Polisi wavamia hotel ya Blue Pearl na kumkamata Mkurugenzi wa (THRDC) Onesmo Olengurumwa

Friday Malafyale

JF-Expert Member
Jan 18, 2017
1,811
2,916
4e02c3af0ee75bfa3f5a93056aae0cf6.jpg


Niko hapa maeneo ya Ubungo Plaza nikiwa nimejiandaa vema kuhudhuria tukio la uzinduzi wa kitabu cha ndugu uyetu Alphonce Lusako ghafla naona magari ya polisi matatu lingine likiwa limepaki kwa mbali.

Hapa nilipo imenibidi nijifanye mpita njia maana wamemkamata Mkuregenzi wa kituo cha utetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) Ndg, Onesmo Ole Ngurumwa pamoja na ndugu Baraka, wamechukuliwa hapa Blue Pearl na Police.

Wanaelekea kuhojiwa na OCD Kituo cha polisi Magomeni.

========
Kitabu kilichotaka kuzinduliwa kinaitwa Sauti ya Watetezi wa Haki Vyuoni.

IMG-20170603-WA0005.jpg


Onesmo Olengurumwa ameachiwa kwa dhamana jioni ya leo.
 
Niko hapa maeneo ya ubungo plaza nikiwa nimejiandaa vema kuhudhuria tukio la uzinduzi wa kitabu cha ndg yetu Alphonce lusako ghafla naona magari ya polisi matatu lingine likiwa limepaki kwa mbali, hapa nilipo imenibidi nijifanye mpita njia maana wamemkamata Mkuregenzi wa kituo cha utetezi wa Haki za binadamu (THRDC) ndg Onesmo Olengurumo pamoja na ndugu Baraka, wamechukuliwa hapa Blue Pearl na Police. Wanaelekea kuhojiwa na OCD Kituo cha polisi Magomeni... Rwanda ya kagame on WORK
Kwani hicho kitabu kinahusu nini? Kama kimegusa maslahi ya wakubwa unategemea nini!...
 
Haya sawa lkn sio hivyo kumbuka udikteta haukuanza hivi hivi
Kilichonishtua ni kwamba, kwanini wavamie kuzuia uzinduzi wa kitabu? Je, kitabu hicho kinahusu nini? Na nani kawapa taarifa kuhusu uzinduzi huo? Hasa ni maswali naamini yeyote anaweza kujiuliza, bila kujali ni udikteta au la...
 
Back
Top Bottom