Polisi wetu wanapeleleza au wanahoji kesi?

Mulama

JF-Expert Member
Apr 16, 2011
3,018
1,791
Nimeona niulize kwenu wana jf suala hili la jinsi polisi wa nchi hii wanavyoendesha kesi za jinai,
Utaona polisi anakamata au analetewa mtuhumiwa kituoni na kumuweka ndani yaani mahabusu kasha kesho yake au baadae atamtoa na kuanza kumuhoji maswali huku akinakili majibu ya mtuhumiwa. Zaidi ya hapo san asana ataenda na mtuhumiwa sehemu anakoishi au alipokamatiwa na kupekuapekua juu juu halafu jalada linakuwa tayari kupelekwa mahakamani.
Je hatua hizi mnadhani zinatosha ku establish kosa la mtuhumiwa na kujenga merit ya kesi mahakamani?
Nawasilisha
 
kutokana na maelezo yako hapo juu hatua hizo hazitoshi kabisa kujenga kesi mahakamani, lakini tukumbuke kuwa polisi wanaujuzi mdogo sana kuhusu criminal laws and procedures ata sheria ya ushaidi na yenyewe hawana ujuzi nayo sana, since there not trained as lawyers, iliushinde kesi ya jinai procedures nyingi za kisheria zinakuwa involved ambapo nikizielezea hapa zitachukua muda mwingi. na kwa jinsi ulivyoeleza ndio maana unakuta mashitaka yanayoendeshwa na polisi katika mahakama za mwanzo, mengi jamhuri uwa inashindwa kuprove kosa.
 
Ahsante mkuu kwa mchango wako mzuri.
sasa tufanyeje au nini kifanyike ili wawe wapelelezi na kuweza kkuondoa raia kukata tamaa na kujichukulia sheria mkononi?
 
ningeshauri kuwa serikali iwaajiri waendesha mashitaka ambao kimsingi sio polisi wawe na nguvu yakuendesha mashitaka katika mahakama za mwanzo,hii itasaidia kupunguza mzigo kwa polisi maana wanachunguza wao na wanaprosecute case wao na vile itasaidia kufanya kesi ziwe znatolewa maamuzi haraka pili, raia waelimishwe juu ya haki na sheria zilizopo kuhusu makosa ya jinai why? basically kila binadamu ana haki za msingi ambazo lazima zieshimiwe mfano kwa mshitakiwa ana haki ya kupata dhamana, sasa unakuta mtu kashikwa asubuhi akaweza kujiwekea dhamana jioni akawa mtaani, wananchi wanaanza ooh, polisi wameongwa wamwachie kumbe hapana ni haki ya huyo mshitakiwa.
 
Back
Top Bottom