WATU tisa wakiwamo askari polisi wawili wa Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam wametiwa mbaroni wakiwa na meno 70 ya tembo (sawa na tembo 35).
Kamanda Matei alifafanua kuwa meno hayo yana uzito wa kilo 305, yakiwa na thamani ya sh 850,500,000, huku akitoa wito kwa wananchi kuwafichua watu wanaojihusisha na vitendo vya ujangili ili wachukuliwe hatua bila kujali nyadhifa zao.
BY Mwananchi.co.tz 30,Julai,2013
Kisarawe: Watu Tisa wawili kati yao wakiwa polisi wa kituo cha Oysterbay. Dar es salaam wamekamatwa Wilayani Kisarawe , mkoani Pwani kwa tuhuma za kukutwa wakisafirisha Meno 70 ya Tembo (kilo 305) kinyume na sheria. Meno hayo kwa hesabu ya Kawaida ni sawa na Tembo 35, wameuwawa! na Thamani yake ni Tsh 850 Milioni.
'' Mwisho wa Kunukuu''
NB: Habari hii kwanza inasikitisha sana. Sijui nchi inakokwenda na hawa ni wachache wanaoshikwa je ambao hawajashikwa?!!! Ukiangalia hesabu hiyo iliyowekwa na mwandhishi yaani Tembo 35 Kwa siku moja inatisha.
Kuna Tasmini moja niliwahi kusikia Clouds Radio kwamba Nchi ina wastani wa kama tembo 7,000 hivi. Sasa Tukichukua 7000 gawanya kwa 35 tunapata 200Days.
So kama tukisema kila siku tembo wauwawe kwa kiasi hicho hapo juu ina maana ndani ya siku 200 Tembo wote Tanzania watakuwa wameisha!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Inatishaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!
Ooooh Mwalimu Nyerere Baba unaweza kufufuka hata uje ukae mwezi mmoja tu uwachape watu vile viboko vyako 12 kabla ya kwenda jela na 12 siku ya kutoka jelaaa?
polisi polisi polisi
Kuua Binadamu - polisi
Kutesa watu - polisi
Kurusha mabomu - polisi
Kuua tembo - polisi
Kuua na kubambikiza mtu kichwa cha binadamu - polisi
Kuficha/kushirikiana na wauza mihadarati - polisi
And yet, waziri mwenye dhamana nao yupo ofisini anadunda!!!!!!!!!!!!!
WATU tisa wakiwamo askari polisi wawili wa Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam wametiwa mbaroni wakiwa na meno 70 ya tembo (sawa na tembo 35). ...........
Kamanda Matei alifafanua kuwa meno hayo yana uzito wa kilo 305, yakiwa na thamani ya sh 850,500,000, huku akitoa wito kwa wananchi kuwafichua watu wanaojihusisha na vitendo vya ujangili ili wachukuliwe hatua bila kujali nyadhifa zao...
Katika hatua nyingine, mkazi wa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam, Ibrahim Mnyanga (58) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na vipande 16 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilogramu 24.5 ....