Nilifikiri kuwa wewe ni mwandishi nguli kumbe nawe una siasa za rejareja hivi.Naunga mkono hoja, Scotland Yard waitwe kusaidia, hata BOT ilipoungua, polisi wetu walishindwa hivyo Scotland Yard waliitwa. Na rushwa ya Rada ya BAE pia tulishindwa Waingereza wenyewe wakafanya kila kitu, hadi aliyehonga akakiri kuhonga ila akaomba asitoe majina bali alipishwe tuu faini kwa non disclosure na ndio hiyo cheji ya rada.
Hata kampuni ya Kagoda iliyokwapua bilioni 40 za EPA tumeshindwa kuichunguza hadi kesho, hivyo ni kweli tuombe msaada watusaidie na hata suala la MV Bagamoyo wanaweza kusaidia!.
Paskali