Waliokamatwa sio wahusika wa PEMBE ZA NDOVU (SIYO MENO) maana wao kwa vyovyote walitumwa na BOSI wao watekeleza kazi hiyo kwa vyovyote huwa wanapewa kitu kidogo.
Kamanda husika wa askari hao anahusika maana anajua ni eneo gani askari wake walipopangwa siku husika, ahojiwe kwa mapana, pia gari husika na wale watu tisa wataje nani kawatuma.
Kiasi cha milioni 15 walizotaka kuhonga walizitoa kwenye akaunti gani kama ni askari wacheki akaunti zao au wale tisa akaunti zao zichekiwe kujua pesa zinavyoingia na kutoka.
Jeshi la Polisi halina tena WELEDI ni muda muafaka sasa kuanzia IGP, KANDA MAALUM DSM, KANDA ZA MIKOA makamanda wajiuzulu kwa ushiriki wao wa moja kwa moja kwenye ujambazi.
Aidha tumpongeze kamanda wa Mkoa wa Pwani kwa kukataa kupokea Rushwa ya hayo majangili.
Tunasubiri Waziri NCHIMBI,akishirikiana na CHAGONJA, KAMUHANDA kutupatia majibu