Wale wote waliofanya kampeni chafu kutomia photo shup na waliowatuma?, ndipo tumalizie na kina Hosea na Six, au turudi nyuma zaidi tangu enzi za 'Tingatinga?'.
 
Hii ya kupeleka wasanii wote Segerea ni nzuri, waonaje kama tungeanzia na wasanii waliochota fedha za EPA kuingilia madarakani, pamoja na hao waliofaidika na matunda hayo ndio kisa wanalindana?.

Waonanaje hata tungewajumuisha na Wale wote waliofanya kampeni chafu kutomia photo shup na waliowatuma?, ndipo tumalizie na kina Hosea na Six, au turudi nyuma zaidi tangu enzi za 'Tingatinga?'.

- Blah! blah! wapi hoja za kulisaidia taifa na wananchi walalahoi? Sitta na Hosea wakutana uso kwa uso breaking news my foot!

- Now it is very clear, nani should be the first candidate wa huu waya wa umeme kuingia kichwani mwake ili aamuke na usingizi mzito sana!

Respect.


FMEs!
 
Charles mulinda ni nani? .................ameshakula hela za mafisadi sasa ndio anataka kutafuta umaarufu yaani mahali pa kutokea kupitia migongo ya watu......................HUYU TUMPUUZE NA KUMUOGOPA KAMA UKOMA.

Tofauti ya mawazo ndio itakayotutoa katika lindi la umaskini .................
 
- Blah! blah! wapi hoja za kulisaidia taifa na wananchi walalahoi? Sitta na Hosea wakutana uso kwa uso breaking news my foot!

- Now it is very clear, nani should be the first candidate wa huu waya wa umeme kuingia kichwani mwake ili aamuke na usingizi mzito sana!

Respect.

FMEs!
Alaa kumbe...!
 
- Blah! blah! wapi hoja za kulisaidia taifa na wananchi walalahoi? Sitta na Hosea wakutana uso kwa uso breaking news my foot!

- Now it is very clear, nani should be the first candidate wa huu waya wa umeme kuingia kichwani mwake ili aamuke na usingizi mzito sana!

Respect.

FMEs!

Please give the devil his due, you should've been proud that JF was the first to break it! leo ndio front imeuza karibu kila gazeti. Au kwa sababu nimegusia na 'Tingatinga' ?.
 
inategemea kama umekielewa ninachokitetea; wengine mnazungumzia posho mimi nazungumzia kitu kingine kabisa.
Kama ni hivyo ni sawa.PCCB ni moja ya TAASISI za UMMA zenye wasomi wengi wa SHERIA. Hawawezi kufanya kazi ya uchunguzi wowote ule bila ya kujiridhisha kwanza kwamba hawaendi kinyume na KATIBA yetu.
 
Spika Sitta,Waziri MKuu Pinda watofautiana kuhusu TAKUKURU


lowassasitta.jpg


Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Mbunge Silaju Kaboyonga na Spika Samweli Sitta wakijadili jambo nje ya Bunge jana Mjini Dodoma.

Na Mwandishi Wetu,Dodoma
Mwananchi
10/27/2009

MSUGUANO kati ya mihimili miwili, Bunge na Serikali umejitokeza baada ya Spika Samuel Sitta na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutofautiana kuhusu hatua ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwahoji wabunge kuhusu tuhuma za watunga sheria hao kulipwa posho mara mbili.

Wakati tofauti hizo zikijidhihirisha kwenye kikao cha faragha cha wabunge kilichofanyika ukumbi wa zamani wa Bunge unaojulikana kama Pius Msekwa, mmoja wa vinara wa vita dhidi ya ufisadi, Dk Harrison Mwakyembe aliongea na waandishi wa habari na kushutuma vikali kitendo hicho cha Takukuru akikielezea kuwa ni cha kisasi na kusema kamwe hatakubali kuhojiwa.

Hatua ya Takukuru kuhoji wabunge hao imetokana na malalamiko kutoka taasisi na mashirika mbalimbali kulalamikia mwenendo wa Kamati za Bunge kudai posho mara mbili kwenye idara na taasisi za serikali. Bunge hugharimia posho kwa ajili ya shughuli za kamati zao zinazosimamia vyombo hivyo, lakini baadhi ya wabunge walidaiwa kuendelea kupokea posho mara mbili, hali ambayo iliilazimisha Takukuru kuanza kuwahoji wanaotuhumiwa kufanya hivyo.

Lakini wabunge, akiwemo Spika Sitta, wamekuwa wakipinga kitendo hicho na jana serikali ilionekana kuunga mkono wabunge kuhojiwa huku Bunge likiendelea kupinga.

Tofauti za watendaji hao wawili wa serikali na Bunge zilizijitokeza jana mchana wakati wabunge walipokutana kwa faragha kupokea taarifa ya agenda zilizopitishwa na Kamati ya Uongozi kwa ajili ya kujadiliwa kwenye mkutano unaoendelea mjini hapa.

Suala la kuhojiwa kwa wabunge lilizua mjadala mkali kiasi kwamba mkutano huo, ambao awali ulikadiriwa kuwa ungechukua takriban saa moja kuanzia saa 5:15 asubuhi, ulimalizika karibu saa 8:00 alasiri.

Katika mjadala huo, mbunge wa Dole, Juma Suleiman N’hunga (CCM) alienda mbali na kusema chombo kilichopaswa kuwahoji wabunge ni Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge na sio Takukuru ambao ni mhimili mwingine wa dola.

Kwa mujibu wa mbunge huyo, kitendo cha Takukuru kuwahoji wabunge ambao ni mhimili wa Bunge ni ukiukwaji wa katiba na akapendekeza Takukuru ikatazwe kuendelea na zoezi lake la kuwahoji wabunge.

Mbunge mwingine aliyechangia mjadala huo mzito alipendekeza Bunge limpigie kura ya kutokuwa na imani na mkurugenzi wa Takukuru, Dk.Edward Hoseah kama ilivyotokea kwa taasisi kama hiyo nchini Kenya.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walitofautiana katika suala hilo, huku baadhi wakihoji sababu za chombo hicho kukaa kimpya wakati Basil Mramba alipohojiwa na kushitakiwa mahakamani.

Mramba, aliyekuwa waziri wa fedha katika serikali ya awamu ya tatu na baadaye waziri wa miundombinu katika serikali ya Rais Jakaya Kikwete, anakabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya ofisi iliyoiingizia serikali hasara ya mamilioni.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zimedokeza kuwa Mramba alitumia mkutano huo kuelezea kwa kirefu namna alivyohojiwa na Takukuru katika mazingira ya kudhalilisha tena na vijana wadogo ambao hawakustahili kumhoji.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, William Shelukindo naye alitumia kikao hicho kuelezea masaibu yaliyomkuta wakati alipoitwa na Takukuru kutoka jimboni kwake hadi Dar es Salaam na kuhojiwa kwa saa nne.

Shelukindo alihoji inakuwaje Takukuru ianzishe uchunguzi huo sasa wakati ambao Bunge linatakiwa kupokea utekelezaji wa maazimio yake ambayo baadhi yanataka DK Hosea awajibishwe.

Pamoja na Spika kueleza kuwa tayari ameandaa mazingira mazuri yatakayotumika kuwahoji wabunge hao ikiwamo kuipatia Takukuru ofisi kwenye jengo la Bunge mjini Dodoma na Dar es Salaam Salaam, bado baadhi ya wabunge walipinga.

Kutokana na michango ya wabunge wengi kuonyesha dhahiri kukerwa na kitendo cha Takukuru, Spika Sitta alitangaza katika kikao hicho kuwa kuanzia hiyo jana mahojiano hayo yamesimamishwa.

Lakini Waziri Mkuu akaonyesha kutokubaliana na maamuzi hayo ya spika na kueleza kuwa uchunguzi huo wa Takukuru utaendelea kwa kuwa ofisi ya Rais Ikulu ndio ambayo imeagiza ufanyike.

Waziri Mkuu Pinda alisisitiza kuwa kinachotakiwa kufanywa si kusitishwa kwa uchunguzi huo bali ufanyike katika maeneo yenye staha na katika mazingira ambayo hayawadhalilishi wabunge.

Mkutano huo haukuelezwa pia kama ni lini ripoti ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge itawasilishwa bungeni katika mkutano huu wa 17 hali ambayo inazidisha usiri na uzito wa mjadala kuhusu kashfa ya Richmond.

Wakati hayo yakiendelea, mbunge wa Kyela, Dk Mwakyembe aliwaambia waandishi wa habari kuwa lengo la Takukuru kuendesha uchunguzi huo ni kuwafunga midomo wabunge wasishikie bango kashfa ya Richmond.

Dk. Mwakyembe, ambaye aliiongoza kamati teuli iliyochunguza kashfa ya Richmond, alisema binafsi hawezi kukubali kile alichodai ni upuuzi wa taasisi hiyo kutaka kuwahoji wabunge katika kipindi hiki tete cha Richmond.

Dk Mwakyembe aliishangaa taasisi hiyo akiitaka ijichunguze kwanza kabla ya kuamua kuwachunguza wabunge kuhusu malipo ya posho mbalimbali, huhusan posho za chakula.

"Takukuru waliponipigia simu kunihitaji, nilikataa kwa sababu kwa mazingira yenyewe hili zoezi linaendeshwa kwa malengo ya kuwafunga midomo wabunge kuhusu sakata la Richmond mimi nilikataa," alisema.

Alisema kuwa malipo hayo ya posho yamekuwepo miaka mingi na yamekuwa yakitengewa bajeti katika fungu la kuwakirimu wageni na haoni chembe yoyote ya rushwa katika suala la malipo hayo.

Dk.Mwakyembe alisema alikataa wito huo wa Takukuru kwa kuwa ulikuwa unakwenda kinyume na haki na madaraka ya Bunge na pia ni kinyume cha vifungu 100 na 101 vya katiba ya nchi vinavyotoa uhuru kwa Bunge.

Sisi wabunge tunasubiri utekelezaji wa maazimio ya Bunge na moja ya maazimio hayo yanataka mtendaji mkuu wa Takukuru awajibishwe kwa kutofanya vizuri kazi yake katika uchunguzi wa Richmond," alisisitiza Mwakyembe.

"Alisema mchakato bado haujakamilika na wewe unaenda kuwahoji wale wanaokuhoji... hilo halikubaliki na ni kinyume cha utawala wa sheria mimi ni mwanasheria mwalimu wa sheria siwezi kukubali upuuzi huu."

Dk. Mwakyembe aliitaka Takukuru kumpeleka mahakamani kama ana makosa na kutamba kuwa hata ikifanya hivyo ataibwaga mahakamani na kusisitiza mafisadi wasitumie vyombo vya habari kumchafua.

Tukiaanza kuongelea mambo ya posho Takukuru wenyewe ndio vinara wa kutoa posho…wametufanyia semina mara mbili mimi; naishi Dar es salaam, wanatulipa posho ya kulala wajichunguze wao wenyewe kwanza, alisema.

Mwanasiasa huyo aliitaka Takukuru kuacha kukimbilia vitu vidogovidogo na badala yake ishughulikie mambo makubwa yenye maslahi kwa nchi.


akasahau kwamba hata hayo mambo makubwa huanza na madogo. hajui kwamba hakuna dhambi kubwa na ndogo, zote ziko sawa tu? halafu hawa ndio tunaosema watunge sheria zetu! for pete's sake, we must be kidding.
 
Porojo za Dk. Mwakyembe
• Atamba anajua sheria, ataibwaga TAKUKURU

na Sauli Giliard, Dodoma

MBUNGE wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, jana aliwashangaza waandishi wa habari wanaohudhuria mkutano wa 17 wa Bunge mjini Dodoma, baada ya kuitisha mkutano nao na kuhoji kwanini wanakunywa chai ya wabunge wakati wamelipwa posho na vyombo wanavyofanyia kazi pasipo kuhojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), badala ya kutoa ufafanuzi wa kama alipokea posho mara mbili au la.
Dk. Mwakyembe alihoji hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari wa Bunge, baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, wakati akitoa ufafanuzi wa kukataa kuhojiwa na TAKUKURU kuhusu kuchukua posho mara mbili kwa kufanya kazi moja.
Akizungumza kwa ghadhabu, Dk. Mwakyembe alisema kitendo cha kuhojiwa na TAKUKURU wakati huu ambapo wajumbe wa kamati iliyochunguza suala la Richmond wakitaka Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Dk. Edward Hoseah, ahojiwe, ni mbinu za kutaka kuwanyamazisha.
Dk. Mwakyembe alisema kupokea posho ni utaratibu wa siku nyingi na wa kawaida, hivyo kuhojiwa sasa ni mbinu tu ya TAKUKURU kutaka wabunge wasimhoji Dk. Hoseah.
Alisema kwa uelewa wake wa kisheria, ikizingatiwa kuwa yeye ni mwalimu wa sheria, pamoja na kubaini mchezo huo, hakukubali kuhojiwa kama alichukua posho mara ya pili katika kikao cha kamati ya Bunge kilichofanyika mjini hapa na alitamba kuwa hata kama TAKUKURU itaamua kumpeleka mahakamani, ataibwaga vibaya.
“Lunch allowances ni utaratibu wa siku nyingi na wa kawaida. Hata waziri akitembelea mikoani huwa anaandaliwa vizuri, licha ya kwamba amepewa posho. Kwani inawezekana kutomwandalia kwa sababu amekwishapewa posho?” alihoji Dk. Mwakyembe.
Aliwashangaza waandishi wa habari alipowahoji kwanini hawajawahi kuhojiwa na TAKUKURU kwa kunywa chai ya wabunge huku ikijulikana kuwa wametumwa na vyombo vyao wanavyovifanyia kazi, huku akidai kushangazwa na hatua ya wabunge kufanyiwa hivyo sasa.
Huku akilifananisha gazeti lililochapisha habari yake ya kukataa na kuomba msaada wa Spika wa Bunge, Samuel Sitta ili asihojiwe na TAKUKURU kuhusu madai ya kupokea posho mara mbili, alisema kama hilo ni kosa, TAKUKURU ndio vinara wa kutoa posho.
Alitoa mfano wa hivi karibuni katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo, ambapo licha ya kufahamu kuwa anaishi jijini Dar es Salaam, ilimpa posho ya malazi.
“Hawa TAKUKURU ndio vinara wa kutoa posho. Inafahamika mimi naishi Dar es Salaam, wananipatia posho, leo hii pamoja na mambo mengi yanayotaka majibu wanataka kutuhoji, kama hii si kuwadhalilisha wabunge ni nini?” alihoji huku akionekana kukasirika.
Mbunge huyo mara kwa mara akihusisha kitendo hicho na mchezo mchafu unaofanywa na aliowaita mafisadi. Alisema TAKUKURU imewaita wabunge kwa kutaka kuwahoji huku wao wakitaka serikali imchukulie hatua Dk. Hoseah na kwamba hilo ni lengo mahususi la kukwamisha juhudi za wabunge.
“Sisi tunataka utekelezaji wa maazimio 23 ya Bunge, mojawapo ni lile la kuhojiwa kwa viongozi wa TAKUKURU,” alisisitiza.
Dk. Mwakyembe alibainisha kwamba, kukaidi wito wa TAKUKURU wa kuhojiwa juu ya suala hilo kunatokana na kinga aliyonayo kama ilivyobainishwa katika kanuni za Bunge sehemu ile ya 100 pamoja na 101, ambayo inamlinda kama mtumishi wa chombo hicho cha kutunga sheria.
Aliendelea kujigamba kuwa kamwe hakuna mtu wa kumng’oa jimboni mwake na aliwataka wale aliowaita mafisadi waelewe kuwa hawawezi kumng’oa, labda wapige kambi kwa miaka mitano wakiwa pamoja na wake zao.
“Mafisadi kuning’oa Kyela ni kazi ngumu, labda washinde Kyela kwa miaka mitano pamoja na wake zao, ndiyo wanaweza kufanya hivyo,” alijigamba.
Alisema wakati TAKUKURU inaendelea kung’ang’ania kuwahoji, zipo hoja za msingi zinazotakiwa kujadiliwa, ikiwa ni pamoja na ile ya nani mmiliki wa Kagoda na Richmond.
Taarifa zilizotufikia kutoka ndani ya kikao cha ndani ya kamati ya wabunge wa CCM, muda mfupi kabla ya kwenda mitamboni zilieleza kuwa wabunge hao wamegawanyika kuhusu suala la kuhojiwa na TAKUKURU, baadhi wakikubaliana na hatua hiyo na wengine wakipinga na kutaka isitishwe mara moja.
Taarifa hizo zilieleza kuwa kundi la kwanza linaloungwa mkono na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, linaunga mkono hatua hiyo ya TAKUKURU, kwa hoja kwamba fedha nyingi za serikali zimepotea kwa kuwalipa posho mara mbili wabunge.
Kundi la pili linalodaiwa kuungwa mkono na Spika Sitta linadaiwa kuipinga hatua hiyo ya TAKUKURU, kwa madai kuwa inawadhalilisha wabunge.
Hata hivyo habari hizo zilidai kuwa, licha ya Spika kutaka hatua hiyo isitishwe, Pinda alitangaza msimamo wake kuwa ni lazima kazi ya kuwahoji wabunge wote wanaotuhumiwa kuchukua posho mara mbili iendelee.
Wakati huo huo, hatima ya kujadiliwa kwa hoja ya Richmond bungeni bado ni tete, hadi sasa hakuna taarifa zozote za iwapo wabunge watafanya hivyo.
Pamoja na sakata hilo la Richmond, mambo mengine ambayo bado haijabainika iwapo nayo yatajadiliwa ni pamoja na Kampuni ya Reli (TRL), TICTS na mgodi wa makaa ya mawe, Kiwira.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari Mkuu wa Bunge, Ernest Zulu, alisema masuala hayo yaliyopewa kipaumbele kuwa yatajadiliwa katika mkutano wa 17 wa Bunge unaoendelea mjini hapa, kwa sasa yapo chini ya kamati husika hadi hapo watakapowasilisha taarifa zake kwa Spika.
“Kwa sasa kamati hizo bado zinapitia taarifa zao, wakishawasilisha bungeni ndipo itajulikana kama watajadili au hawatajadili,” alisema Zulu.
Hata hivyo alisema kuna uwezekano wa Bunge kuongezwa siku mbili zaidi badala ya kumalizika Novemba 6, likaisha Novemba 8.
Zulu alisema katika kikao hicho kutawasilishwa hoja tatu.
Watakaowasilisha hoja hizo ni Mbunge wa Longido, Saning’o ole Telele (CCM) anayelalamikia ukiukwaji wa haki za binadamu kwa wafugaji waliohamishwa kwenye maeneo yao na wawekezaji. Mbunge mwingine atakaetoa hoja binafsi ni Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA), Halima Mdee, ambaye anataka ufafanuzi wa jinsi Kiwanda cha Tanganyika Packers kilivyobinafsishwa. Mwingine ni Lazaro Nyalandu, Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), ambaye hoja yake binafsi ni kutaka masuala ya dini yasijadiliwe bungeni.


h.sep3.gif


juu
blank.gif
blank.gif


Hakuna sheria inayotetea upumbavu!!!!! yaani kwa vile yeye ni mwanasheria ndiyo maana anataka kukomaa hata mahala pasipostahili? anyway, naogopa kusema kwa sababu watasema nimesema! bora ninyamaze miye mwana wa mwenzenu, maana hawakawii hawa....
 
Back
Top Bottom