Polisi wetu ni wana CCM?


Rule no 1 kama wewe ni mfanyakazi wa serikali na unaingia kwenye chama jiengue kwanza serikalini na ndio uje kwenye chama.

Sasa nataka kuuliza kombe still ni police na kama ndio aachane na upolice kwanza na ndio ajiunge CCM,

Na kama alisha staaafu upolice ni lini alijiunga CCM?
kwani inastahajabisha sana mapema tu anatangaza nia na ni majuzi tuu alikuwa kamanda wa Trafiki nadhani kama sijakosea iweje leo wananchi wa eneo husika ati wamekuomba ugombeee?

Kwa Tibaigana naweza kidooogo nae nika muhoji Uzoefu wake kwenye siasa ni wa muda gani? na ni lini nae alikuwa/kajiunga kwa chama "CCM"? maana nimekuwa na watoto wake na wameoa nao, nasija wahi mwona Tiba kwenye Siasa Tokea naanza mfaahamu huko msoma, Singinda, Tanga, Dodoma na hapa Dar?

 
Makamanda wote wa vyombo vya ulinzi ni wanachama,washabiki na wapenzi wakubwa wa CCM. Tukumbuke kuwa hawa ndiyo vitendea kazi vya CCM katika kuwadhibit wapinazani.Kule Pemba mwaka 2001 walioua wanachma wa CUF si polisi hawa hawa? Hivyo wanapostaafu lazima wapozwe kwa kuingizwa kwenye ulaji kwa kofia ya siasa.
 
Jambo la msingi hapa ni kuona jinsi wastaafu hao wasivyo waadilifu na pia kukosa haya katika jamii. wangesubiri kidogo kuthibitisha kwamba wameanza kujihusisha na siasa baada ya kustaafu kwa kuwa lazima wajipange.
Kulingana na maadili ya kazi zao, walitakiwa wasijihusishe na siasa, lakini leo tunawaona wakitangaza nia za kugombea muda mfupi tu baada ya kustaafu.
Huo ni uthibitisho kwamba walikuwa wakijihusisha na siasa wakiwa ofisini, hivyo siyo waadilifu na ni sababu tosha ya kutoa pingamizi ndani ya chama wanachotangazia nia na pia kama wakipitishwa pingamizi litolewe kwenye tume.
Naamini maamuzi yasyo ya kinafiki yatawaondoa, labda itashindikana tu kama walipokuwa ofisini viongozi watoa maamuzi walikuwa wanapata maslahi binafsi toka kwao na hivyo kuwalipa fadhila!
Nawashauri washindani wao wajiandae kwa mapingamizi kwa hoja ndani ya vyama na kwenye tume hata kama watafanyiwa mizengwe lakini watakuwa wametoa somo kwa wengine.
 
jamani hapa shida Yangu ni hii, Jeshi la wananchi wa Tanzania linasema, Kiongozi kuanzia meja na kuendelea, akistaafu ni lazima akaee not less than 2 good years without involvement in politics. Nadhani inaweza kuwa hivyo kwa polisi(sina hakika). Ila hapo lazima watakuwa makada na kutimiza malengo ya chama chao wakiwa kazini.
 
Pasco asante sana kwa kutuweka sawa kuhusu hili. Nimekuelewa vizuri lakini si unaona umuhimu wa sheria hizi haupo? Imewekwa kama kiini macho. Nadhani unaelewa ninamaanisha nini maana ukiangalia kuna sababu nyingi za kuniaminisha hivyo.
 


...Tatizo ni wao wenyewe sio sisi. Sentensi yako ilipaswa kuwa...'wajistaafie wenyewe kwa heshima'! (Ondoa hiyo 'tuwaachie'! Sisi hatuhusiki na maamuzi yao!)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…