richaabra
JF-Expert Member
- Jul 12, 2016
- 1,472
- 3,535
Dodoma. Haieleweki kama ni kutokana na tishio la Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) au ni mabadiliko ya kawaida,mPolisi wameamua kuweka ulinzi mkali mjini hapa.
Jana, Kamati Kuu ya CCM ilifanya kikao kwenye jengo la makao yake makuu maarufu White House, ambalo lilikuwa na ulinzi mkali wa polisi wenye sare, askari kanzu, askari wa kikosi cha mbwa, hali iliyofanya mtu asiyehusika kupenyeza maeneo hayo kuwa ngumu tofauti na ilivyozoeleka.
Magari yaliyobeba askari polisi, vikosi vya mbwa na maofisa Usalama wa Taifa walionekana kutanda maeneo yote kuzunguka jengo hilo lililopo Barabara Kuu, katikati ya mji wa Dodoma. Mapema wiki hii, mkuu wa mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana alitoa tahadhari kwa mtu yeyote anayetaka kufanya vurugu, akisema wamejiandaa vizuri kukabiliana nao.
Jana, Kamati Kuu ya CCM ilifanya kikao kwenye jengo la makao yake makuu maarufu White House, ambalo lilikuwa na ulinzi mkali wa polisi wenye sare, askari kanzu, askari wa kikosi cha mbwa, hali iliyofanya mtu asiyehusika kupenyeza maeneo hayo kuwa ngumu tofauti na ilivyozoeleka.
Magari yaliyobeba askari polisi, vikosi vya mbwa na maofisa Usalama wa Taifa walionekana kutanda maeneo yote kuzunguka jengo hilo lililopo Barabara Kuu, katikati ya mji wa Dodoma. Mapema wiki hii, mkuu wa mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana alitoa tahadhari kwa mtu yeyote anayetaka kufanya vurugu, akisema wamejiandaa vizuri kukabiliana nao.